Charles Hilary afafanua sehemu ya ardhi ya Bagamoyo kumilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu Zanzibar na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Charles Hilary amefafanua suala la eneo lililopo Makurunge Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kumilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Amesema “Eneo linaitwa Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA), marehemu Rais Julius Nyerere alilikabidhi kwa Rais wa Pili wa Zanzibar, Abood Jumbe, lilikuwa likitumika kuwanenepesha ng’ombe kabla ya kusafirishwa kwenda Zanzibar.

“Kulikuwa na Meli inaitwa Jitihada iliyotumika kuwasafirisha ng’ombe, baadaye mradi huo ulififia na hakukuwa na ng’ombe wanaosafirishwa, eneo likabaki tu kwa muda mrefu.

“Watu wengi wameona liko tupu wakanza kuvamia, kuna watu walianza kuuziwa na wengine wakawa wanaambiwa jenga haraka.”

Alipoulizwa kuusu Hati
“Kuhusu nyaraka zikiwemo Hati zinafanyiwa kazi kwa sasa.”

"Tulipoona uvamizi unaendelea ndipo tukatoa taarifa, eneo hilo lina ukubwa wa Hekari 6,000, kabla ilikuwa zaidi ya 17,000, likapunguzwa kwa makubaliano ya Zanzibar na hao waliogaiwa.

“Sehemu ya eneo hilo pia linaingia shamba la miwa la Bakhresa, kwa sasa Serikali inaangalia na muda mfupi ujao tutajua kitakachofanyika pale.”
IMG-20230606-WA0219.jpg
Chanzo: PowerBreakfast (Clouds FM)
 
Hajafafanua na wala hajatoa maelezo ya kutosha. Kalikimbia swali kwa kusema "kwa sasa tusiongelee hilo". Kuna red flags nyingi sana kwenye hili suala.

Kwa mujibu wa maelezo yake, eneo la RAZABA huko Makurunge lilikua na ukubwa wa hekari 17,000. Mpaka leo hii kasema lina hekari 6,000 tu. Nani anaweza kuachia zaidi ya nusu ya mali yake kirahisi hivyo?

Masoud alipouliza kuhusu vielelezo vya umiliki na kama huenda hayati Mwl. Nyerere alimkabidhi mzee Jumbe eneo hilo walitumie kwa muda tu na sio kulimiliki moja kwa moja, akalikwepa swali.

Dada yangu ni mmoja kati ya wahanga wa eneo hili la Makurunge, inauma sana.
 
Angalizo tu; wachangiaji baadhi wajue hilo eneo limetolewa tangu enzi za Mwalimu. Wasije kufikiria ni awamu ya sita. Maana kuna wavivu wa kusoma history ya nchi ila wepesi kujadili history ya nchi wasiyoijua.🙏🙏🙏
Hati zinashughulikiwa saiv means wanataka kurasimisha now, na kama limepungua kutoka ha 17000 to ha 6000 inamaanisha umiliki wao ulikoma.
 
Anawaambia hataki kuongelea hati, anataka story.
Hati ndio zinashughulikiwa saiv, maanake ndio wanakabidhiwa rasmi.
Huyu ni mzazibar lazima atetee Zanzibar.
Hilary, ambaye pia aliasisi kipindi cha Charanga Time kilichomzidishia umaarufu akiwa Radio One Stereo, alizaliwa Zanzibar miaka 56 iliyopita eneo la Jang’ombe. Aliwahi kunusurika kuuawa kwa risasi mwaka 1964, siku moja baada ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyoundoa utawala wa Sultan na kuiweka Serikali ya Watu wa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom