Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT Wazalendo msiingiwe na tamaa fanyeni makubaliano ya Hekima, nafasi ya kushinda Urais Ubunge na Udiwani mnayo

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Nataka kuwashauri viongozi wakuu wa vyama hivi vya upinzani ambavyo vinaonekana kukikosesha usingizi chama chetu cha CCM upande wa bara na Visiwani.Msikosee hapa kwa tamaa za muda mfupi, kuweni na long term plans.

URAIS
Urais kwa Upande wa bara mwachieni Tundu Lisu wa CHADEMA agombee na visiwani mwacheni Maalim Seif Agombee, najaribu kusema hivi ni kutokana na aina ya Wagombea wa CCM tulionao.Kwa bara Dr Magufuli kupambana na Lissu ni sahihi kabisa kulingana na siasa za hawa wawili za ukali na za kutoogopana. Ni wanasiasa wachache sana Tanzania wenye ujasiri wa kuikosoa serikali ya CCM hadharani bila kuogopa ukimtoa Tundu Lisu.
Upande wa Zanzibar hapa siwezi kuongea sana kwa sababu iko wazi kabisa kua Maalim Seif siasa za huko yeye anauzoefu nao na ndiyo nafasi yake.

Ningemuomba Mzee wangu Benard Membe atulie tu maana anayo nafasi kubwa sana ya kupata nafasi za juu serikalini upinazani ukishinda na hata kua PM, anayo nafasi hata ya Spika wa bunge la Jamhuri ikiwa mtakuwa na sayansi nzuri ya kugawana majimbo kiufundi kisha mkaachiana.
ACT bara msihangaike na Urais kwa sababu bado chama chenu hakijawa na ushawishi mkubwa sana kama ilivyo Zanzibar,bara Urais mking'ang'ania hamtashinda kuliko ambavyo mngetafuta wabunge wawasaidie kuongeza nguvu na nje ya bunge .Kwa bara CHADEMA ndio wenye Ushawishi mkubwa karibia 20 ya mikoa ya Tanzania bara ukiachia ile michache 5 ya Pwani ambayo ACT mtakua na nguvu kiasi.

UBUMGE
Msikomalie Urais mkaacha kukitwaa Chombo hiki muhimu cha kufanya maamuzi, Maana mkilitwaa bunge hata Rais akitoka CCM hatoweza kufanya chochote bila ya Spika kuamua, yaani sawa na Democratic na republican vya USA.
Pigeni na kisha zichangeni hesabu zenu vizuri kuachiana majimbo, sahihisheni mapema kwa kushirikiana wote mfute madhaifu ambayo CCM wamekua wakiyatumia kuwashinda.
Wekeni wagombea wenye ushawishi kwa umma, wapeni elimu za namna ya kumudu uchaguzi ikiwa bado ni mapema. Chukueni form mapema mzipitie na wanasheria wenu kifungu kwa kifungu kisha zirejesheni mapema msiwape nafasi wakurugenzi kuja kufanya yao.
wawikeeni mapingamizi mapema wagombea wa CCM wasio na sifa msisubiri ninyi kuja kuwekewa muenguliwe, waengueni wao wenyewe.

UDIWANI
Hizi nafasi ni muhimu sana, ndiyo zinakipa Chama kulitwaa Halmashauri za miji,Wilaya, manispaa na jiji. Mkipata madiwani wengi ndivyo mtakavyopatq halmashauri nyingi zikawa chini yangu. Hii itawarahisishia sana kuimarisha na kutekeleza sera zenu bila bughudha.

HESABU HII LAZIMA MUENDE NAYO.
Ikiwa Jimbo X lina wapiga kura 10, CCM inaweza kupata kura 4, CHADEMA kura 3 na ACT 2, Maana yake mkiungana mtapata kura 6 na mbunge mliyeemuunga mkono ninyi lazima ashinde.
Ni hivyo hivyo hesabu ni ile ile kwenye Urais na Udiwani.


SHTUKIENI NJAMA NA UJANJA HUU WA CCM MAPEMA.
Kuna tetesi kua kuna mbina ya siri sana imeanza kutumiwa na CCM kuwashawishi wagombea wenu kuwapa madau manono waachie majimbo waunge mkono juhudi wakati wa kampeni na ninyi mbaki bila wagombea wao wapite bila kupingwa.Tetesi hizi zipo na ni mkakati kwa kila jimbo na kila kata.Watu wenu wengi bado wana njaa na tamaa, mkifeli katika hili mmekwishaa.
wapimeni watu wenu mapema kabla hawajachukua forms za kugombea.Litaftieni mwarobaini wake haraka iwezekanavyo.Msiponielewa nawapa pole sana na shauri yenu.
 
Kweli kuishi kwingi kuona Mengi.
1. Leo tunaongelea Act na Chadema kama vyama vya upinzani vyenye ushawishi nchni
2. Nccr ya James Mbatia baada ya kununuliwa na ccm ndio imejifia rasmi
3. Cuf iliyosumbua wakati wa Kikwete mwaka 2000 leo haijulikana hata ilipo.
4. Tlp ndio ilishajifia.

My take hivi vyama vya kipuuzi kama Cuf, tlp na nccr mageuzi na vinginevyo vingefutwa tu ili vibaki vitatu tu, na ikitokea chadema wameshinda basi na ccm nayo ifutwe.
 
Makubaliano yalishavunyika tokea walipo mlazimisha Lissu apande jukwaani na kucheza muziki wa ACT. Ni Zitto tu ndio analazimisha miungano. Kwa upande wa Chadema, uhusiano wao na Zitto ilikufa pale pale Arusha.
 
Makubaliano yalishavunyika tokea walipo mlazimisha Lissu apande jukwaani na kucheza muziki wa ACT. Ni Zitto tu ndio analazimisha miungano. Kwa upande wa Chadema, uhusiano wao na Zitto ilikufa pale pale Arusha.
Hizi ni hisia, ni fair kabisa Lissu kupewa bara na Maalim Seif kupewa Zenji
 
Kweli kuishi kwingi kuona Mengi.
1. Leo tunaongelea Act na Chadema kama vyama vya upinzani vyenye ushawishi nchni
2. Nccr ya James Mbatia baada ya kununuliwa na ccm ndio imejifia rasmi
3. Cuf iliyosumbua wakati wa Kikwete mwaka 2000 leo haijulikana hata ilipo.
4. Tlp ndio ilishajifia.

My take hivi vyama vya kipuuzi kama Cuf, tlp na nccr mageuzi na vinginevyo vingefutwa tu ili vibaki vitatu tu, na ikitokea chadema wameshinda basi na ccm nayo ifutwe.
Haviwezi kufutwa ni kielelezo kua Tz kuna demokrasia ya kweli.Mtaviambia nini vyombo na jumuiya za kimataifa?
 
Haviwezi kufutwa ni kielelezo kua Tz kuna demokrasia ya kweli.Mtaviambia nini vyombo na jumuiya za kimataifa?
Sioni umhimu wa kuwa na utitiri wa vyama ambavyo havina msaada wowote kwa maendeleo ya taifa badala yake vimegeuka kuwa parasites.

Vikibaki hata vitatu tuu vinatosha
 
Ushauri mzuri na ushauri wa aina hii umekuwa ukitolewa na watu wengi tu,sasa wasipoufanyika kazi,watakuja kujilaumu baadae.
 
Hizi ni hisia, ni fair kabisa Lissu kupewa bara na Maalim Seif kupewa Zenji
Huwezi kuamka asubuhi ukasema leo naungananisha chama hicho na kile. Kama itikadi zepisha, hata ufanye nini, muungano utakuwa wa kushinda uchaguzi lakini sio wa kuongoza serikali au nchi, maana sera nyingi na mitazamo isio endana. Na ndio maana duniani kote serikali za mseto ni ngumu kuziunda

Na ukiongeza na hisia za Chadema kwa kiongozi wa ACT, ndio kabisaa muungano unakuwa mgumu. Pitia yaliyotokea 2013.
 
URAIS
Urais kwa Upande wa bara mwachieni Tundu Lisu wa CHADEMA agombee na visiwani mwacheni Maalim Seif Agombee, najaribu kusema hivi ni kutokana na aina ya Wagombea wa CCM tulionao.Kwa bara Dr Magufuli kupambana na Lissu ni sahihi kabisa kulingana na siasa za hawa wawili za ukali na za kutoogopana. Ni wanasiasa wachache sana Tanzania wenye ujasiri wa kuikosoa serikali ya CCM hadharani bila kuogopa ukimtoa Tundu Lisu.
Upande wa Zanzibar hapa siwezi kuongea sana kwa sababu iko wazi kabisa kua Maalim Seif siasa za huko yeye anauzoefu nao na ndiyo nafasi yake.


Ningemuomba Mzee wangu Benard Membe atulie tu maana anayo nafasi kubwa sana ya kupata nafasi za juu serikalini upinazani ukishinda na hata kua PM, anayo nafasi hata ya Spika wa bunge la Jamhuri ikiwa mtakuwa na sayansi nzuri ya kugawana majimbo kiufundi kisha mkaachiana.
ACT bara msihangaike na Urais kwa sababu bado chama chenu hakijawa na ushawishi mkubwa sana kama ilivyo Zanzibar,bara Urais mking'ang'ania hamtashinda kuliko ambavyo mngetafuta wabunge wawasaidie kuongeza nguvu na nje ya bunge .Kwa bara CHADEMA ndio wenye Ushawishi mkubwa karibia 20 ya mikoa ya Tanzania bara ukiachia ile michache 5 ya Pwani ambayo ACT mtakua na nguvu kiasi.
Mwanahabari Huru jamani fanyieni kazi huu ushauri. Hili ni wazo zuri sana. Msigawane kura!
 
Back
Top Bottom