Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
Taarifa sahihi ni kuwa wa break wanarudi muda mfupi ujao kuchagua wajumbe wa NEC viti 20 (kundi la kifo) sasa hizo habari za katibu mkuu mpya ni mazingaombwe tu...

hilo kundi la watu 20 hapo ndio watu watakapochoka na hao watakaotajwa ! subirini mtasikia mtandao umerudi ??
 
Masatu,
Hizi habari za Makamba nje sio sahihi. Katibu mkuu anapendezwa na Mwenyekiti na CC inamthibitisha. Kikao cha leo ni cha Mkutano mkuu ambao unachagua wajumbe wa NEC.
Are U sure?... ama ndio katika kutufunga kamba sisi tusojua/ona yanayojiri CCM Dodoma.
 
kada stay tuned,HIVI RUSHWA ITAISHA LINI?
 
Kwa nini mhangaike hivi wakati habari zote tutazipata tu kupitia vyombo halali, au Invisible anawalipa kwa kuleta mabreaking news?

..una ugomvi naye?

..si wengine tunapenda hizo breking newz!

..wengine hivyo vyombo halali walipo havipo!

..sasa hii ya kulipwa inatoka wapi?
 
Masatu,

Uko right, habari ya katibu mkuu haiwezi kupatikana leo.

Katibu wa CCM anachaguliwa kwenye NEC mpya, yaani baada ya NEC kuchaguliwa, watakaa na ndio watamchagua katibu mkuu baada ya kupendekezwa na JK.

Sasa hata NEC haijaundwa, tayari waganga wa mvua wanasema Makamba kaondolewa?

Labda kama huo ni utabiri lakini sio habari ya kweli.
 
Masatu,

Uko right, habari ya katibu mkuu haiwezi kupatikana leo.

Katibu wa CCM anachaguliwa kwenye NEC mpya, yaani baada ya NEC kuchaguliwa, watakaa na ndio watamchagua katibu mkuu baada ya kupendekezwa na JK.

Sasa hata NEC haijaundwa, tayari waganga wa mvua wanasema Makamba kaondolewa?

Labda kama huo ni utabiri lakini sio habari ya kweli.

Sema wewe kiazi... nikisema mimi mhogo mchungu! hao waganga wa mvua wapo wengi sana hapa...
 
benmwinyikl4.jpg



You know Them.


msekwace4.jpg



Msekwa



zuma1ie4.jpg


JK na Jacob Zuma


wapambetv7.jpg



Washabiki au wakereketwa wa CCM?



yyla7.jpg



Usafiri


Picha kwa hisani ya hakingowi.
 
Naomba niseme kidogo. Nimekuwa mfuatiliaji wa karibu wa JF kwa karibia mwaka. Nimegundua kwamba jamboforums kuna rangi nyingi sana when it comes to politics in Tanzania. Muhimu zaidi, wengi wa Jamboforums wanaonyesha bado wana imani na chama chao cha mapinduzi kwani wakati wa chaguzi hizi huwa wanakuwa wana base hoja zao zaidi on nini kitaimarisha au kuvunja chama. Ukweli huu huwa unazidi kujiidhirsha nyakati hizi za chaguzi ambapo wengi huwa wanakuwa na preferences za on nani awe au asiwe kiongozi ndani cha chama cha mapinduzi na kusahau kabisa how hizi development can or should shape upinzani. Mbali zaidi, kama kawaida, siasa za kusengenyana na kuanikana na vilevile kutafutiana kashfa humu jamboforums huwa hazikawii kujitokeza baada ya chaguzi. Hakika nyakazi za chaguzi za ccm ni muda mzuri sana wa kuchambua msimamo wa wana jamboforums wengi sana. wengi hawapo consisent na misimamo yao ya kisiasa. Hili ni bayana kama ukitumia muda wako kidogo kuangalia historia ya postings za watu kadhaa humu over time. In other words, wengi humu hawana dira. tusubiri matokeo ya NEC yapite na tutaona haya kwa mara nyingine tena.
 
Kazi,
Mjadala mzuri. Katika ilani kumi za Chama alizotaja. Ameongela moja baada ya nyingine na kuelezea zilivyotekelezwa so far.

Ukiangalia kwa makini ameongelea kuanzia walivyodhibiti Ujambazi mpaka tatizo la Umeme.

Kwa ufupi ni kuwa katoa mifano hai katika kila kipengele.
Yaani ilikuwa hotuba safi sana kaka, itafute uisome.

Mimi nimeleta to hints, ila kaka mimi huwa natazama pande zote za shillingi ndio maana utaona kuwa nimesema, HAKUONGELEA KWANINI MIKATABA NI SIRI. Ila kaongela kuundwa kwa tume huru, nyinyi wapinzani na viongozi wa dini mtakuwemo!

FD!
Kwangu mimi haya ni marudio kwani nilimsikia alipotembelea Nchi Moja Mwaka jana mwezi juni kama sikosei Halafu nikamsikia tena alipotembelea Asia.
yote alikuwa akituhutubia wa Tanzania na Aliyaeleza na kuyatolea mifano kama ulivyoanisha,Tangu nilipomsikia Asia ilikuwa mwezi kama huu yaani kwa kifupi mwaka umepita Lakini Hajayachukulia hatua yanayopaswa na ambayo alisema tunafanya hayajafanywa.Turudi kwenye swala la Madini alilisema hili kabla hajaingia madarakani na sasa miaka miwili ndiyo hiyo hajafanya lolote,Aliahidi kutoruhusu Mikataba mipya tumeshuhudia akiwepo kwenye nafasi yake hiyo mikataba mipya ikisainiwa,aliahidi kutatua tatizo la umeme tumeshuhudia mikataba ya kuleta umeme kusainiwa na alieleza ni kwasababu ya haraka ndiyo maana waliamua kukodisha majenereta ili kukabili hali ya ukosefu wa umeme pamoja na kuwa ghali Lakini hadi leo hii hayo majenereta hayajaweza kutatua tatizo la umeme na kuingiza umeme walioahidi wangeuzalisha ,Na tatizo lilikujatatuliwa angalau kidogo baada ya bwawa letu kujaa na kuruhusu maji kuingia kwa mvua za rehema za Mungu.Ndiyo ninasema haya yote na mengi yakiwemo ya wala rushwa ,ya kiwemo ya mahalu, ya kiwemo ya bodi ya mikopo LAKINI Hakuna waliowajibishwa na hakuna yaliyotekelezwa kama alivyosema na mwaka toka nimsikie kwa mara ya mwisho umepita na hata hili la kusafiri alisema watu wanalalamika kwamba nasafiri sana lakini ninawaeleza nitasafiri sana labda mpaka mwakani yaani april mwaka huu aliahidi angetulia nyumbani Lakini cha ajabu April imepita bado anakata mawingu tu,KWAHIYO Mh Rais anaongea yenye matumaini mara zote Lakini utekelezaji au usimamizi wa yale anayotueleza na kuyasimamia ni Duni au haupo KABISA.Kwahiyo na rudi kule kule kwenye hoja ya msingi kwamba sasa ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo yale anayotueleza au anayoyaongea na yasibaki kuwa ni simulizi za nenda rudi kwa kutumia ilani ya chama,tunaelewa ilani ni Nzuri ,tunaelewa anayotueleza ni mazuri,Lakini hatuelewi ni kwanini hayatekelezwi au yanatekelezwa kinyume na maelezo yake au na ilani ya chama, anacheza na amana tuliyompa.
 
FD

Unasema unatazama pande mbili za shilingi lakini ukweli wa mambo unaangalia upande wako wa CCM hadi unagombea ka-something. Nakutakia la kheri kwenye kinyang'anyiro hicho.
 
hilo kundi la watu 20 hapo ndio watu watakapochoka na hao watakaotajwa ! subirini mtasikia mtandao umerudi ??
Maneno yako mazito sana,hata mimi nayaona yamejikita katika matokeo yatakayojiri ambayo ndio yatakayo isambaratisha CCM,wenyewe kwa wenyewe,Ukichukulia kauli ya Muungwana akisema Wengine hata wakishindwa kwa kura moja halali, wanalalamika ,hapa pana ashiria matatizo ambayo amekwisha tonywa na alizidi pale alipo wapiga jembe wengine kwa kuchimba mkwala alisema Wale wanaotumia fedha zao zitapotea bure.Hapo kunaonyesha kuna watu ambao wanatumia fedha nyingi kusaka nafasi za NEC,aidha alikuwa akionyesha dalili za wazi watakaopita hawatakuwa na faida ndani ya chama zaidi ya kutafuta njia za kurudisha fedha zao,na hivyo chama kitapambana nao
 
Kazi,

Kuhusu kuchukua hatua amesema kesi ya Mahalu (hakumtaja) ipo mahakamani. Na tutegemee kesi 38. Kuna viongozi 38 wa serikali wanahojiwa sasa hivi...

Is it not a good move?, amesema kwa sasa even ukituma SMS wanaifanyia kazi, yaani hata majungu wanayafanyia kazi, kikieleweka ni mahakamani.
FD!
Ni kweli kama hayo ynafanyika ni hatua nzuri Lakini yanafanyika wapi?Kwa mfano Mahalu tunalijua na mwaka umepita hii hili ni credit Sasa kwanini anakwama hapo asiendelee kwa wengine ,Karamagi kusaini Mkataba wakati alisema hawatasaini mikataba mipya tena hili nalo amelielezaje au amemchukulia hatua gani? Waliolitia taifa hasara kwa kushauri Richmond ipewe tender na hatimaye kusainiwa mkataba na kwamba wangeweza kutatua tatizo letu la umeme nao wamefanywa nini?
 
JK msanii tu, anavuta muda na mambo yatabaki kama yalivyo. Maneno matupu hayavunji mfupa. Baada ya huu mkutano watafungasha mafaili na kufungua mengine lakini shehe ni yule yule kanzu ndio mpya.

Wawekezaji wapya wataingia kwa mbinu zile zile chafu na wanaoweka mikataba feki kama Karamagi wataendelea kutumia pesa ya walipa kodi bila aibu. Richimondulian atakuwa ndiye kinara na kasungura kake itabidi WTZ wote kawatoshe kama alivyosema Mzee ruksa unashona jacket (koti) kutokana na kitambaa ulichonacho.
 
Kazi,
Mjadala mzuri. Katika ilani kumi za Chama alizotaja. Ameongela moja baada ya nyingine na kuelezea zilivyotekelezwa so far.

Ukiangalia kwa makini ameongelea kuanzia walivyodhibiti Ujambazi mpaka tatizo la Umeme.

Kwa ufupi ni kuwa katoa mifano hai katika kila kipengele.
Yaani ilikuwa hotuba safi sana kaka, itafute uisome.

Mimi nimeleta to hints, ila kaka mimi huwa natazama pande zote za shillingi ndio maana utaona kuwa nimesema, HAKUONGELEA KWANINI MIKATABA NI SIRI. Ila kaongela kuundwa kwa tume huru, nyinyi wapinzani na viongozi wa dini mtakuwemo!.
Alichotakiwa azungumze mambo ya Chama chake na si mambo ya Serikali,maana ameonekana akilihutubia Taifa na wanachama waliokuwepo ndani ya ukumbi sijui amewapiga chenga,au alijisahau na kuona Tanzania nzima ni ya wana CCM kumbe yupo ndani ya ukumbi na wenzetu,ila mfahamuni Muungwana anachosema sicho anachokitenda,ndipo hapo amezungumza mengine kumbe ana yake mengine ,tusubiri matokeo.
 
Naomba niseme kidogo. Nimekuwa mfuatiliaji wa karibu wa JF kwa karibia mwaka. Nimegundua kwamba jamboforums kuna rangi nyingi sana when it comes to politics in Tanzania. Muhimu zaidi, wengi wa Jamboforums wanaonyesha bado wana imani na chama chao cha mapinduzi kwani wakati wa chaguzi hizi huwa wanakuwa wana base hoja zao zaidi on nini kitaimarisha au kuvunja chama. Ukweli huu huwa unazidi kujiidhirsha nyakati hizi za chaguzi ambapo wengi huwa wanakuwa na preferences za on nani awe au asiwe kiongozi ndani cha chama cha mapinduzi na kusahau kabisa how hizi development can or should shape upinzani. Mbali zaidi, kama kawaida, siasa za kusengenyana na kuanikana na vilevile kutafutiana kashfa humu jamboforums huwa hazikawii kujitokeza baada ya chaguzi. Hakika nyakazi za chaguzi za ccm ni muda mzuri sana wa kuchambua msimamo wa wana jamboforums wengi sana. wengi hawapo consisent na misimamo yao ya kisiasa. Hili ni bayana kama ukitumia muda wako kidogo kuangalia historia ya postings za watu kadhaa humu over time. In other words, wengi humu hawana dira. tusubiri matokeo ya NEC yapite na tutaona haya kwa mara nyingine tena.

..raia,sijui kama we ni mwema kweli,ila,karibu!

..hili baraza ni pana sana na lina kila aina ya watu,wenye kila aina ya msimamo na wengine hawana kabisaa!

..nadhani kitu cha muhimu si kuwa katika upande gani wa kisiasa,bali,ni uwezo wa kutoa mawazo ya nini kifanyike ili nchi yetu iweze songa mbele vizuri na kwa manufaa ya wengi!

..kuna kipindi issues zilikuwa zinakatwa hapa mpaka ilitia msisimko!hali si hivyo kwasasa!kwani majungu yamezidi!focus imepotea...unajikuta unaongea au kuchangia pumba!

..kama nilivyosema awali,hili ni baraza na baraza ni watu!sasa,kwenye wengi kuna mengi na ndio haya!ila,naamini ipo siku tutarudi kwenye kukata issues baada ya huu upepo mbaya wenye pepo baya utakapopita!

..wapo watu kama fd,dua,mjj,mkandala,philemon mikael,kithuku,jokakuu,masatu,invicible,kada,mwafrika wa kike,samvulachole,mtupori,fmes,drwho,mtumwitu,na wengine ambao nadhani wamebadilisha majina. hawa walikuwa wanakata ishu si mchezo...ila siku hizi....aagh!tuache huu upepo upite!

..kuwa na subra,hii ndio tanzania!
 
Yeah. Kusuhu mambo ya mafisadi kashamaliza. Makofi leo amna. Hata JK akisema CCM Oyee. Lakini wanaorespond ni kidogo. angalia nyuso za makada!

Makada wamekasirika walijua hiki ni kipindi chao cha mavuno makubwa (rushwa) toka kwa wagombea mbali mbali sasa wameula wachuya!
 
Back
Top Bottom