Sababu kuu ni kuwa sisi sio watumwa nchini kwetu.
Mtanzani wa kawaida kabisa anauwezo wakumiliki ardhi na kufanya biashara ndogo ndogo, na kama anaakili za ujasiliamali anaweza kutajirika. Hakuna nchi yoyote Afrika kufananisha na Tanzania kwenye maendeleo yanayojumuisha watu wote.
Pili, hati za kusafiria Tanzania zilikuwa hazitolewi hovyo hovyo na kuanzia 2016 serikali ilianza tena kubana kutoa hati.
Kipindi cha zamani (enzi za Nyerere) ilikuwa ni lazima upate 'exit visa' (kibali kutoka serikalini) kabla ya kuondoka nchini. Hii ilifanya watanzania wengi kutojisumbua kuondoka, na hata walipoondoa masharti bado wengi wakawa hawataki kuondoka.