Imani ndio itamuokoa mtu na sio dini.
Huh hivi kwani dini ni nini? Iman ni nini? Ningependa kujua mtazamo au ufaham wako kuhusu hili.
Navyojua mie Dini ni mfumo na mwenendo wa Maisha. Kuanzia unakula vipi, unazungumza vipi, unatembea vipi, malezi kwa ujumla, utafutaji rizki na so sooo... kwamba mfumo mzima wa maisha ndio dini yenyewe. Na pale inaposemwa kuna dini nyingi duniani upande wangu naelewa kuna mifumo mingi ya maisha duniani. Kuna mifumo ya kiislam (Unyeyekevu), kuna mifumo ya kikristo, kipagani n.k
Then, Imani... Kwa ufaham wangu mimi ni kusadiki au kua na hakika ya mambo yanayoonekana na yasioonekana. Vile katika hili kuna Imani tofauti tofauti sana. Nitolee mfano Aina za Imani zinazofanana na tunacho kiongelea hapa. Imani ya Kiislam na Imani ya Kikristo.
Hua nshangazwa mtu anaposema toa mambo ya kidini hapa? How akati dini ni mfumo na mwenendo wa Maisha. Kwanini mtu huyo asiseme toa mambo yako ya kiimani hapa. Au kwanini isiwe mfia Imani iwe mfia dini? Kwani kiini cha mtifuano kipo kwenye Imani sio kwenye mienendo ya Maisha na kama ipo basi ni michache.
Nimesema haya kwasababu naona kama ni vitu viwili ambavyo vinatumika isivyo sawa kimazoea. Hivi viwili vinaweza kua pamoja au visiwe pamoja.
Kuna watu hawana Imani, yaani hawaamini katika yasio onekana ila wanaendesha maisha yao kwa kufata moja ya mifumo ya miasha iliyopo either ya Kiislam, Kikristo au mengineyo.
Kuna watu wana Iman ya Kiislam ila wanaishi kwa kufata mfumo wa Kikristo na kuna watu pia wana Iman ya Kikristo ila wanaishi kwa kufata mfumo wa maisha ya kiislam. Au pia unakuta wana imani za kiislam au kikristo ila wanaishi kipagani.
Kuna mda naonelea kutoelewa maana ya halisi ya vile tunavyozungumza inatosha kuchochea huu mkanganyiko uliopo... Na mkanganyiko uliopo hauwezi kutoka kamwe kama mtu hayupo radhi kujifunza kitu kipya hata kama kikiwa tofauti na kile ambacho tayari keshajifunza.
Hivi kuna mtu alishawah waza kwa nafasi yake vipi kama kila kitu unachofaham hadi leo hii ni Uongo na hakipo?