Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
..raia,sijui kama we ni mwema kweli,ila,karibu!

..hili baraza ni pana sana na lina kila aina ya watu,wenye kila aina ya msimamo na wengine hawana kabisaa!

..nadhani kitu cha muhimu si kuwa katika upande gani wa kisiasa,bali,ni uwezo wa kutoa mawazo ya nini kifanyike ili nchi yetu iweze songa mbele vizuri na kwa manufaa ya wengi!

..kuna kipindi issues zilikuwa zinakatwa hapa mpaka ilitia msisimko!hali si hivyo kwasasa!kwani majungu yamezidi!focus imepotea...unajikuta unaongea au kuchangia pumba!

..kama nilivyosema awali,hili ni baraza na baraza ni watu!sasa,kwenye wengi kuna mengi na ndio haya!ila,naamini ipo siku tutarudi kwenye kukata issues baada ya huu upepo mbaya wenye pepo baya utakapopita!

..wapo watu kama fd,dua,mjj,mkandala,philemon mikael,kithuku,jokakuu,masatu,invicible,kada,mwafrika wa kike,samvulachole,mtupori,fmes,drwho,mtumwitu,na wengine ambao nadhani wamebadilisha majina. hawa walikuwa wanakata ishu si mchezo...ila siku hizi....aagh!tuache huu upepo upite!

..kuwa na subra,hii ndio tanzania!
Sana mkuu tupo pamoja. Sema tu kuna baadhi yetu hubadili mwelekeo wa mada wakishaona wanazidiwa hoja, ndio maana raia mwema anashangaa. Tatizo sasa kijiwe kinabadilika nakuwa cha mipasho na udaku. Mtupori kawa Idimi, kabadili jina. Sababu ni kuwa kuna mtu anajiita 'Mtu pori'. Nikamwachia jina, sitaki makuu.
Mi naendelea kusubiri nyeti toka ndani ya Kizota Dodoma.
 
mtandao wasirudi mchezo ..hiyo kamati ya uchaguzi ikiongozwa na samuel sitta,rostam aziz ,maua daftari,batilda burian saha...unategemeani kwenye kundi la watu 20??
 
Akina Lunyungu na wengine mliopo Kizota, watu hatulali tunasubiri kwa bashasha matokeo, hala hala jamani!
 
Habari kutoka kizota - dodoma. Wagombea NEC CCM viti 20 tanzania bara waaanza kujidani.
 
natania tu mzee, akianguka Lowassa basi CCM imekwisha. ila wataanguka vigogo kwa sababu nafasi 20 tu kuna watu ambao nadhani watapita tu Lowassa ni mmoja wao.
 
Leo JK kadhihirisha kwamba hakuna Dr.Nchimbi ila ndugu Nchimbi na wengine wote wenye real PhD waliitwa Dr.so and so . Patamu hapo.Lunyungu kuna habari gani huko ? Mzee kaachia for real ama bado tu ?

Ukisoma Mwananchi ya juzi ndugu Mtanzania utakuta habari ya Malecela kupotea ukumbini baada ya jina Msekwa kuletwa hadharani.
 
Mkuu Malecela, aliingia kwenye kikao akiwa amefuatana na mtoto wake wa kike anayeitwa DR. Mwele Malecela, na walizni wake wawili, na mkewe ambaye naye anatafuta ujumbe wa NEC,

Wamekuwa wakihudhuria hivyo vikao toka mwanzo hadi mwisho, hizi habari za Mwananchi, unless kama wewe ni mwandishi wao, kama una beef naye anakuja huko majuu, mwisho wa next week atakuwa London, baadaye New York na DC vipi ukikutana naye ukamtolea machungu yako mkuu badala ya kuendelea kutoa sumu humu ambazo hazina kichwa wala miguuu,

Hivi huoni kuwa hata wananchi siku hizi wamekushitukia na Malecela wako kuwa lazima una something personal, lakini unaweza kusema kuna tunaomfahamu tunaweza kukusaidia mkuu!
 
Wakati tunasubiri matokeo tujiweke busy kidogo kuchanganua hili na lile masaa yapite, au mwaonaje.

kwa mwendo huu, uchaguzi utamalizika sio chini ya saa sita usiku. tunawaamini ndugu zetu mliopo hapo kizota kutupatia taarifa za maendeleo huko.

Katika vile viti 20 vya bara, kama tulivyokwisha one, kuna wagombea ambao wana kura za itifaki na ni lazima wapite kwa kura nyingi sana. there is no doubt kwamba Kinana, makamba, mwambi, komba na Lowassa watakuwa ni top five, na watapata kura sio chini ya 1,000 kila mmoja.

Kwa mtazamo wangu, mMtandao unaweza kupata watu wake wengi tu kwenye NEC. Hii inatokana na ukweli kwamba kila katika pita pita zao au za wapambe wao huko mikoani, pia walikuwa wanapeleka pia majina ya nani apigiwe kura na nani asipigiwe. Wenyeviti na makatibu wa CCM wamekuwa wanapewa instructions mbali mbali on how to act wakija dodoma. Hii imekuwa inafanywa very scientifically na kwa siri ya hali ya juu. Just as Kikwete na Lowassa walipopiga na butwaa NEC ya mwaka 2002 kwa kupata kura kidogo, same thing in a differet game kinatokea wakati huu. Tusisahau kwamba huko mikoani kuna wajumbe wa makambi ya Sumaye, JK/Lowassa, Salim, Malecela, na Mwandosya. Na kila kambi itajaribu kupiga kura upande wake huku iki minimize kura za kambi nyingine. Kelele za Kikwete kuhusu rushwa ni upuuzi tu kwani wagombea wote wale wenye majini makubwa wamesambaza wapambe na magari mengi na mipesa huko mikoani na wamepewa siri ya jinsi gani TAKURU wana-operate. Ndio maana TAKURU haishiki watoa rushwa wa majina makubwa.

Piga, ua, Mtazamo wangu wa matokeo ya NEC 20 bara ni hawa:

Profesa Idris Mtulia, Andrew Chenge, Edward Lowassa, Abdulrahman Kinana, Juma Kapuya, John Komba, Yusuf Makamba, Benard Membe, Kingunge Ngombale- Mwiru,John Chiligati, Hassan Ngwilizi, Emmanuel Mwambulukutu, Aggrey Mwanri,Stephen Wassira, Christopher Mwita Gachuma, Enock Chambier, Frederick Sumaye, William Lukuvi, Jaka Mwambi, na James Msekela.

Tutegemee kusikia malalamiko mengi sana kutoka kwa wale walioshindwa. Na kikwete kusema kwamba eti mtoa rushwa hatasamehewa amejifunga kitanzi sababu atatakiwa kuingilia kati uchaguzi huu. CCM kwa kweli ipo hatarini sana. Wamalize huu upuuzi wao na turudi kwenye mambo ya maana kwa maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania.

Lakini danganya toto ya kuunda kamati maalum ya madini yenye upinzani, wasomi na wataalam hapo nampa heko JK kwani kina Zitto, Slaa.. wasipokuwa makini, ndio atakuwa amewapiku. Pia kamati hii italishwa vizuri na mambo yatakuwa kimya over time huku rasilimali zeti zikiondoka kwa mwendo ule ule. Dawa hapa ni upinzani kukataa upumbavu wa kamati za kienyeji Tanzania ambazo tumeshachoka nazo.
 
Lakini danganya toto ya kuunda kamati maalum ya madini yenye upinzani, wasomi na wataalam hapo nampa heko JK kwani kina Zitto, Slaa.. wasipokuwa makini, ndio atakuwa amewapiku. Pia kamati hii italishwa vizuri na mambo yatakuwa kimya over time huku rasilimali zeti zikiondoka kwa mwendo ule ule. Dawa hapa ni upinzani kukataa upumbavu wa kamati za kienyeji Tanzania ambazo tumeshachoka nazo.

Hawezi kuwapiku kwa kuunda kamati ambayo inaweza kabisa kuwa haina uwezo wowote wa kuleta mabadiliko ya kweli yenye kuwanufaisha Watanzania. Pia madudu ni mengi mno kiasi mbacho inabidi afanye kweli na wananchi waone hivyo hasa katika kupambana na ufisadi, rushwa za vingunge, viongozi wanaojilimbikizia mali kwa kutumia nyadhifa zao na matumizi mabaya ndani ya chama na siri kali.
 
Lowassa kuanguka?

Mwanakijiji,

Si tumesoma hapa kwamba CCM wamebadilisha katiba ili waziri mkuu na waziri kiongozi wawe wajumbe wa NEC na CC, kwahiyo Lowassa wala hata hahitaji kugombea, huenda jina lake likaondolewa kwenye
hilo kapu la wajumbe 20.
 
Leo JK kadhihirisha kwamba hakuna Dr.Nchimbi ila ndugu Nchimbi na wengine wote wenye real PhD waliitwa Dr.so and so . Patamu hapo.Lunyungu kuna habari gani huko ? Mzee kaachia for real ama bado tu ?

Ukisoma Mwananchi ya juzi ndugu Mtanzania utakuta habari ya Malecela kupotea ukumbini baada ya jina Msekwa kuletwa hadharani.

Murangira,

Nilisoma gazeti la Mwananchi. Walichoeleza ni kwamba walimtafuta mzee Malecela baada ya kikao ili aelezee kilichotokea kuhus yeye
kuacha kuwa Maikamu wa Mwenyekiti lakini hawakumpata Malecela.

Sasa je hiyo ina maana Malecela alikimbia kikao? watu wangapi kila siku wanatafutwa na waandishi wa habari na hawapatikani?

Naona kwenye hili humtendei haki mzee Malecela.
 
Naona wazee wa mabreaking news wameshindwa kuleta mavituz, ngoja tukalale sasa, tutasoma kesho.
 
Naona wazee wa mabreaking news wameshindwa kuleta mavituz, ngoja tukalale sasa, tutasoma kesho.

Mzee mbona mapema? Wengine tutasubiri tu mpaka tusikie vilio vya waliobwagwa na nderemo za walioshinda.

News za kuzisubir muda mrefu huwa tamu zaidi kwi kwi kwi!!!!
 
Back
Top Bottom