Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nimeangalia gemu ya jana hakika manchester united wana kocha wachezaji wanacheza kiume lisandro top top top

Casemiro hana mjadala kaacha pengo kubwa yote kwa yote mabadiliko ni makubwa sana ndani ya miezi 6 si jambo jepesi kocha mpya kutoboa ndani ya top 4 halafu ratiba yanyewe imemkalia vibaya wanapumzika siku 3 tu wanakutana na mech halafu wanatoa upinzani wa kutosha

Kwa upande wa liverpool na chelsea majeruhi wao wakipona ligi itakuwa nzito sana

Spurs conte alishasema wana project mpya ndio maana wamepooza ila sio wa mdebwedo.

Newcastle hawa wanatoa upinzani haswaa top 4 bado ngumu.

Wee ni mtu wa mpira wa kibisa respect
 
Tulijitahidi sana sema tuna makosa madogo madogo hasa tunapofanya sub.
Mosi viungo wetu tukianza na Eriksen umri umeanza kumkamata yupo slow sana na mara nyingi anapokonywa mipira kirahisi.
Game ya kwanza Arsenal walifunga goal likakataliwa,ni huyu huyu Eriksen alipokonywa mpira kijinga.

McTommy ana miaka 26 sasa,ni wakati mzuri wa kumuuza mapema fedha yake atafutwe kiungo mzuri.

Shaka alimpeleka sana Shaw,sijui kwanini Kocha akutafuta solution mapema !.

Bado nina imani na kocha katutoa mbali sana na tukitilia maanani ana muda mfupi sana EPL.Nina hakika kadri siku zinavyosonga kuna mambo mengi atayafanyia kazi ikiwemo mshumbuliaji wa kati na kuongeza viungo mahiri na vijana.

Wakati umefika wachezaji wafuatao waondoke mara moja.
1. Harry Maguire
2. Phil Jones
3. Anthony Martial
4. Anthony Elanga
5. Donny Van de Beek

ETG aachwe atengeneze Project yake ndo kwanza ana miezi 6 lkn stil yupo top 4.
Arteta ameshatengeneza ya kwako ndo maana Arsenane wapo on fire......
 
Wee ni mtu wa mpira wa kibisa respect

City kacheza na spurs na wolves nimeona wamebadilika mkuu na wao walipoteana wingi wa mech ni msala kuna muda naikumbuka chelsea ya conte 2017 walikuwa wakicheza kila mwisho wa wiki hawana mashindano mengine walikuwa wanatoa kichapo haswaa walipoingia kwenye mashindano maane walipoteana
 
dedaab10-318d-4069-a43b-65882cec53df.jpg
 
Ilitoa ahuweni kwa beki zetu, kuna muda zinchenko hakuwa huru kucheza, sababu ya Anthony, alipokuja mtoa, zinny akawa huru, akawa anasogea kwenye kiungo ndio ule msako ukafanyanyika.
Yale Yale ya Argentina kumtoa Dimaria sku ya final FIFA, washukru kulikuwa na sub ya dybala , somehow same to Dimaria
 
Anthony huwa Ni kiazi, kitendo Cha kumtoa mliturahisishia kazi Sana

Nilikaa na mashabiki wa man u ,nikagundua hawajui mpira ,walikuwa wanataka Anthony atoke,

Nikawaambia Anthony Ni mzinguaji ila leo anafanya Magalhaes na zinny wasipande ovyo ,

Alipotoka walinielewa
 
Pamoja na yote lakini hatuna machaguo mengi kwenye eneo la ushambuliaji.
Ukiliangalia bench baada ya timu kukamatwa unashindwa umnyanyue nani akabadilishe mchezo.

Kuna wakati nawaza kama ile yellow kadi ya Casemiro kama ilikuwa ya kujitakia vile,Zaha hakuwa na impact kubwa kwa eneo alilokuwepo hadi jamaa amrukie vile.

Hata hivyo tumejitahidi sana kwa hawa Arsenal waliochachuka mbaya msimu huu.
GGMU
 
Kuna siku nilielezea kwenye uzi wenu kwanini tuliwafunga japokuwa mlituzidi kiuchezaji.

MBINU, MBINU, MBINU. Ile mechi hatukushinda kibahati tu na pale tulikuwa vibaya tukacheza counter attack football. Sasa hivi tunapiga kotekote maana defensively tume-improve na pasi pia tunaziweza, kwenye timu zilizotengeneza nafasi nyingi msimu huu tupo. Emirates ni uwanja tu.
Total dominance,no janja janja
IMG-20230123-WA0020.jpg
 
Arsenal ya kawaida sana na jana defense yenu imekuwa exposed na Brighton.

Brighton ndiyo timu pekee ukiacha United imeonyesha udhaifu wenu ni vile tu na wao walikuwa na makosa mengi ya kiulinzi na udakaji.
Kwakweli Arsenal ya kawaida Sana

Manchester United stats in details: Arsenal had 63 touches in the United box!! 63!!

That’s the highest total in any Premier League game this season. United only had 12 in Arsenal’s box.

Arsenal’s 3.2xG (off 25 shots) is their highest this season.
IMG_20230123_190207.jpg
 
Kwakweli Arsenal ya kawaida Sana

Manchester United stats in details: Arsenal had 63 touches in the United box!! 63!!

That’s the highest total in any Premier League game this season. United only had 12 in Arsenal’s box.

Arsenal’s 3.2xG (off 25 shots) is their highest this season.View attachment 2493118
Hongereni arsenal kwa kuchukua ubingwa wa kumfunga man u
 
Umeanza kufuatilia mechi za Man U vs Arsenal lini?

Kama una uzoefu hiyo kauli usingeitoa.
Fuatilia toka enzi za Fergi na Wenger, Arsenal ndio mnadominate mpira kwa maana ya ball possession.
Ila matokeo huwa yanakuwa tofauti.

Fuatilia. Utajifunza kitu.
Kipind Cha Unai emery ,Arsenal haikuwa ina dominate mechi
 
Back
Top Bottom