"theology"
Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 8.
Inatokea post namba 2358.
Sheha; wachawi wenzenu wengine wa hapa mtaani ni kina nani?
Afisa; Hio ni siri ambayo hatuwezi kuisema hadi kifo. Mmeshatushika sisi na wote waliohusika na hii kazi, ambao hawajahusika hata kanuni za kikawaida zinakatzaa kuhusishwa.
Bakora: Mimi namuunga mkono kwa hilo. Tuendelee na mengine.
Sheha; Tueleze waliohusika.
Afisa; Wameshikwa wote na sikjii kama wapo hai mpaka sasa, maana hukumu ya hili ni kifo tu, haina mjadala kichawi. Hata chama chetu tukikamata waliongilia himaya yetu bila kukubaliana kabla tukiwakamata ni kifo tu. Labda tusiwakamate.
Bakora; Huyu analeta mambi ya kichawi ili apoteze muda. Mimi nashauri kwa kua ewotw wamekiri wahukumiwe.
Sheha, wapelekwe mahakamani?
Bakora; ndio, hilo moja na sisi tutapitisha hukumu yeytu kwanza na nyinyi, hususan wewe, upo hapa Kiserikali huo utakua uamuzi wako. Sisi hukumu yetu, hatuwezi kuisema hapa mbele za watu, tunajua tuwajulisha vipi, hatutaki kesi.
Sheha; Nimeelewa. Mimi wacha nipige simu polisi, mkubwa wa kitiuo cha hapa jirani namfahamu.
Bakora: hautompata huyo leo, wala kesho. Labda umpigie msaidizi wake.
Sheha, aah kasafiri?
Bakora; Ndio.
Sheha, wewe ngeni Sheikh, unajuaje?
Sheha: Mimi tunafahamiana nae, najua kua kasafiri alfajiri ya leo. Uliza hata ofisini kwao waytakueleza.
Sheha; Sasa tunafanyaje?
Bakora; Wazo la kuwashitaki hawa ni zuri, ushahoidi woite upo na wao lazima watakiri hawatoisumbua mahakama, kwa kua binti yupo hai, sijui hukumu yao itakuaje kiserikali.
Sheha: Wacha nipige simu hapo nje,. jamani akam kuna hawa leteni ytunywe. Haya si mabo madogo, maana naanza vbipi kuwael;eza polisi?
Bakora: Waeleze ukweli kama ulivyouona na kuusikia kuanzia alfajiri. Watuhumiwa si hawa hapa mnao?
DSheha; Sawa wacxha niende nje nikapige simu.
Kijana: Na mimi wacha niende nje, kweli kama kuna kahawa uje jamani.
Kuna wanawake wakainuka, waksema kule ipo nyingi wacha tukalete na vikombe.
Mimi, Kijana, Balora tukatoka nje. na wengine wote wakatufata kasoro watuhumiwa tu. EWakabaki wamekaa, kama wamepigiliwa misumari.
Kutoka nje mimi na kija n na Bakora yukaenda kukaa pembeni, tukawacha pale Waunguja na Sheha wao.
Bakra: sasa hapa kaszi imeisha, hawa sisi tutatimiza hukumu kama ya wale, hawatiweza kufanya kazi kabisa, lak9ini cha kwanza inatakiwa mali za yule bwana lazima huyu binti na mamake walipwe kwa machungu waliopitia. Na huyu mumewe, ndio hana chake tena. Mtito yule asafiroshwe kabisa asibaki Unguja, maana hii hadithi tayari ipo mitaani saa hizi inazagaa kama moto wa makumbi.
Kahaw aikaja tukanywa pale.
Sheha; Polisi wanakuja kikosi cha maana.
Bakora twendeni ndani tukamalize sisi tuna safari jamani, hapalkaliki.
Tukaingia ndani wote, mimi nikaitwa ndani na kina mama huko, nikakuta kumbe mipango yao ya kumsafirish binti kwenda bara ytayari lakini hakuna alieambiwa, na ataondoka na mama yeke mdogo, kimyakimya. Nikaone heri. Ikaja sauti ya Arsis kichwani ikinambia, usiwe na wasiwasi, yupo chini ya ulinzi wetytu, wewe uytawaona Datr hao. Nyyie mnawsza kusafiri wakija polisi anagalia msisema lenu mkafanywa mashahidi, itakua ngumu kwenu nenda rudi. Nikamuelewa.
Ile tunatusi ndani hatujjakaa polisi wamegonga nje, akatoka Sheha akaanza kuomngea nao, nje, na sisi tukaaga,m hakauna aliesema chochote. Tukatoka mimi, Bakora na kijana, mama ndani huko washasuka kuondoka na binti na mamake mdohgo. Tukaondoka.
WWale mbwa wawili wakachukuliwa wakapelkwa polisi, wakaelezea kama walivyoelezea, wkawekawa ndani bila dhamana, mahakamni siku ilipofika kwa kua wanakiri makosa, wakahukumiwa jela. Walipokua jela ndio hukumu ya majini walioifanya hio kazi ikapitishwa.
Tutaendelea na kionjo kingine tutaporusi, hiki cha Unguja tukimalizie hapa.
Simba.
Itaendelea
Simba