Bado napenda Tanzania na bado naamini uchumi wenu upo under-valued. Nimesema hivyo kwa muda mrefu sasa kwamba kulingana na miradi mingi inayoendelea Tanzania na kwamba mnaeexport chakula ukanda wote huu na munauza dhahabu ya $3 billion kwa mwaka, uchumi wenu haustahili kuwa mdogo hivyo. Gdp yenu inastahili kuwa mkubwa kushinda hio $70 billion ambayo serikali huwa inataja. Halafu mumekwama hapo kwa $60-70 billion kwa miaka mitano au sita sasa japo uchumi wenu unakuwa kwa asilimia 5 au 6% kila mwaka. Licha ya kurebase uchumi wenu mwaka wa 2014 na 2019 bado uchumi wenu umekwama pale pale. Tatizo liko wapi ikiwa nchi kama Ethiopia ambalo lina a more primitive economy linashinda uchumi wenu kwa ukubwa? Mimi huwa ninashuku Tanzania bureau of statistics haina ujuzi unaofaa na wanahitaji msaada kutoka nje ili waweze kupima ukubwa wa uchumi wenu vizuri.
Kuna uwezekano wameshindwa kuzingatia sector mpya zinazoingia kwenye uchumi wenu kwa mfano boda boda wa pikipiki wamekuwa wengi sana miaka mitano zilizopita hapa Africa mashariki, hii lazima izingatiwe kwenye kucalculate mapato ya nchi kama sub-sector mpya ya transportation and logistics. Na mambo ya internet nayo imechipuza biashara mpya kama ya kuuza na kuchuuza bidhaa kupitia mtandao. Halafu miradi mikubwa kama JNHPP ambayo ni takriban $2.5 billion na SGR yenu ambayo ni zaidi ya $4 billion, unaweza imagine kama ni cement au vyuma vinanunuliwa ndani ya nchi basi ni cement ngapi zinanunuliwa hapo? Miradi za daraja ni cement ngapi zinanunuliwa hapo? Ni watu wangapi wanapokea mishahara wanaofanya kazi kwenye miradi hii? Yaani itakuwaje uchumi wenu umekwama kwenye $60 billion kwa miaka mitano? Haiwezekani, lazima kuna tatizo mahali.
Mimi huwa naona uchumi wenu umekaribia wetu na unastahili kuwa around $90 billion. Lakini hio ni maoni yangu tu kwa sababu sijakaa chini na kupitia ripoti ya gdp yenu kwa undani kama nilivyofanya ya Kenya. By the way, Imf wana kitengo maalum ya kusaidia nchi masikini kuboresha statistical reporting capacity zao. Nchi nyingi za Africa zipo hovyo sana katika kupima ukubwa wa uchumi zao. Kuna nchi za central Afrika ambazo hazijawahi kurebase uchumi zao kwa zaidi ya miaka ishirini. Nchi nyingi za Afrika zipo hovyo sana kwenye suala hili. Inawezekana Kenya tunabahatika kupata training na maarifa kutoka Imf na World Bank kwa maana taasisi hizi zina regional headquarters hapa Nairobi. Halafu Kenya sisi tunapenda kujipendekeza kwa wazungu so unakuta Wafanyikazi wa KNBS wanapata training kila wakati jinsi ya kupima na kuclassify different sectors za uchumi. Wafanyakazi wa KNBS huwa wanakwenda hadi ulaya kupata trainings kila uchao kwenye masuala ya kumeasure, kuclassify na kureport different sectors za uchumi. Tieni bidii kidogo kwenye hili. Nchi kama ya South Afrika ipo mbele sana kwenye suala hili kiasi cha kwamba wao hurebase uchumi wao kila baada ya mwaka mmoja badala ya kila baada ya miaka mitano kama tunavyofanya Kenya na Tanzania. South Afrika wao wanarebase kila mwaka kwa sababu wana pesa na ujuzi na wataalam wa kutosha.