Acha mambo ya kipuuzi, mambo afenye mkoloni bado tunayashikia bango kwamba ni ya ukweli wakati muungano tulionao sisi hatuutaki sababu umejaa mapungufu kibao. Mambo ya mjerumani na muarabu hayatuhusu, wote walititawala kimabavu na kufanya makubaliono wao wenyewe bila kuwahusisha wenyeji. Mambo ya kipuuzi kabisa
Mkuu hili jina lako Kakumamoto , ni mtihani na changamoto kweli kweli kwa baadhi yetu kulitamka!. Sisi wengine ni dhaifu!, uki imagine tuu, ka... kadogo!, ka moto!, lazima katakuwa ni ka..mu kweli kweli!, sasa sisi wenye udhaifu wa hisia za karibu, tunaanza kupata taabu na kuteseka!.
K
 
Leo nimekutana na clip ya Chars Hilary akiongea akitanabaisha kuwa kuna hekta elf 6 wilayani Bagamoyo ni mali ya serikali ya Zanzibar na mtu kutoka bara haruhusiwi kufanya shughuli za aina yoyote ndani ya ardhi hiyo kwani sio mali ya serikali ya Tanzania bara.

Jambo hili limenisikitisha sana and sijajua inakuwaje wazanzibari wawe na ardhi yao Tanganyika wakati mtanganyika ukifika Zanzibar ni sawa umeenda Kenya tu.

======
Msemaji wa Serikali ya Zanzibari, Charles Hillary amesema Shamba la Zaba lililoko Makurunge wilayani Bagamoyo ni mali ya Serikali ya Zanzibar hakuna mtu anayeruhusiwa kufanya shughuli yoyote eneo hilo.

Msemaji amesema Zanzibar imemiliki eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 6000 tangu mwaka 1977. Na amesema yoyete atakayeuziwa eneo katika ardhi hiyo hatalipwa fidia.

Pia soma: Zanzibar ndani ya Tanganyika ilianzia huku na 4,000 Coast villagers face land loss to investor
zamu yao sasaivi. kuna siku mtakuja mtembee kwa mguu hadi kisiwa ndui.
 
Tanzania ni nchi moja ya JMT, ambapo Zanzibar ni sehemu ya JMT, SMZ na Mzanzibari yoyote yuko huru kumiliki Ardhi huku kwasababu kila Mzanzibari ni Mtanzania, ana haki zote za Utanzania ikiwemo kumiliki Ardh...
KWA HERUFI KUBWA.

ENEO LA PWA NI YA KUANZIA TANGA HADI MTWARA PAMOJA KILOMETA MIA MOJA KUTOKA UFUKWENI HADI RUFIJI, KILWA, MAFIA, LILIKUWA MALI YA ZANZIBAR MPAKA MWAKA 1900 WAINGEREZA WALIPOKUJA KUITWAA NA KUIINGIZA KATIKA BRITISH PROTECTORATE
 
KWA HERUFI KUBWA.
ENEO LA PWA NI YA KUANZIA TANGA HADI MTWARA PAMOJA KILOMETA MIA MOJA KUTOKA UFUKWENI HADI RUFIJI, KILWA, MAFIA, LILIKUWA MALI YA ZANZIBAR MPAKA MWAKA 1900 WAINGEREZA WALIPOKUJA KUITWAA NA KUIINGIZA KATIKA BRITISH PROTECTORATE
Si kweli ni kilomita 100!, ni 10 miles za coastal stripe, na lilinunuliwa na Wajerumani na Waingereza mwaka 1890 kupitia mkataba wa Hellingoland au The Zanzibar Treaty na sio 1900!.
P
 
Tanzania ni nchi moja ya JMT, ambapo Zanzibar ni sehemu ya JMT, SMZ na Mzanzibari yoyote yuko huru kumiliki Ardhi huku kwasababu kila Mzanzibari ni Mtanzania, ana haki zote za Utanzania ikiwemo kumiliki Ardhi...
Kwa maelezo yako ndugu Mayalla, una maanisha Mkataba wa "The Zanzibar Treaty" ndo uliowapa Zanzibar haki ya Kumiliki eneo Tanganyika? Makubaliano ni ili walindwe na ndicho ambacho Tanganyika inafanya na si kumilikishwa eneo, kama ingalikuwa hivyo basi Zanzibar wangepaswa kuwa na eneo na Kenya pia kwa sababu pwani ya Kenya kama ilivyokua kwa pwani ya Tanganyika ni miongoni mwa maeneo yaliyokua chini ya sultani kabla ya Mkataba Huo kusainiwa.
 
Kwa maelezo yako ndugu Mayalla, una maanisha Mkataba wa "The Zanzibar Treaty" ndo uliowapa Zanzibar haki ya Kumiliki eneo Tanganyika?
Hapana!. Zanzibar ilipewa eneo la maili 10 za ukanda Pwani ya Africa Mashariki, na ule mkutano wa Berlin wa mwaka 1884, ulioitishwa na Von Bismarck.

The Zanzibar Treaty of 1890, ndio ulilirudisha eneo hilo Tanganyika.

Hii issues ya sasa ya Ranchi ya Makurunge, ni eneo linalomilikiwa na Zanzibar kwa umiliki tuu wa Ardhi ndani ya Tanzania bara, na sio sehemu ya Zanzibar ndani ya JMT.
Makubaliano ni ili walindwe na ndicho ambacho Tanganyika inafanya na si kumilikishwa eneo,
Ni kweli makubaliano ya Ujerumani na baadae Uingereza ni kumlinda Sultan. Baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Sultan mpinduliwa alikimbilia Uingereza na kuomba msaada kuja kusaidiwa, Uingereza ikakubali, ikatuma manowari za kijeshi kuja kuikomboa Zanzibar, by the time manowari za Uingereza zimefika Mombasa, huku nyuma tukaungana kukawa hakuna tena nchi ya Zanzibar, iliyopo ni JMT, hivyo safari Uingereza ya kuigomboa Zanzibar, ikaishia Mombasa!. Tanzania ndio mlinzi wa Zanzibar!.
kama ingalikuwa hivyo basi Zanzibar wangepaswa kuwa na eneo na Kenya pia kwa sababu pwani ya Kenya kama ilivyokua kwa pwani ya Tanganyika ni miongoni mwa maeneo yaliyokua chini ya sultani kabla ya Mkataba Huo kusainiwa.
Sio hivyo.
P.
 
Back
Top Bottom