7seven
JF-Expert Member
- Mar 27, 2022
- 3,744
- 8,065
Ninachotetea ni kuwaingiza TISS kwenye mambo ya kijinga ya uchonganishi. Hivi kweli taasisi nyeti inayolinda usalama wa Taifa na raia wake kwamba iko Kenya inaratibu mchakato wa kuiba kura nisimame mbele na kupongeza kwamba ni sahihi kweli mkuu wangu?Mkuu, hawa wakenya usiwatetee kwa lolote sio watu wazuri hata kidogo, Lissu yupo Belgium lakini wanamuamini na kutumia maneno yake kuikandamiza na kuipinga Tanzania, vipi unasema kwamba Miguna yupo Canada hawezi kujua kinachoendelea Kenya?
Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
Kama ningeambiwa ni CCM wanamsupport mgombea fulani ningeona kidogo ni sawa maana wote ni wanasiasa lakini TISS, JWTZ na POLISI wapo kwenye nchi ya watu,raia wa hiyo nchi wanaitafsiri vipi, je wakiamini wakalipa kisasi tutakuwa tumejipostion vipi.
Chuki na fitina zozote kwenye nchi yetu tuzipinge kwa hoja na kutanguliza Uzalendo mbele hasa zile zinazogusa na kuhatarisha Usalama wa Taifa.
Hivi mkuu unajua siyo kila taarifa ni habari sahihi, na siyo kila ukweli unaoujua ni lazima uuseme hadharani, vitu vingine tupige kimya huu ndio Uzalendo kwa nchi yetu.

