Inatokea post namba 114.
Ile kuingia jiji la gharama Dar, ndio nikajuwa kweli macho yamefunguka. Njiani nilikua natafakari sana kilichotokea Chalinze na nini kiliendelea baada ya sisi kuondoka, sijapata jibu la haraka. Nikadhamiria, tukifika nyumbani nimuite Arsis anieleze.
Kufika Kariakoo Dar, ikanijia sauti ya Arsis, ikinieleza "kua makini sana, sasa huku ndio kuna mengi sana utayaeshuhudia, kitu kilichokuponza pale Chalinze ni wale wanga walikua na uwezo wa kuiona pete yako. Kuanzia sasa tunaiwekea pazia, na wewe ukiingia sehemu ukiona watu sio wa kawaida igeuze pete, kwenye hicho kito chake kiwe ndani ya kiganja. Itasaidia, kutotambulika haraka kama una uwezo wa kuwaona. Lakini chunga sana utavyo "behave" ukiona chochote ambacho sio cha kawaida (alisema "behave" hivyo hivyo kwa Kingereza). Nikawa namjibu bila kutoa sauti kua nimeelewa.
Tukaingia Kariakoo, mitaa ya kati kabisa, mtaa wa Tandamti nadhani na Nyamwezi ile, nyuma ya kituo cha polisi ya Msimbazi. Mzee akatushusha, mama akasema nipeleke, tukiwa tayari sisi tutaende na traxi nyumbani. Tukaagana na mzee na Sister wangu wao wakaendelea na safari, mimi na mama tukashuka. Ile tunatembea njiani nikaanza kuona maajabu.
Nikaanza kuona watu wapo uchi kabisa, nikaanza kuona viumbe vya kiajabu ajabu, ambavyo sio binadam kabisa, lakini nikajua hata mama yangu havioni, kwani tulipishana navyo vyenyewe ndio vinatukweppa sisis alakini sisi tukawa tunatembe kama hakuna kitu, Kidogo nianz kuwakwepa lakini sauti ikanijia ikanambaia usiwakwepoe, huwei kugongana nao hao. Ukiwakwepa wataju unawaona wataanisha ugomvi.
Muhimu ilikua ni maajabu tu kwangu, mama akaingia maduka anayoyuataka pale mtaa wa lsikukuu na Tandamyti, kuna maduka makiubwa mawili matatu ya vyakula, alienda kununua avitakavyo mimi nikamwambia nakungija kwa pembeni hapa. Basi niloyashuhudia, kama mtu una roho ndogo unaweza ukatoka mbio. Kuna wateja waliokuja pale sio binadam kabisa na wao walikua wanaagiza vitu, lakini nina uhakika waliokua wanwahudumia na wateja wengine waliwaona kama binadam, mimi nilikua pete yangu nimeigeuza na kiganja nimekifunga isionekane kabisa.
Mama alipomaliza pale, tukaenda mbele kidogo kuna maduka ya vufungashio, mwenye mama alikua na biasshra zake na kina mama wengine. Akanunua anavyovitaka, tukaenda kiyuo cha taxi hapo hapo karibu tu, mwenye duka la vifungashiuo anaonesha anafahamiana sana na mama, akamwabia usijali mama vitakufata vitu vyako mpaka nyumbani, ukichelewa utavikuta vimeshafika. Huyo kijana ndio yule simba wako? Mama akamwabia umemsahau, jamaa wa dukani akasema amkua sasa anatisha, ulikua ukija ne hapa bado kabisa. Alikua wapi siku nyingi sijamuona? Mama akasema yupo, si unajua wakikua hawa hawataki kutoka na mama zao. Yule jamama akasema "wajinga hawa, hawajui maana ya soko na biashra". Mama akacheka, aksema huyo mtu wa spana na baba yake, yeye garo lako likiwa na shida mtafute. Jamaa akasema, tena itakua vizuri, mana mafundi wasumbufu sana. Mama akamwabia yupo na baba'ke gereji, babake anamsisitiz hataki mteja wake apewe usumbufu. Jamaa wa dukani, tutembelee simba, nipe zako, gari likikorofisha nikupigie. Nikampa namba tukaondoka zetu.
Tukapanda taci akamwambia mwenye taxi, nipitishe kw Issa hapo nichukue vitu vyangu. Huyu Issa ni maariufu sana duka lake la vyakula pale Kariakoo, ndipo nilipoona wateja wengine sio binaadam wanenda kununua vitu. Ka ufupi Kariakoo nzima ilijaa mambo ya ajabu ajabu, kuna watu wako uchi, kuna watu unawaona vilema kumbe sio watu. Kuna watu huoni kabisa sura zao, Kuna watu wamebeba watu wengine kama wanawatembeza lakini wengine hawawaoni. Yaani pale ni vurugu tupu, Kuna watu niwashuhudia wapo nje madukani, wakiwa uchi kabisa na wamekaa juu ya viti, tena maduka mengi tu. Nikaona watu wanauza bidhaa mtaani uchi kabisa. Kama wale kina mama wa Chalinze, tena wanawake kwa wanaume. Nikaona wanawake wanauza bidhaa uchi lakini ukiwatazama viuri unaona ni kama wanaume aliovaa kimjini wanafanya biashara. Mjjini wansema ni vurugi mechi.
Tulipoondoika kuelekea Ilala ndio nikaufaidi mtaa wa uhuru, kuanzia ile raundi abauti ya Uhuru mpaka tunaelekea Ilala ni vituko vitupu, watu wapo uchi kwa makundi, kuna watu wamekaa pale raundi abauti uchi wa nyama, hawana hata habari ya dunia, wenye juruka, wenye kutua. Niliona kitu kimoja cha ajabu mpaka nikata kustuka, ndani ya taxi. Niliona kuna watu wawili warefu wamevaa nguo sio za kaiwa kama sare fulani, lakini walikua wanatembea kiukakamavu huku wanakagua kila kitu wanachokiona, wakatazama sana taxi tulioipanda nikaona kama wamnesemezana kitu wakawa wanaifata taxi kama wameona kitu kisicho cha kawaida, pale pale ikaja sauiti ya Arsis ikanambia, usiogope hawawezi kuwafikia kabisa, wataishia kuwatazama tu. Nitakueleza zaidi kuuus hao unaowana baadae. Basi taxi yetu kila inapokwenda na wao wako pembeni wanatembea nyuma yake lakini hawaifikii, mwisho wake wakageuza wakarudi walipotoka, kama wamaumua hawawezi kuifikia.
Tukafika nyumbaniu salama salmini, mimi nikiwa hoi kwa mawazo. Nikaingia chumbani kwangu moja kwa moja, sikungoja kitu nikaingia kukoga, nikaslai. Ndio nikatoka nje nikachukua nanasi moja kubwa nikalimenya nikawa nalila peke yangu, likiua tamu kweli. Nikasema leo sili kitu, hili hili linatosha kabisa, nilipomaliza nikanawa nikaingia chumbani kujipumzisha kidigi nilikua nimechika zaidi kiakili kuliko kimwili.
Itaendelea.