ndugu yangu
Nicxie huku Tz sio kila raia ananunua unga, idadi kubwa ya watanzania ni wakulima (wanamiliki mashamba) hayo mahindi ukitoa gharama za kilimo, kinachowagharimu kingine ni pesa ya kukoboa na kusaga (hii ni kama Tz sh 200 tu) .. na wengi wasio na mashamba hununua mahindi na kwenda kusaga wenyewe .. kwahyo number kubwa ya wabongo hutumia pesa kidogo tu kwaajili ya msosi.. hizo mboga mboga ndio usiseme ukiachana na DAR mikoa mingi ya Tz karibu kila nyumba (za waTz maskini au wa maisha ya kati) utakuta kuna bustani za mboga mboga, kwamfano Arusha katikati ya mji wao (jijini) kuna bustani za mboga mboga kibao.. kwahyo msosi bongo sio noma na ndio mana huwezi kuona tunaandamana eti kisa kukosa msosi.. na vile tumebarikiwa kila aina ya mazao bongo yanaota ..