Kwanza nieleweke jambo moja, binafs katika vitabu sina kitu kinaitwa biblia bali injili. Hata katika nguzo ya tatu ya Iman inayosema kuamini vitabu vyake naamin katika injili sio biblia.
Vitabu vyote havipingani bali vinasadikishana. Mfano ni pale Mwenyezi Mungu mtukufu aliposema katika Suratul Baqarah aya ya 87 na 136.
Hapa nitanukuu Tarjama peke yake
87. Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukafuatisha baada yake Mitume wengine. Na tukampa Isa, mwana wa Mariamu, hoja zilizo waziwazi, na tukamtia nguvu kwa Roho Takatifu. Basi kila walipo kufikieni Mitume kwa yale ambayo hayapendwi na nafsi zenu, mlijivuna; wengine mkawakanusha, na wengine mkawauwa.
136. Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.
So hapo nimeanza kukuelezea hayo ili usinihusishe na Biblia, na sina hakika kama kuna Muislam anayeijua dini yake vizuri akasema anaiamini biblia bila kukufuru. Ni biblia ndio inaongelea utatu wa Allaah, ni Biblia inayosema Yesu ni mwana wa Mungu, ni Biblia ndio inasema Yesu ni Mungu, So mie kama Muislam hicho sio katika kitab changu kwani kinapingana na vitab vingine bali Injili iliyoshushwa kwa Issa mwana wa Maryam ndio kitabu changu.
Kwani Injili haisemi yote hayo bali inasema kua yeye Issa A.S ni mtume aliyeletwa katika zama zake kufundisha watu wamuabdu mwenyezi Mungu mmoja kama ilivyo kwenye vitab vilivyo tangulia na Quran iliyokuja baada yake. Kwasababu vitabu vya Allah mlezi havipingani bali vinasadikishana.
Mwisho nimalizie kwe hoja yako,
Maelezo yangu juu kwenye reply ile ni katika kutaka kukuonesha mafundisho yanayoongelea vitabu hivi vya dini namna yanavoweza kuzua mkanganyiko kwa kutoa mfano wa mafundisho yaliyopo yanayohusu watoto wa Adam A.S.
Kama nilivyomjibu
FaizaFoxy binafs hua sipendelei kujihusisha na jambo ambalo nahisi lina uwalakini. Hasa hasa yanahusu Historia ya zama zilizopita.
Nimejikita katika kujenga Iman yangu tu, kumjua na kumuabudu alieniumba tu kwa kuhakikisha nampwekesha vile anavyohitaji ila sio zile za Nabii flan anaitwa flan au alipaswa kufanya hivi au alifanya hivi na vile kwani hua naona havina uzito katika lengo aliloniumbia Mola wetu mlezi.
That's why na kusoma kwangu kooote yaliyomo kwe huu uzi, cha kwanza na nilitaraji kingekua cha mwisho kureply ilikua ni ile post ya
Etugrul Bey alipoteleza kwa kusema kua malaika ni wasaidizi wa Allaah mtukufu.
Wish you kheri bi idhn Llah