Ifike mahali viongozi wa hii timu watambue kwamba kuna wachezaji wengi sana ambao hawastahili hata kukaa benchi achilia mbali kuvaa jezi ya United....

Mchezaji kama hujilund sijui hujilimdu anafanya Nini pale united?

Eti winga kama Anthony ndio unategemea akupe matokeo kwenye game kubwa si utani huu.. Mchezaji kama Anthony ni wakuingia dk ya 88 wakati timu ikiwa inaongoza, kwanza timu serious huyu angekuwa anacheza mechi za EFL tu basi
 
United imebakia jina tu na status, timu hakuna anayeiogopa, sasa hivi timu yoyote kwenye zile top six(totenham,Arsenal,Man city na Liverpool) ikipata hata matokeo ya sare tu dhidi united inajiona kama imepoteza mechi... Kudroo dhidi united is regarded as failure, yaani mashabiki wa timu zingine tunaona ni Bora timu yetu itoke dro na timu kama Aston villa au new castle lakini sio united.

Kuna muda Huwa naiangalia hii timu yenu kisha nakumbuka hivi hii timu ndio ilikuwa inatusumbua kipindi kile cha SAF mpaka kila mtu akawa anaichukia...?? Naishia kusikitika tu

Binafsi siku hizi nimejikuta nawaonea huruma na wakati zamani united ndio timu niliyokuwa naichukia sana hapa chini ya jua.
 
Kumtoa Fred na Kisha kumleta Amrabat ni sawa na kuuza rungu Kisha kununua manati halafu utegemee eti utakuwa sawa na mtu anayemiliki bunduki(Rodri, Rice,Caicedo,Szibol etc)
 
Sheffield United inayotumia uwanja wa OLD TRAFFORD
Sijajua board wanaangalia mpira gani.... so far tumekuwa ovyo kweli.... Timu yetu wachezaji hawasurvive sababu ya mfumo mbovu wa uchezaji....ila badala tukomae kujenga structure nzuri tunazidi kudidimia
Muda mrefu hujaonekana, natumai waendelea vyema kiafya na kifikra.

Yes nipo,
bado sijapata starehe ya kuniweka mbali na manchester united.

Japokuwa naumia nafsini kwa jinsi tunavyocheza mechi zetu dhidi ya timu pinzani ila sina budi kuifuatilia hii timu.

Ujinga huu ninaoushuhudia nakumbuka walikuwa wanafanyiwa ARSENAL miaka minne iliopita, now liverpool na man city wote wanakhofu wanapocheza na THE GUNNERS.

Football heritage
Nipo na afya njema Mwenyezi Mungu anasaidia....ni majukumu tu yanabana....pia toka bwana Jassim afeli na bid yake nikaona nioujguze speed na hii timu.

Yes Arsenal wameimprove sana sababu ya watu sahihi pale juu hasa Edu (alishinda best football director mwaka huu nafikiri October kama sijakosea)

Naimani tukipata director sahihi na technical director sahihi tunaweza fika sehemu.
 
Manyumbu hatuwapendi ila asanteni sana kwa kazi nzuri mliyofanya.

Tunawaombea muingie top four. UEFA bila nyumbu is boring!

Ila hii mentality ya kushangilia droo sio nzuri kwa timu kubwa kama nyumbu!
 
Manyumbu hatuwapendi ila asanteni sana kwa kazi nzuri mliyofanya.

Tunawaombea muingie top four. UEFA bila nyumbu is boring!

Ila hii mentality ya kushangilia droo sio nzuri kwa timu kubwa kama nyumbu!
Mimi naamini Man U ni timu kubwa lakini si Man U ya sasa,mimi ni shabiki wa Man U lakini kwa game ya jana dhidi ya Liver aliye kwenye ubora tena nyumbani kwake ikiwa tumetoka kufungwa na Bournemouth 3-0 tena OT jana nlitegemea tungefungwa tu. Si sawa kushangilia draw ila kwa mimi kwa matokeo ya jana nmeridhika kabisa
 
Back
Top Bottom