Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hua napenda kuangalia convo za watu kabla ya mechi, wakati wa mechi na baada ya mechi.

Unamshuhudia mtu anajisifia na kuponda kila kitu. Anaandika Arsenal hawana timu ya kutufunga, mechi yetu na wao sisi tunaenda kufanya mazoezi.

Baada ya kupata goli unamuona akiapia kwamba ushindi ni uhakika hawezi kumpinga kocha.

Goli linarudishwa unamuona anaandika sisi tukipata goli tunajisahau.

Linapigwa goli la pili unaona anasema Weghorst hafai na pengo la Casemiro lipo wazi (Juzi Erik alisema walishinda bila Casemiro na yeye akashangilia hii declaration)

Wanarudisha goli unaona anaandika hili ni bonge la header hawa Arsenal bado wetu tu.

Dk 10 mbele anaandika hii mechi bora iishe Arsenal inatusaka mno.

Wanapigwa la 3 anaanza kumtukana kocha na kila mchezaji.

In a span of two hours unamshuhudia mtu uwezo wa akili yake ukiwa tested, unamuona akiwa desperate, akiwa vulnerable, akiwa anasubiri miujiza yaani anajiexpose kila kitu.

Kuna mshkaji wangu tulikua tunabishana juzi akatoa kashfa, Rashford alivyoscore akaweka status. Baada ya game akafuta status akaandika kwamba kwa United hii ndiyo mechi yao ngumu kabisa kwakua Arsenal is a better side so tusijisifie kwakua wao ni wabovu.

Na hapo shida ni nini? Shida ni kwamba hawatumii akili.

Hamna kingine.
🤣🤣🤣🤣
 
Jinsi tulivyoumia leo kwangu ni ishara Ten Hag anafanya kazi kubwa sana. Nikikumbuka miezi 6 tulipokuwa na hapa tulipo. Nani angeweza kufikiri hata tukifungwa mechi 3 mfululizo bado tupo top 4?

Binafsi I'm very grateful so far, Arsenal, City na L'pool hizi ni timu ambazo benchi la ufundi lipo kwa zaidi ya misimu mitatu. Hatuwezi kujilinganisha nao kwa sasa, benchi letu la ufundi ndio kwanza wana miezi 6 tu.

Naona mwanga ndani ya msimu ujao. Msimu huu top 4 na kikombe kimoja yatakuwa mafaniko makubwa sana na mahala tulipotoka msimu mmoja nyuma. Japokuwa nilianza kujipa moyo wa kufanya kitu ila Arsenal wapo serious msimu huu.
Maisha yanaenda kasi sana yaani leo hii aseno tunagawana nae point za home and away
 
👏👏👏 pongezi kwenu ManUtd inaonekana tulitegemea ushindani mkubwa na hamkutuangusha mkaleta ushindani kweli kweli. Mnazidi kuimprove. Mtakuwa tishio Kwa bottom teams huko na Hawa top teams wasipokaa chonjo watauwawa sana nanyi (eg Citeh). Ila kwetu nyie Bado mabwana wadogo sana
 
Tukishashinda mechi ya arsenal baada ya hapo natabiri mechi zote 17 zilizobakia ni win win
.
d1255055620f0e6a.jpg
 
Our main target ni 6 points from Asernal.Weekend hii tunaendeleza tulipoishia kwaiyo tutawapiga 3+ goal kama ngoma na kuchukua 3 points kwasababu 3 muhimu tulizonazo:
1. Uwezo ( Timu imeimarika na inastahili)
2. Nia (Kuirejesha heshima ya club iliyopotea)
3. Sababu (Kuchukua ubingwa msimu huu)
Tulisema tutarudi hapa
 
pongezi kwenu ManUtd inaonekana tulitegemea ushindani mkubwa na hamkutuangusha mkaleta ushindani kweli kweli. Mnazidi kuimprove. Mtakuwa tishio Kwa bottom teams huko na Hawa top teams wasipokaa chonjo watauwawa sana nanyi (eg Citeh). Ila kwetu nyie Bado mabwana wadogo sana
Mkuu naona akili zako umeamua kutozitumia unasema sisi mabwana wadogo kwenu kwani game ya kwanza ilitokaje.

Ushindi wa jana wa arsenal unajua umetokana na nyie kupoteza game ya kwanza dhidi yetu ilikuwa ni lazima mpambane tu ni mara chache timu kubwa zinapokutana mmoja aondoke na point zote 6.

Sisi tunachojua tuliwachapa kwetu mmetuchapa kwenu sioni cha ajabu hapo mna point zetu 3 tuna point zenu 3 mnajimwambafai hapa utadhani game zote mlitufunga.
 
Back
Top Bottom