Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Picha: Kushoto ni Freeman Mbowe, Kulia ni Amosi Makalla
Katika hatua ya kuonesha kujipendekeza kulikopitiliza, RC Amos Makalla amesema:
"Rais Samia Kuna watu eti wanakukosoa kwa maboresho ya Bandari zetu ilhali umefanya jambo hilo kwa uwazi Bungeni kama Azimio. Yeye Mbowe (Freeman) hasemi kama wameanza kupokea ruzuku tena kachukua Bilioni 2 na kusweka mfukoni kwake kimya kimya. Sasa nani muwazi kati Yako na yeye".
Makalla amesema hayo mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan katika tamasha la utamaduni Bulabo hapa Mwanza.
Chanzo: TBC1