Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Hata swala Adam kuwa binadamu wa kwanza lipo kwenye Biblia, waandishi wa Quran walisahau kucopy.
hapana. watafsiri ndio walikolitoa huko. Adam wa kwenye Qur'an na kisa cha Adam wa Qur'an ni tofauti kabisa na Afdam wa biblia. Kwenye Qur'am mimi na wewe na wengine wengi ni Adam pia.

Msome Arsis kaanza kuchambua ni nini Adam kwenye Qur'an, ndio, ni nini, sio ni nani.
Simba.
 
alafu huyu Arsis huko post za nyuma alisema biblia ni kitabu cha wagiriki..nyie kama wakristo mnasemaje kuhusu hilo embu mbane Arsis atupe majibu kuhusu biblia ni kitabu cha wagiriki kivp yaan?
Swali zuri sana, ukweli ni...
Kwa sababu hakuna mtume yeyote aliekuja na Biblia. Hata neno Biblia ni la Kigiriki. Hata ndani ya bilia hakuna neno biblia kwenye aya hata moja ya biblia.
Simba.
 
ASILI YA MAJINI --2
Baada ya kuona kuwa majini wameubwa kwa moto kwa mujibu wa quran nije katika hadithi za bwana mtume muhammad swalalah alaiy wasalam.
Aisha (RA) alieleza kwamba Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Malaika waliumbwa kutokana na nuru, majini waliumbwa kutokana na moto na Adamu aliumbwa kutokana na kile kilichoelezwa kwenu."
عن عائشة رضي الله عنه قالت: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «خُلقت الملائكة من نور، وخُلق الجَانُّ من مَارِجٍ من نار، وخُلق آدم مما وُصِفَ لكم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
Hadthi hii ni sahihi na imepokewa na muslim, Katika hadithi hii tumeona kuwa Malaika wameumbwa kutokana na nuru , majini kutokana na moto na wanadamu kutokana na kile tulichoelezwa kwa maana hapa mtume alisha waeleza kuwa mwanadamu kaumbwa kutokana na udongo.
Hivyo hakuna shaka kuwa asili ya majini ni mwale wa moto. Tuje katika melengo yao kwanini majini wameumbwa?

LENGO LA KUUMBWA MAJINI.
Imetajwa katika Quran kuwa lengo la wanadamu na majini kuumbwa ni kumuabudu Allah. Kama ilivyokuja katika quran (Adh-Dhariyat 51:56)
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ -- sikuumba majini na watu ila waniabudu.

Hapa tunaona kuwa lengo kuu la kuumbwa majini na sisi wanadamu ni kumuadu Allah, swali linakuja ikiwa ilo ndio lengo la kuumba mbona majini na wanadamu tunafanya mambo ya kumkufuru mungu nadhani umesoma katika kisa cha bwana simba mabalaa ya majini jinsi wanavyokata majii(kunywa pombe), wanavyofanya uchawi na mabalaa mengine, Kuhusu wanadamu apo bwana Battor unajua mabalaa ya mwanadamu uzinzi, wizi, rushwa, chuki, uongo, dhulma, zinaa, mauaji, kukata undugu, kusengenya, ushoga, utapeli n.k kwanini yote haya na Allah anasema lengo ni kumuabudu yeye?
Quran inajibu kwa kusema katika surah Al-Insan (76:3) ''Hakika Sisi tumemwongoza katika njia. Ikiwa atashukuru au akufuru."
إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا
Hapo wamezungumzwa wanadamu kuwa muongozo upo na njia ni mbili tu ushukuru au kukufuru na majini pia imeelezwa katika surat jinn kuwa kuna kundi la majini lilisikia quran nalikakiri kuwaa ni ya ajabu na inaongoza katika haki na hawatamshikisha mola wao.
"قُلْ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ اسْتَمَعَ نَفَرٌ مِّنَ الْجِنِّ فَقَالُوا إِنَّا سَمِعْنَا قُرْآنًا عَجَبًا * يَهْدِي إِلَى الرُّشْدِ فَآمَنَّا بِهِ وَلَنْ نُشْرِكَ بِرَبِّنَا أَحَدًا"
Lakini pia katika aya ya 11 ya surat jiinn inasema

''وَأَنَّا مِنَّا ٱلصَّـٰلِحُونَ وَمِنَّا دُونَ ذَٰلِكَۖ كُنَّا طَرَآئِقَ قِدَدٗا'' -- Na hakika miongoni mwetu wapo walio wema, na miongoni mwetu wapo kinyume na hivyo; tulikuwa njia mbalimbali.
Hapa utaona kuwa majini wenyewe wanasema kuna wema na wabaya hivyo suala linabaki kwa mwanadamu au jinn kuchagua njia ya kufuata na watakao mtwii Allah malipo yao ni pepo na watakao kufuru na kumuasi ALLAH ni motoni kama ilivyo katika quran
"قَالَ ادْخُلُوا فِي أُمَمٍ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِكُم مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ فِي النَّارِ"
(Allaah) Atasema: Ingieni motoni pamoja na ummah zilizokwishapita kabla yenu miongoni mwa majini na wana Aadam”. [Al-A’araaf: 38]

Toka nimeanza kuelezea mpaka hapa kuna mambo utagundua kuwa kwa mujibu wa uislamu:-
  • Malaika wameumbwa kwa nuru, Majini kwa moto na wanadamu kwa udongo
  • Lengo la majini na wanadamu ni kumuabudu Allah.
  • Watako fanya kinyume na kumuabudu Allah malipo yao ni Moto.
Hivyo basi, Ushirikiano wowote wa mwanadamu na majini katika kumuasi Allah ni makosa na imekatazwa katika uislamu hilo halina mjadala, ni KUFRU.
Mjadala unabaki Je ni sahihi mwanadamu na majini kushirikiana katika wema mfano bwana Arsis alivyoshirikiana na Simba katika kumuokoa msukule huko unguja na mifano kama hiyo Je yafaa?
Inshaalah, Nitalieleza pia kwa kadri ninavyoelewa, Hapa hapataki muhemko maana pana mambo mtu anaweza ona yafaa kumbe haifai na mengine kuona hayafai kumbe yafaa.
Nitarudi kuelezea maisha ya majini, kuzaana kwao, tabia zao, na kubwa zaidi kwanii wanasumbua wanadamu.
Arsis anasema anangoja umalize atarudi kuja kuchambua, kwani kisa cha adama kinaendana sambamba na majini, mtakiona anavyoendelea na kisa cha adam, na atakuja kujibu hizi post zako.

Mwaga elimu.
Simba.
 
Binafsi naona suala la Majinni linaenda sambamba na suala la Adam.

Kwa mtazamo wangu zote ni lebo tu.

Naomba juuliza swali, kwako au yeyote yule anaweza kujibu, ikiwemo Arsis.

Hivi ni nini tofauti ya Iblis, afrit, jinni, jaan, insan, bashar, shetan, adam, Khalifa, malaika, ruh, nafs qareen, nabii, rasul?

Yote hayo yapo kwenye Qur'an.
Naam, Nitajaribu kuweka katika mpangilio ambao unaweza lete mtiririko mzuri nitaanza na Jinni

JINNI - Ni kiumbe wa Allah aliyeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah, Wameumbwa kwa moto na wanauwezo wa kuchagua kufanya mema au maovu, sawa na wanadamu.
Wanaulimwengu wao ambao wanadamu hatuwezi kuwaona labda mpaka ufunguliwe macho kama bwana Simba. Wapo wema na wabaya lakini wana maisha simple compared na mwanadamu yaani wengi katika majini ni waasi wanafanya mabalaa sana habari zao kwa undani zipo katika Quran Surat jinn lakini pia Quran 51:56, 6:128.

INSAN - Huyu ni mwadamu ameumbwa kwa madhumuni maalum ya kumuabudu Allah na kuwa khalifa duniani, Kama walivyo majini basi na wadamu wana uhiari wa kufanya mema au maovu. Habari za mwanadamu zimejaa katika quran.
Kuhusu uumbwaji wake 23:12 -14 Inaeleza malengo ya kuumbwa kwake 51:56 Inaeleza.
Mpaka hapa utaona viumbe ambavyo vimeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah na wana uhiari ni majini na wanadamu ndio maana hukmu siku ya malipo ni kwa ajili ya majini na wanadamu tu.

IBLIS - Huyu ni katika majini, Ndiye aliyekataa kumsujudia Adam, na akafukuzwa katika rehma za Allah, Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa Iblis anawadanganya sio wanadamu tu bali hata majini wenzake.
Majini kwakuwa wanaweza kuwa wema au wabaya basi iblis huwa anawadanganya majini wenzake wamuasi Allah kisha anawatuma waje kuwadangaja wanadamu pia, Hivyo kuna majini wengi tu hawaijui haki kwasababu Iblis anawachezea kwa kuwalaghai.
Imeelezwa katika hadithi kuwa iblis ana kundi kubwa la wafuasi na anawatuma kila siku kuwafarakanisha wanadamu

عَنْ جَابِرٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ: «إِنَّ إِبْلِيسَ يَضَعُ عَرْشَهُ عَلَى الْمَاءِ ثُمَّ يَبْعَثُ سَرَايَاهُ فَأَدْنَاهُمْ مِنْهُ مَنْزِلَةً أَعْظَمُهُمْ فِتْنَةً. يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ فَعَلْتُ كَذَا وَكَذَا فَيَقُولُ: مَا صَنَعْتَ شَيْئًا. ثُمَّ يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ: مَا تَرَكْتُهُ حَتَّى فَرَّقْتُ بَيْنَهُ وَبَيْنَ امْرَأَتِهِ، فَيُدْنِيهِ مِنْهُ وَيَقُولُ: نِعْمَ أَنتَ»

Tafsir : Kutoka kwa Jabir, alisema: Mtume Muhammad ﷺ alisema: "Hakika Iblisi huweka kiti chake juu ya maji kisha anatuma vibaraka wake. Yule ambaye anaonekana kuwa karibu naye zaidi ni yule ambaye anafanya maasi zaidi. Mmoja wao huja na kusema: ‘Nimefanya hivi na hivi,’ naye (Iblisi) husema: ‘Hujafanya chochote.’ Kisha mwingine huja na kusema: ‘Sikumuacha mpaka nilipomtenganisha yeye na mkewe,’ naye (Iblisi) humkaribisha karibu naye na kusema: ‘Wewe ni mbora''
Hapo utaona jinsi Iblis anavyowatuma majini kufanya mabaya lakini pia Wanadamu wapo wanaomuabudu huyu Iblis.

SHETANI - Hii ni sifa ya kiumbe muovu katika majini na wanadamu hivyo jinni au mwanadamu akiwa muovu anakuwa shetani ingawaje katika quran kuna aya nyingi zinataja shetani zikimaanisha Iblis hii ni kwa sababu Iblis aliaswi na akahukumiwa moto na lengo lake nikutafuta kundi kubwa katika majini na watu wa kwenda nae motoni hivyo Iblis ni shetani moja kwa moja, Jinni na mwanadamu wanaweza kuwa mashetani kwa vitendo vyao vya kufru. Nawaweza wasiwe mashetani kwa wema wao na uchamungu.
Ndio maana kabla ya kuanza kuosoma Quran tunataka hifadhi kwa Allah kutokana na shatani kwa maana wabaya wote katika watu na majini na Iblis mwenyewe Allah atukinge kwao.

Nitaendelea Inshaalah.
 
Sio Qur'an inahitilafiana, wanahitilafiana mmaulamaa na tafsiri.

kama mada ya Adam inaoendelea humu, wapo wanasema Adam ni mtu wa kwanza n ammoja tu wapo maulamaa hilo hawalikubali, sasa tuisome Qur'an mwenye ushahidi wa Qur'an ndio mshindi au sio? Si uliona Arsis kapandisha video clip ya Alim mkubwa sana anasema Adam wapo wengi ttena aliisitiza kwa Kiarabu :kathiiiir".

Na wewe si ulikua unahitilafiana na hilo au sasa umeshakubali kua Afam hatajwa kua ni mtu wa kwanza kuumbwa ndani ya Qur'an?
Simba.
Hapana msimamo wangu mpaka sasa Adamu ni binadamu wa kwanza kulingana na nilivyosoma mimi na uelewa wangu wa quran na wanzuoni wanavyosema.
Suala la wanazuoni wanaosema Adamu sio binadamu wa kwanza nilikubali lipo ila mpaka sasa hoja za wamaosema Adamu ndio wa kwanza nazielewa zaidi, Ndio maana nasisitiza Arsis aendelee na Mada ya Adamu huenda nikaona kitu kipya au akatoa hoja zenye nguvu, Ila msimamo wangu ni kuwa Adamu ni binadamu wa kwanza kuumbwa kulingaana na hoja nilizozitoa na wachangiajiwengine walivyotoa. Kuna sehemu nasubiri Arsis afike hapo tutakuwa tunatafuna Muwa kwenye fundo.
 
Hapana msimamo wangu mpaka sasa Adamu ni binadamu wa kwanza kulingana na nilivyosoma mimi na uelewa wangu wa quran na wanzuoni wanavyosema.
Suala la wanazuoni wanaosema Adamu sio binadamu wa kwanza nilikubali lipo ila mpaka sasa hoja za wamaosema Adamu ndio wa kwanza nazielewa zaidi, Ndio maana nasisitiza Arsis aendelee na Mada ya Adamu huenda nikaona kitu kipya au akatoa hoja zenye nguvu, Ila msimamo wangu ni kuwa Adamu ni binadamu wa kwanza kuumbwa kulingaana na hoja nilizozitoa na wachangiajiwengine walivyotoa. Kuna sehemu nasubiri Arsis afike hapo tutakuwa tunatafuna Muwa kwenye fundo.
Unaweza kutupa ushahidi wako wa kwenye Qur'an?

Au wewe unafata hoja za watu badala ya Qur'an?
Simba.
 
Naam, Nitajaribu kuweka katika mpangilio ambao unaweza lete mtiririko mzuri nitaanza na Jinni

JINNI - Ni kiumbe wa Allah aliyeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah, Wameumbwa kwa moto na wanauwezo wa kuchagua kufanya mema au maovu, sawa na wanadamu.
Wanaulimwengu wao ambao wanadamu hatuwezi kuwaona labda mpaka ufunguliwe macho kama bwana Simba. Wapo wema na wabaya lakini wana maisha simple compared na mwanadamu yaani wengi katika majini ni waasi wanafanya mabalaa sana habari zao kwa undani zipo katika Quran Surat jinn lakini pia Quran 51:56, 6:128.

INSAN - Huyu ni mwadamu ameumbwa kwa madhumuni maalum ya kumuabudu Allah na kuwa khalifa duniani, Kama walivyo majini basi na wadamu wana uhiari wa kufanya mema au maovu. Habari za mwanadamu zimejaa katika quran.
Kuhusu uumbwaji wake 23:12 -14 Inaeleza malengo ya kuumbwa kwake 51:56 Inaeleza.
Mpaka hapa utaona viumbe ambavyo vimeumbwa kwa lengo la kumuabudu Allah na wana uhiari ni majini na wanadamu ndio maana hukmu siku ya malipo ni kwa ajili ya majini na wanadamu tu.

IBLIS - Huyu ni katika majini, Ndiye aliyekataa kumsujudia Adam, na akafukuzwa katika rehma za Allah, Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa Iblis anawadanganya sio wanadamu tu bali hata majini wenzake.
Majini kwakuwa wanaweza kuwa wema au wabaya basi iblis huwa anawadanganya majini wenzake wamuasi Allah kisha anawatuma waje kuwadangaja wanadamu pia, Hivyo kuna majini wengi tu hawaijui haki kwasababu Iblis anawachezea kwa kuwalaghai.
Imeelezwa katika hadithi kuwa iblis ana kundi kubwa la wafuasi na anawatuma kila siku kuwafarakanisha wanadamu

عَنْ جَابِرٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ: «إِنَّ إِبْلِيسَ يَضَعُ عَرْشَهُ عَلَى الْمَاءِ ثُمَّ يَبْعَثُ سَرَايَاهُ فَأَدْنَاهُمْ مِنْهُ مَنْزِلَةً أَعْظَمُهُمْ فِتْنَةً. يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ فَعَلْتُ كَذَا وَكَذَا فَيَقُولُ: مَا صَنَعْتَ شَيْئًا. ثُمَّ يَجِيءُ أَحَدُهُمْ فَيَقُولُ: مَا تَرَكْتُهُ حَتَّى فَرَّقْتُ بَيْنَهُ وَبَيْنَ امْرَأَتِهِ، فَيُدْنِيهِ مِنْهُ وَيَقُولُ: نِعْمَ أَنتَ»

Tafsir : Kutoka kwa Jabir, alisema: Mtume Muhammad ﷺ alisema: "Hakika Iblisi huweka kiti chake juu ya maji kisha anatuma vibaraka wake. Yule ambaye anaonekana kuwa karibu naye zaidi ni yule ambaye anafanya maasi zaidi. Mmoja wao huja na kusema: ‘Nimefanya hivi na hivi,’ naye (Iblisi) husema: ‘Hujafanya chochote.’ Kisha mwingine huja na kusema: ‘Sikumuacha mpaka nilipomtenganisha yeye na mkewe,’ naye (Iblisi) humkaribisha karibu naye na kusema: ‘Wewe ni mbora''
Hapo utaona jinsi Iblis anavyowatuma majini kufanya mabaya lakini pia Wanadamu wapo wanaomuabudu huyu Iblis.

SHETANI - Hii ni sifa ya kiumbe muovu katika majini na wanadamu hivyo jinni au mwanadamu akiwa muovu anakuwa shetani ingawaje katika quran kuna aya nyingi zinataja shetani zikimaanisha Iblis hii ni kwa sababu Iblis aliaswi na akahukumiwa moto na lengo lake nikutafuta kundi kubwa katika majini na watu wa kwenda nae motoni hivyo Iblis ni shetani moja kwa moja, Jinni na mwanadamu wanaweza kuwa mashetani kwa vitendo vyao vya kufru. Nawaweza wasiwe mashetani kwa wema wao na uchamungu.
Ndio maana kabla ya kuanza kuosoma Quran tunataka hifadhi kwa Allah kutokana na shatani kwa maana wabaya wote katika watu na majini na Iblis mwenyewe Allah atukinge kwao.

Nitaendelea Inshaalah.
Hapa mimi nina swali kwenye hoja ya kwanza ya Jini.

Kama jini ni kiumbe cha Allah wameumbwa ili wamuabudu Allah, je majini wanatumia kitabu gani?

Je majini ni dini gani?

Je majini wanaswali wapi?

Je kuna ukweli wowote kwamba kuna binadamu wanatengeneza majini na kuyafuga na kuyatuma?

Naomba na Arsis atie neno kwenye haya maswali yangu yanayonitatiza.

Asante.
 
Simba nauliza kwanini bank haziibiwi kishirikina/Chuma ulete wanasema kwamba Bank zinalindwa na majini. Kuibia lazima utumie silaha au kuvunja

Hayo majini yanayolinda bank isiibiwe kishirikina yanamilikiwa na nani? Bank au serikali au bank ya dunia?
Wanaiba sana tu lakini kuna ulinzi wa kwenye bank ambao ni siri kubwa sana, unalinda kuibiwa na watu na majini, lakini watu wana akili sana wanaiba na huo ulinzi upo, wakipata upenyo tu.
Simba.
 
Swali zuri sana, ukweli ni...
Kwa sababu hakuna mtume yeyote aliekuja na Biblia. Hata neno Biblia ni la Kigiriki. Hata ndani ya bilia hakuna neno biblia kwenye aya hata moja ya biblia.
Simba.
Swali: Kitabu Kitukufu cha Imani ya Uislam kilikuja na Mtume gani?
 
alafu huyu Arsis huko post za nyuma alisema biblia ni kitabu cha wagiriki..nyie kama wakristo mnasemaje kuhusu hilo embu mbane Arsis atupe majibu kuhusu biblia ni kitabu cha wagiriki kivp yaan?
Quran ni kitabu kimoja, lakini Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 ndio unapata jina Biblia.

Mtume Muhamad hakuacha vitabu vya sunna hadithi na sila.

Jews kitabu chao kinaitwa Tanakh ni mkusanyiko wa vitabu pia ikiwemo Torati.

Ni simple logic tu.
 
Ma shaa Allah ilm za kila aina zimepamba moto huku.

Ingawa tunachota lakini Simba usichelewe kukimalizia kisa cha Kojani na Comoros.

Unakuwa kama tamthilia za kituruki?
Umenitelekeza kinamna flan hiv, wakat nataka unimwagie elimu yakujitoa Jini likikukumba.
 
arsis vip hik kitabu necrominicon.nan alindika

Screenshot_20240904_171240_AliExpress.jpg
 
Hapa mimi nina swali kwenye hoja ya kwanza ya Jini.

Kama jini ni kiumbe cha Allah wameumbwa ili wamuabudu Allah, je majini wanatumia kitabu gani?

Je majini ni dini gani?

Je majini wanaswali wapi?

Je kuna ukweli wowote kwamba kuna binadamu wanatengeneza majini na kuyafuga na kuyatuma?

Naomba na Arsis atie neno kwenye haya maswali yangu yanayonitatiza.

Asante.
Maswali mazuri sana
Nitakujibu inshaallah
Arsis kuna ombi hapa Arsis atiye neno kwenye maswali ya Dr Matola PhD
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom