State Capture: Mamlaka ya Rais Samia yanapoharibiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa yanayotokea Mwanza

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Unaweza sema Mamlaka ya Rais Samia imetekwa( State Capture) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Ni katiba mpya tena vyombo vya habari vya Kimataifa vinamtaja Rais Samia kama kinara wa kukandamiza haki na Demokrasia Tanzania kwa kuwakamata viongozi wa Chadema mjini Mwanza Tanzania

Mtu mmoja na ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza anaamua kujichukulia mamlaka ambayo hayapo kisheria kuzuia uhuru wa watu kutoa maoni juu ya Taifa Lao wanataka liwe na muundo upi (Katiba Mpya)

Propaganda kama zilizofanyika wakati wa hayati Magufuli, Matokeo yake yameonekana sasa na hili Rais Samia amekiri wawekezaji walikimbia na Uchumi wa nchi umeporomoka kutoka asilimia 7% mpaka asilimia 4%

Katikati ya Taifa lililogawanyika kutokana na watu wake kugawanywa kikabila na Kichama na mtangulizi wa Mama Samia, Sasa Rasmi jina la Rais Samia limeanza kuchafuliwa Kimataifa kwa kosa la mtu mmoja na ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza aliyewakamata viongozi wa Chadema usiku wa manane akiwemo Mwenyekiti wa chama Taifa Mh. Freeman Mbowe

Matokeo ya sera hizi za kuminya haki na uhuru yanaenda kugusa Uchumi ulioporomoka moja kwa moja na kuathiri Sekta ya uma na binafsi

Mosi, Sera za Mama hazitabiriki tena kwa wawekezaji wa Kimataifa ambao wanahitaji taarifa za uwazi na ukweli, Uchumi utaenda kuporomoka zaidi na hivyo mwakani hakuna tena ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi

Pili, Kuendelea na wafuasi wa Rais aliyemtangulia kama mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambao wamezoea kujitwalia sheria na Mamlaka ya Rais mkononi, Hakuna mwekezaji atakaye wekeza kwenye mikoa ya namna hiyo na hili Rais Samia alipaswa kuliona kwa jinsi Ole Sabaya alipoharibu Mali za wawekezaji, Tutegemee anguko kubwa la bei za mazao ya wakulima

Tatu, Chuki juu ya Chuki imeanza kutamalaki tena, Funzo la mtangulizi wa Mama Samia kwa yaliyotokea kila mtu anamtazama Rais Samia kwa macho matatu, Jicho la tatu limeshaamini Tozo za miamala ya simu na Ukamataji wa wanasiasa, Rais Samia ndie anawatuma kuyafanya haya, Bila kuunganisha Taifa lolote utakalofanya ni sawa na kazi bure

Ushauri
Taifa kwa sasa linahitaji kupumua kutokana na Funzo kubwa toka kwa Rais aliyemtangulia Mama Samia, Kupumua kwa Taifa ni watu kutoa maoni yao juu ya Taifa Lao, Watu kuponya majeraha yaliyoachwa na utawala kabla ya Rais Samia, Kuzuia maoni ya wananchi ni kutengeneza chuki isiyotibika ambayo baadhi ya watu walishangilia kifo cha mtangulizi wa Mama Samia

Madhara yaliyofanyika Kimataifa ya nahitaji kuponywa na walioyaongea Kimataifa, Ni muda wa kuwaunganisha watu wenye exposure Kimataifa ambao tayari wanaaminiwa na vyombo vya habari Kimataifa kwa taarifa kama za Leo kukamatwa Kwa wafuasi wa chadema tayari vyombo vya Kimataifa vimewahoji watu hao kuhusu aina ya sera na utawala wa Rais Samia

Nguvu ya watu waliopo mtandaoni Twitter na hapa Jamii Forum wanasukuma agenda kimkakati sana Kimataifa, Rais mtangulizi kabla ya Mama Samia alijaribu kuzuia hii mitandao lakini ndio iliyomuonyesha Kuwa hajali sera za Kimataifa na utengamano na ilipelekea anguko kubwa kama Taifa
 
Unamsingizia mkuu wa mkoa Kwa lipi we kiroboto , mkuu wa mkoa anaweza ingilia masuala ya kisiasa ana benefit nayo kivipi , hakuna mkuu wa mkoa anayeweza kufanya maamuz mazito kama yale bila high command , huu upumbavu sijui mtauacha lini , mwambie akuteue wewe bas na mkeo
 
Unamsingizia mkuu wa mkoa Kwa lipi we kiroboto , mkuu wa mkoa anaweza ingilia masuala ya kisiasa ana benefit nayo kivipi , hakuna mkuu wa mkoa anayeweza kufanya maamuz mazito kama yale bila high command , huu upumbavu sijui mtauacha lini , mwambie akuteue wewe bas na mkeo

Shida yake JPM. Yani anapambana na marehemu. Ndo mana.
 
Nilisikia eti Magufuli hajawahi safiri kwenda nje zaidi ya Afrika.
Jibu
Hakupata mialiko kutokana na Sera zake.
Uhuru Kenyata alialikwa hadi na Papa
Tujifunze
 
Nilisikia eti Magufuli hajawahi safiri kwenda nje zaidi ya Afrika.
Jibu
Hakupata mialiko kutokana na Sera zake.
Uhuru Kenyata alialikwa hadi na Papa
Tujifunze
Alipopata hiyo mialiko siku hizi kenya hawana shida, ni mbinguni hakuna kufa wala hakuna shida yoyote wamepta baraka zote kutokana na hiyo mialiko.
Watu wake wana laha kama ya malaika,
Hawalimi wala hawafanyi kazi, wanakula ma kucheza kisha kulala tu, na wakimuimbia uhuru adumu milele hapo kenya 😁😁😁😁😁
 
Mnatumia nguvu kubwa sana,alafu haiwasaidii kwasababu huku mitaani raia hawana time hata,yani wapowapo tu kwenye mishe zao.
 
Mkuu wa mkoa hahusiki maana hawezi fanya aliyofanya bila kupata baraka za Rais,kauli ya kwamba watu wameanza choko choko ilyotoka kwa Rais ndio chanzo na practically amewaagiza polisi kudhibiti upinzani uku akijificha kwa watendaji. Watu waoga ni hatari sana!

Rais SSH ameshachafuka tutarajie ajae maana huyu tumeshamuona na zama zake hazitadumu,zinapotea kwa kasi sana
 
RC ni CHAWA wa raisi kwaiyo ukiona maagizo kayatoa rc ujue ni raisi ndiye aliyetoa. Lazima wafanye hivyo kwa sababu moja ya kundi litakaloadhirika na katiba mpya ni pamoja na maRC
 
Ninajibu kichwa cha habari yako mkuu, kwa maana sikusoma yaliyo ndani yake.

Hakuna kitu kama hicho cha "Mamlaka ya rais Samia kuharibiwa na mkuu wa mkoa..."

Mkuu wa mkoa au mtu mwingine yeyote hawezi kamwe kumharibia rais, atajiharibia mwenyewe. Mkuu wa mkoa hawezi kuwa na uwezo huo wa kumharibia rais.

Sasa sijui haya mawazo ya "rais kuharibiwa" huwa watu wanayatoa wapi, na kwa nini hawaamini kwa nini rais akawa anajiharibia mwenyewe!
 
Hawa wote ni maharamia na kwa pamoja yafaa kuiomba jumuia ya kimataifa kuwatazama kwa uzito kama wale maharamia wanaosumbua ukanda wa bahari ya hindi eneo la ukanda wa karibu na afrika mashariki na karibu na somalia.
 
Nilisikia eti Magufuli hajawahi safiri kwenda nje zaidi ya Afrika.
Jibu
Hakupata mialiko kutokana na Sera zake.
Uhuru Kenyata alialikwa hadi na Papa
Tujifunze
Siasa za Tanzania ni za ajabu sana
Unahubiri umoja na upendo huku ukitengeneza chuki kubwa
 
Hii nchi ni lini watu watajikita kwenye uzalishaji??

Kila siku ni siasa tu yaani porojo tu hakuna anayetaka kuzalisha.
 
Wawekezaji wababaishaji hatuwataki wabaki huko huko. Uhuru bila mipaka siyo uhuru tena bali ni upumbavu.
 
Mkuu umeandika vizuri , ila Binafsi nakataa kwamba RC MWANZA anaweza fanya haya bila baraka kubwa TOKA juu, NAKATAA, hakuna namna SSH RAIS ANAWEZA JITENGA NA HILI, ANAUSIKA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom