Baada ya vyombo vya habari kuwekewa pingamizi kuhusu habari za Lissu, sasa mmeelewa kwanini CHADEMA walizuiwa kuingia uwanjani msiba wa Mkapa?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Wengi walidhani kwamba Chadema walichelewa kuingia uwanjani kwenye msiba wa Mkapa na ndio maana walizuiwa kuingia. Hata account ya Sugu ilidafuliwa kupandikiza wazo hilo. Yote haya yalikuwa mpango maalum. Njama.

NIlieleza wazi kwamba habari kutoka jikoni zilieleza wazi kwamba kwa makusudi kabisa Chadema walipewa muda wa kuwasili uwanjani ambao wangekuta Raisi Magufuli ameisha ingia uwanjani, na hivyo wazuiwe kuingia kwa kisingizio cha kufuata protokali, kwamba wasingeingia baada ya Raisi Magufuli kuwa ameshaingia.

Lakini ukweli ni kwamba tukio hili la msiba lililofanyika siku moja tu baada ya Lissu kurejea nchini, lilihofiwa kwamba lingempaisha Lissu kwa free publicity. Hata kuna watu walihisi kwamba Lissu angeshangiliwa pale ambapo angekuwa akiishuka garini, na hili lilionekana kwamba ni jambo lisilokubalika kabisa, kwa kuzingatia uwepo wa vyombo vingi vya habari na watu waliokuwa wakiangalia luninga na kusikiliza redio juu ya tukio hili.

Hata ilihofiwa kwamba kesho yake Lissu angekuwa habari kuu kwa baadhi ya magazeti badala ya tukio la msiba, kwa vichwa kama "Umati wa waobolezaji waziziam kumshangilia Lissu akiingia uwanjani kwenye msiba wa Mkapa".

Hiki ndicho kilisababisha kwa makusudi kabisa viongozi wa Chadema wachezewe kwa kupewa muda ambao wangeambiwa wamechelewa na Raisi Magufuli ameshaingia uwanjani hivyo wasingeruhusiwa kuingia kama ujumbe.
 
Tatizo langu kubwa sio hao viongozi wa Cdm kuzuiwa, bali walifuata nini? Huyo marehemu alikuwa na chuki ya wazi dhidi ya cdm, na alikuwa anapanda kwenye majukwaa ya siasa hata baada ya kustaafu, akipandikiza chuki dhidi ya cdm. Ni lini huyo marehemu aliwahi kuhudhuria msiba wa kiongozi yoyote wa Cdm? Inatakiwa akifa mwanaccm hakuna mwanacdm kwenda, na kinyume chake. Hakuna haja yoyote ya kuonyeshana mshikamano wa kinafiki.
 
Tatizo langu kubwa sio hao viongozi wa Cdm kuzuiwa, bali walifuata nini? Huyo marehemu alikuwa na chuki ya wazi dhidi ya cdm, na alikuwa anapanda kwenye majukwaa ya siasa hata baada ya kustaafu, akipandikiza chuki dhidi ya cdm. Ni lini huyo marehemu aliwahi kuhudhuria msiba wa kiongozi yoyote wa Cdm? Inatakiwa akifa mwanaccm hakuna mwanacdm kwenda, na kinyume chake. Hakuna haja yoyote ya kuonyeshana mshikamano wa kinafiki.
MKuu, msiba ni msiba. Hata adui jirani akifa utaenda kwenye msiba. Kumbuka unaoenda kuwafariji ni wafiwa, sio maiti.

Unafikiri misiba ya vibaka watu hawaendi?
 
Labda suala la kujiuliza ni kwamba Chadema walienda msibani na usafiri ulioandaliwa na serikali? Angalia haya maelezo ya serikali; Kimsingi watu wangechukuliwa toka Karimjee kuanzia saa 12.30 hadi saa 1.30 asubuhi. Gari ya mwisho ya serikali kutoka Karimjee ingepeleka watu uwanjani saa moja na nusu asubuhi.

Sasa, ikiwa Chadema walienda uwanjani na gari ya serikali ambayo huenda hata haikuwa ya mwisho kuondoka Karimjeee, kwa nini wazuiwe? Au ndio tuseme walizuiwa kwa kuwa Raisi Magufuli "aliamua" kuwahi uwanjani kuliko ilivyotakiwa?

1597146552128.png
1597146603781.png
 
Yaani Chadema wote, viongozi na wanachama wao hakuna aliyesikia ratiba na utaratibu huu wa kuaga mwili. Ratiba iliyotoka siku moja kabla ilisikika kwa viongozi wa dini, vyama vingine vya siasa, wawakilishi wa kimataifa isipokuwa Chadema.
 
Yaani Chadema wote, viongozi na wanachama wao hakuna aliyesikia ratiba na utaratibu huu wa kuaga mwili. Ratiba iliyotoka siku moja kabla ilisikika kwa viongozi wa dini, vyama vingine vya siasa, wawakilishi wa kimataifa isipokuwa Chadema.

Walisikia Mkuu. Kumbuka kimsingi Chadema walichelewa, ila kuchelewa kwao kulikuwa "planned". Na hao wengine uliowataja hata kama "walichelewa" haikuwa tatizo, waliruhusiwa kuingia. Waliogomewa kuingia ni Chadema peke yao.

Jiulize, Chadema walienda uwanjani na gari maalum la serikali? Gari ya mwisho ilikuwa saa 1.30 asubuhi. Kwa hiyo kama ni "kuchelewa" wasingepewa gari kuanzia kule Karimjee.
 
Walisikia Mkuu. Kumbuka kimsingi Chadema walichelewa, ila kuchelewa kwao kulikuwa "planned". Na hao wengine uliowataja hata kama "walichelewa" haikuwa tatizo, waliruhusiwa kuingia. Waliogomewa kuingia ni Chadema peke yao.

Jiulize, Chadema walienda uwanjani na gari maalum la serikali? Gari ya mwisho ilikuwa saa 1.30 asubuhi. Kwa hiyo kama ni "kuchelewa" wasingepewa gari kuanzia kule Karimjee.
Kwa hiyo unafuta kauli yako hii? "NIlieleza wazi kwamba habari kutoka jikoni zilieleza wazi kwamba kwa makusudi kabisa Chadema walipewa muda wa kuwasili uwanjani ambao wangekuta Raisi Magufuli ameisha ingia uwanjani, na hivyo wazuiwe kuingia kwa kisingizio cha kufuata protokali, kwamba wasingeingia baada ya Raisi Magufuli kuwa ameshaingia."
 
Kwa hiyo unafuta kauli yako hii? "NIlieleza wazi kwamba habari kutoka jikoni zilieleza wazi kwamba kwa makusudi kabisa Chadema walipewa muda wa kuwasili uwanjani ambao wangekuta Raisi Magufuli ameisha ingia uwanjani, na hivyo wazuiwe kuingia kwa kisingizio cha kufuata protokali, kwamba wasingeingia baada ya Raisi Magufuli kuwa ameshaingia."
Hapana Mkuu, mpango huu ulifanywa mapema sana, yaliyobaki ilikuwa utekelezaji tu. Hata kama Chadema wangeenda pale saa 12.30 kuchukua gari ya kwanza bado "wangechelewa"

Mwili wa Mkapa ulifika saa ngapi uwanjani? Magufuli aliingia saa ngapi uwanjani? Chadema walifika Karimjee saa ngapi?

Ukinijibu haya maswali ninaweza kufuta kauli yangu
 
Hapana Mkuu, mpango huu ulifanywa mapema sana, yaliyobaki ilikuwa utekelezaji tu. Hata kama Chadema wangeenda pale saa 12.30 kuchukua gari ya kwanza bado "wangechelewa"

Mwili wa Mkapa ulifika saa ngapi uwanjani? Magufuli aliingia saa ngapi uwanjani? Chadema walifika Karimjee saa ngapi?

Ukinijibu haya maswali ninaweza kufuta kauli yangu
Basi ya Viongozi wa vyama ndio iliyo mbeba Lipumba, Cheyo na wenzi wao, Viongozi wenu wangechelewaje? Aaaah nimeelewa sasa!!!! "Walichelewa" sababu ni mbinu "WALIYOPANGA"
 
Tatizo langu kubwa sio hao viongozi wa Cdm kuzuiwa, bali walifuata nini? Huyo marehemu alikuwa na chuki ya wazi dhidi ya cdm, na alikuwa anapanda kwenye majukwaa ya siasa hata baada ya kustaafu, akipandikiza chuki dhidi ya cdm. Ni lini huyo marehemu aliwahi kuhudhuria msiba wa kiongozi yoyote wa Cdm? Inatakiwa akifa mwanaccm hakuna mwanacdm kwenda, na kinyume chake. Hakuna haja yoyote ya kuonyeshana mshikamano wa kinafiki.
Mkuu tindo you're bold than this bwana!

Ukishapewa cheo cha Maiti/marehemu/mfu huwa tunasahau mapungufu yote aliyokuwa nayo mtu huyo aliyefikwa na mauti, na kuvishwa "Ubinadamu"!

Na hiki ndicho kilipaswa ukiandike au ukae kimya!

Maana hata kuandika kwa chuki namna gani, marehemu hana nafasi yakusikiliza grudges zako kwake.

Tusamehe. Aliteleza kama mwanadamu. Tumpe nafasi aipumzishe nafsi yake
 
Basi ya Viongozi wa vyama ndio iliyo mbeba Lipumba, Cheyo na wenzi wao, Viongozi wenu wangechelewaje? Aaaah nimeelewa sasa!!!! "Walichelewa" sababu ni mbinu "WALIYOPANGA"
Swali nzuri sana! Labda walijichelewesha baada ya kufika uwanjani ili wawalaumu CCM

Pia labda viongozi wengine wa vyama walichelewa lakini wao wakaruhusiwa kuingia isipokuwa Chadema!
 
Mkuu tindo you're bold than this bwana!

Ukishapewa cheo cha Maiti/marehemu/mfu huwa tunasahau mapungufu yote aliyokuwa nayo mtu huyo aliyefikwa na mauti, na kuvishwa "Ubinadamu"!

Na hiki ndicho kilipaswa ukiandike au ukae kimya!

Maana hata kuandika kwa chuki namna gani, marehemu hana nafasi yakusikiliza grudges zako kwake.

Tusamehe. Aliteleza kama mwanadamu. Tumpe nafasi aipumzishe nafsi yake

Huo muda wa kufumbia macho watu waliokuwa wanapandikiza chuki kwenye jamii ndio umechangia wengine kuendelea kuwa waovu. Sisi wengine hatuna muda wa kunenepeshea ng'ombe mnadani boss. Ulikuwa mtu mwema tunakusifu ukiwa hai au umekufa, ulikuwa baradhuli tunakupa kubwa yako uwe hai au mfu, ili iwe fundisho kwa wengine fullstop.
 
Mkuu tindo you're bold than this bwana!

Ukishapewa cheo cha Maiti/marehemu/mfu huwa tunasahau mapungufu yote aliyokuwa nayo mtu huyo aliyefikwa na mauti, na kuvishwa "Ubinadamu"!

Na hiki ndicho kilipaswa ukiandike au ukae kimya!

Maana hata kuandika kwa chuki namna gani, marehemu hana nafasi yakusikiliza grudges zako kwake.

Tusamehe. Aliteleza kama mwanadamu. Tumpe nafasi aipumzishe nafsi yake
Kama ambavyo hakutupumzisha sisi wakati wa uhai wake hatuna budi kuendelea kuchokonoa maiti yake kwa kukumbushia Masaibu aliyotufanyia.
 
Mwanadamu utahangaika weee ila mpango wa Mungu huwa HAUKWAMI - hili nina uhakika nao kwa 100%.
 
Uongo uongo uongo kila kitu mnasingizia CCM nadhani hamko tayari kuchukua nchi.....wananchi wa kawaida wanajua kabisa chadema mlijichelewesha leo hii mnaanza kubadili maada mnasingizia ccm ? .Hapan hapana....huo ni uongo...ungeeni mingine lakini sio hili.
 
Synthesizer ningekuelewa kama ungesema walizuiwa kuingia kwenye basi liliobeba viongozi wengine wa vyama vya siasa kwa madai kwamba wamechelewa.
KUna Mkuu mmoja hapo juu amesema walifika uwanjani na basi lilelile lililobeba viongozi wa vyama vingine. Sasa hapo ndio mkoroganyo hata zaidi.
 
Uongo uongo uongo kila kitu mnasingizia CCM nadhani hamko tayari kuchukua nchi.....wananchi wa kawaida wanajua kabisa chadema mlijichelewesha leo hii mnaanza kubadili maada mnasingizia ccm ? .Hapan hapana....huo ni uongo...ungeeni mingine lakini sio hili.
Huyo "kila mtu" anaejua, amejuaje, alifuatana na Chadema? Unaona jinsi na wewe pia unaamini kwamba kila kinachosemwa dhidi ya Chadema ni kweli, hata wanaposingiziwa uongo, uongo, uongo!
 
Back
Top Bottom