Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Wakili wa upande wa utetezi Moses Mahuna akieleza kuhusu Sabaya na wenzake
kushinda rufaa yao na kuachiliwa huru katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.
Sabaya na wenzake watatu wamebakiza ngwe moja ya hukumu ya kesi ya uhujumu uchumi baada ya Mahakama Kuu ya kumwachia huru muda huu. Warufani wengine katika kesi hiyo ni Silvester Nyegu na Daniel Mbura, waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka matatu ya unyang'anyi kwa kutumia silaha.
Oktoba 15, mwaka 2021, Hakimu Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Odira Amworo, alimtia hatiani Ole Sabaya na wenzake kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.
Ole Sabaya wakati akifikishwa Mahakamani kusikiliza rufaa yake Mei, 2022
Pia, soma=> Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha