Hua napenda kuangalia convo za watu kabla ya mechi, wakati wa mechi na baada ya mechi.
Unamshuhudia mtu anajisifia na kuponda kila kitu. Anaandika Arsenal hawana timu ya kutufunga, mechi yetu na wao sisi tunaenda kufanya mazoezi.
Baada ya kupata goli unamuona akiapia kwamba ushindi ni uhakika hawezi kumpinga kocha.
Goli linarudishwa unamuona anaandika sisi tukipata goli tunajisahau.
Linapigwa goli la pili unaona anasema Weghorst hafai na pengo la Casemiro lipo wazi (Juzi Erik alisema walishinda bila Casemiro na yeye akashangilia hii declaration)
Wanarudisha goli unaona anaandika hili ni bonge la header hawa Arsenal bado wetu tu.
Dk 10 mbele anaandika hii mechi bora iishe Arsenal inatusaka mno.
Wanapigwa la 3 anaanza kumtukana kocha na kila mchezaji.
In a span of two hours unamshuhudia mtu uwezo wa akili yake ukiwa tested, unamuona akiwa desperate, akiwa vulnerable, akiwa anasubiri miujiza yaani anajiexpose kila kitu.
Kuna mshkaji wangu tulikua tunabishana juzi akatoa kashfa, Rashford alivyoscore akaweka status. Baada ya game akafuta status akaandika kwamba kwa United hii ndiyo mechi yao ngumu kabisa kwakua Arsenal is a better side so tusijisifie kwakua wao ni wabovu.
Na hapo shida ni nini? Shida ni kwamba hawatumii akili.
Hamna kingine.