chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. GE2020 CHADEMA Tunduma: Wananchi wakimsindikiza Mwakajoka kuchukua fomu za Ubunge

    TUNDUMA MAMBO MOTO. Wanachama wa chadema na Wananchi jana wamemsindikiza mbunge wao Frank Mwakajoka Kuchukua Form ya Ubunge Jimbo hilo... #niyeye2020
  2. J

    Wateule wa Rais Magufuli waliotokea CHADEMA wameongoza kwenye kura za maoni isipokuwa Patrobas Katambi

    Bado natafakari tetemeko la ardhi lililotokea jana katika eneo kubwa la nchi yetu huku nikisubiri orodha ya wagombea ubunge wa CCM itangazwe. Wateule wa Rais Magufuli waliotokea CHADEMA akina Juliana Shonza, Prof Kitila Mkumbo, Dr Mollel na Mwita Waitara wameongoza kwenye kura za maoni...
  3. GE2020 CHADEMA Kyela tunasubiri kwa hamu kumdhamini Lissu

    Kyela ndio mwanzo wa nchi yetu kutokea Malawi na ndio mwisho wa Nchi hii ukitokea Dar es Salaam , unapotokea Malawi bendera ya kwanza ya chama cha siasa unayoiona unapovuka boda tu ni bendera ya Chadema , hii ndio bendera ya mwisho ya chama unayoweza kuiona pale boda kabla hujavuka kwenda Malawi...
  4. J

    Nimeshangaa kuwakuta CHADEMA Mpwapwa!

    Mara kwa mara nimekuwa nikitembelea mji wa Mpwapwa na Kibakwe kwa shughuli za kilimo lakini sijawahi kuona dalili za uwepo wa CHADEMA wilayani humo. Leo nimeona mtandaoni kuwa polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanachadema wa Mpwapwa waliokuwa wanawasindikiza wagombea wao kuchukua...
  5. CHADEMA nawapongeza sana kujigawa kikanda kueneza chama

    Huu utaratibu wenu naona umekua wa mafanikio sana na umuwasaidieni kuwafikia wananchi kwa haraka sana. Nimeona jinsi viongozi wenu wa kanda walivyojipambanu siku ya mkutano mkuu wenu, inaonekana kila kanda inawajibika ipasavyo. Pengine hiki ndicho kitu ambacho kimemfanya chama chenu kuanguka na...
  6. GE2020 Ushauri: Ili kuepuka hujuma Fomu zote za wagombea ubunge na udiwani wa CHADEMA zipitie ofisi za kanda kuhakikiwa

    Huu ni ushauri ninaoupeleka kwenye ofisi ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, Mh John Mnyika kwamba wagombea watakapozichukua fomu hizo kutoka kwenye ofisi za Tume ama kwa Wakurugenzi baada ya kuzijaza basi ni vema zikahakikiwa na ofisi kubwa kabisa za kanda ili kuondoa uwezekano wowote wa kukataliwa na...
  7. GE2020 Msemaji wa Serikali, Dkt. Abbas: Suala la CHADEMA kuongeza ubeti wao katika wimbo wa Taifa tumemuachia Msajili wa Vyama vya Siasa

    SUALA LA CHADEMA TUMEMUACHIA MSAJILI WA VYAMA Masuala yote yanayohusu maudhui ya utangazaji kisheria yapo chini ya Waziri mwenye dhamana ya habari, Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 pia imefafanua hilo, Sheria inatungwa lakini Kanuni zinatungwa na Mamlaka inayotekeleza sheria hiyo...
  8. J

    Japo hawezi kushinda kiukweli, CHADEMA imemtendea haki Tundu Antipas Lissu!

    Kitendo cha kamati kuu ya CHADEMA kumpitisha Tundu Lissu kuwa mgombea wa urais huku ikimuweka pembeni bilionea Lazaro Nyalandu ni cha kizalendo ndani ya chama. Niwapongeze wajumbe wa CHADEMA kwa kutoyumbishwa na kurudia makosa ya kuzungusha mikono kama 2015. Hapa Lumumba tunasubiria majina ya...
  9. S

    Habari ya Mgombea Urais kupitia CHADEMA ndugu Tundu Lissu yaandikwa na waandishi 14

    Katika gazeti la Mwananchi la tarehe 11/8/2020 yenye kichwa cha habari kinachosema "SIMPITISHI YEYOTE MATESO HAYA" habari hii yenye paragrafu 29 imeandikwa na waandishi 14, ambao ni Daniel Mjema, Bakari Kiango, Andrew Gasper, Mussa Juma, Rachael Chibwete , Twalad Salum, Rehema Matowo, Ernest...
  10. J

    GE2020 Hesabu hazidanganyi: CCM wataongezewa kura za Lowassa na CHADEMA watapunguziwa kura za Lowassa, CUF na NCCR Mageuzi

    Ni kwamba CCM na Dkt. Magufuli tayari wana mtaji wa kura walizopata 2015 na watafaidika na kurejea kwa mzee Lowassa ambaye ana ushawishi mkubwa. Kura za CCM zitaongezeka. CHADEMA na Tundu Lissu watazikosa kura za CCM ( kupitia Lowassa) walizopata 2015 kadhalika watazikosa kura za UKAWA yaani...
  11. Q

    GE2020 Singida, Iramba: Mamia ya wananchi wa Shelui, wamemzuia barabarani Mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu ili awasalimie

    Mgombea Urais wa JMT kwa tiketi ya Chadema Mhe. Tundu Lissu akiwasalimia mamia ya wananchi katika Mji wa Shelui, Jimbo la Iramba, leo Jumanne Agosti 11, 2020 waliosimama barabarani na kumzuia kwa muda wakimtaka asimame na kuwahutubia kwanza kabla hajaendelea na safari.
  12. S

    Baada ya vyombo vya habari kuwekewa pingamizi kuhusu habari za Lissu, sasa mmeelewa kwanini CHADEMA walizuiwa kuingia uwanjani msiba wa Mkapa?

    Wengi walidhani kwamba Chadema walichelewa kuingia uwanjani kwenye msiba wa Mkapa na ndio maana walizuiwa kuingia. Hata account ya Sugu ilidafuliwa kupandikiza wazo hilo. Yote haya yalikuwa mpango maalum. Njama. NIlieleza wazi kwamba habari kutoka jikoni zilieleza wazi kwamba kwa makusudi...
  13. Hotuba za Mgombea urais kupitia CHADEMA ni nzuri sana, haziwezi katu kurushwa live!

    Kwa mnaofuatilia YouTube channel ya CHADEMA MEDIA TV utakubaliana nami, kila atakaposimama Lissu, unaona nyuso za tabasamu kwa wananchi. Wananchi wanakuwa wakimsikiliza kwa makini kana kwamba yeye ndiye Rais, hanunui jogoo wala hatoi zawadi kwa wananchi maskini lakini wote wanatabasamu. Kila...
  14. GE2020 Baada ya Kamati Kuu CHADEMA kumpitisha Alinanuswe Mwalwange kugombea Ubunge Kyela, wananchi walipuka kwa Shangwe, vifijo vyatawala

    Hii ni kwa sababu kwa miaka mingi sana jimbo la Kyela limekosa mbunge ambaye ni Mkazi halisi wa Kyela , kwa zaidi ya miaka 15 Kyela imekuwa na mbunge mpita njia, Mwakyembe alikuja Kyela kuomba kura ama kuja kuzika ndugu zake na kujiondokea zake , akirudi tena basi labda kuna ziara ya Waziri Mkuu...
  15. CHADEMA mjitafakari kwa hili

    Haingii akili ninyi kama Chama Kikuu cha Upinzani kwa zaidi ya miaka kumi kukosa TV ya kurusha mikutano yenu mubashara! Nashindwa kuelewa idara yenu ya uenezi inafanya kazi gani? Kama imekufa pia mtuambie tujue moja! Leo mtu akitaka kujua Tundu Lissu aliongea nini baada ya kuchukua fomu ya...
  16. GE2020 CHADEMA na ACT Wazalendo msiingiwe na tamaa fanyeni makubaliano ya Hekima, nafasi ya kushinda Urais Ubunge na Udiwani mnayo

    Nataka kuwashauri viongozi wakuu wa vyama hivi vya upinzani ambavyo vinaonekana kukikosesha usingizi chama chetu cha CCM upande wa bara na Visiwani.Msikosee hapa kwa tamaa za muda mfupi, kuweni na long term plans. URAIS Urais kwa Upande wa bara mwachieni Tundu Lisu wa CHADEMA agombee na...
  17. J

    Mgombea urais wa CHADEMA anaposhindwa kutafsiri maana ya fedha za ndani, atatuvusha kweli?

    Ni lazima watu wakaelewa mkopo unapatikanaje? Mkopo siyo msaada au zawadi bali ni fedha unayopewa na mkopeshaji kulingana na uwezo wako kilasirimali. Hivyo uwezo wako wa ndani ndio factor kuu ya maamuzi kama unakopesheka ama la. Kule India kwa mfano kuna utaratibu wa mkopo kulipwa kwa mkopo...
  18. GE2020 Kampeni za Uchaguzi mkuu - 2020 mitandaoni ni mtifuano wa kufa mtu kati ya TEAM Tundu Lissu (CHADEMA) vs TEAM John Magufuli (CCM)

    This is very interesting, kwa kweli... Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC), kampeni rasmi za kila mgombea za nchi kavu, angani au majini za kutembea kijiji kwa kijiji, kata kwa kata, jimbo kwa jimbo Tanzania nzima zitaanza trh 26/8/2020.... Lakini kampeni zisizo rasmi za MTU kwa MTU...
  19. GE2020 Orodha ya wagombea wa ubunge wa CHADEMA Tanzania Bara Oktoba 2020

  20. CHADEMA Media nawaona kama mnapwaya mno

    CHADEMA Media mmezubaa mno, hivi inakuwaje mnashindwa kufanya Livestreaming ya matukio ya Mgombea wetu hadi tunaanza kubambiabambia platforms zingine ambazo zinafanya censorship kubwa sana katika kureport matukio ya Kipenzi chetu, Mteule aliyeyashinda mauti Tundu Antiphas Lissu? Yaani mnazubaa...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…