Wataingia kundi la binadamu wakistarabika bt for now sio mbaya ukiwaweka kundi moja na nguruwe
Katika nchi yetu kumejawa na ufisadi, kila kukicha tunaibiwa. Na kila siku tunagundua tumeibiwa na tunawasema waliotuibia muda huo huo bila kujali nyazifa zao. Wapingazi wa ufisadi wako sehemu zote kuanzia ccm mpaka upinzani. Ccm wako wachache sana ni wa kuwahesabu! Kwamba huyu akisimama kukemea ufisadi ni ajenda yake ya siku nyingi na ni kweli anapokemea anamaanisha kile anacho kiongea.
Sehem muhimu ya kukemea ufisadi ni bungeni.
Nataka kukumbushwa kidogo kuhusu raisi wangu Mheshimiwa JPM. Kwa mtu yeyote mwenye kumbukumbu clip yeyote au maandishi yeyote aliyowahi kuyatoa bungeni kuonyesha kukelwa na ufisadi. Lini aliwahi kupinga ufisadi waziwazi .
Nani aliwahi kumsema kwa ufisadi wake iwe ndani ya serikali au nje ya serikali. Binafsi Rais Wangu simwoni kama zao la wapingaji wa ufisadi. Tukumbuke tabia ya mtu haitokei ghafra ni hulka yake ya siku nyingi.
Binafsi sina kumbukumbu ya siku yeyote akikemea ufisadi kabla ya kuwa rais. Zaid zaid naona ufisadi uliofanyika chini ya wizara yake na hajawahi kuzitolea ufafanuzi. Najiuliza lini alibatizwa na kuwa muumini wa kupinga ufisadi?? Bungeni kuna wabunge wa ccm waliwahi kuukemea ufisadi mfano marehemu Filikunjombe. Hata olesendeka kabla hajapewa hiyo mic. Lini rais aliwahi kuukemea ufisad? Waumin wake hebu nileteen data kidogo nijiridhishe. Ila mimi nawaletea ufisad uliofanyika chini yake.
Meli ya mv bagamoyo. Hela zetu zimeenda bure..
Kuna billion 200. mkaguzi mkuu aliwahi kuzisemea hazieleweki zimetumika wapi na hajawahi kuzitolea ufafanuzi. Pia mimi ni mdau wa ujenzi katika secta ya ujenzi kumejawa na rushwa ile mbaya na hilo eneo amelisimamia kwa kipindi kirefu. Angekua muumini wa kuupinga rushwa angeinyoosha wizara ya ujenzi tenda zipatikane bila ten % . Lakn nawahakikishia na kwa wale wanaojishughulisha na shughuri za ujenzi wataniunga mkono.huwez pata tenda ya serikali bila kutoa rushwa kwa kamati zinazopitisha miradi ya ujenzi. Hiyo imepelekea barabara zetu kuwa mbovu. Kabla barabara haijaisha unakuta nyuma imefumuka.
Majengo yenye gharama ndogo kujengwa kwa gharama kubwa. Na tena yakiwa chini ya kiwango. Usije shangaa darasa la shule kujengwa kwa milion 60 wakati ungepewa wewe hiyo hela ungejenga kwa milion 10. Yeye ndio alikua msimamizi. Hivyo binafsi namwona yeye ni chanzo cha ufisadi katika wizara ya ujenzi.
Kutokana na hayo hapo juu sioni sura na tabia ya rais wetu kuwa mpingaji wa ufisadi. Ndio kwanza kakutana na Lugumi kakaa kimyaaaa. Escrow imerudi tena tuwalipe hela zingine staili nyingine, yuko kimyaaaaaa. Amebaki kukimbizana na wafanyakazi yaan watumishi hewa kana kwamba hilo ndio tatizo kuu la hii nchi. Zaid naona maneno yenye kuonyesha kuuchukia ufisadi ila sion matendo kutoka kwake. Jambo ambalo anaonekana amechukua kauli mbiu ya wapinzani ili naye aonekane ni muumini wa upingaji wa ufisadi wakati yeye si muumini.
Nawakumbusha tena waumini wa Magufuli kaanza lini kuuchukia ufisad?? Alikua anasubili awe rais??
Huko nyuma amelisaidiaje taifa katika kukemea ufisadi???
Naomba clip za Rais magufuli akiwa mbunge akikemea ufisadi bungeni.