Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Ndugu zangu majira ya jana 31th May 2023 Ikulu ya Zanzibar kupitia msemaji wake ilitoa taarifa kwa umma kwamba inamiliki shamba la hekta elfu 6 huko Wilaya ya Bagamoyo upande wa Tanzania Bara. Kwamba ardhi hiyo ni mali ya serikali ya Zanzibar kwa ajili ya wazanzibar hivyo ni marufuku mtu yoyote kutoka Tanzania Bara kutumia eneo hilo hata kama anatoka hapohapo Bagamoyo.
Baada ya kuona, kusikiliza na kusoma taarifa hiyo nilipigwa na butwaa. Nilijiuliza kwamba hili jambo linawezekanaje? Kwani kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar Ibara ya 1 inasema; ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง ๐ฃ๐ ๐๐๐๐ ๐๐ข๐๐๐ฎ๐ค ๐๐ฃ๐๐ค ๐ก๐ ๐ข๐๐ฅ๐๐ ๐ ๐ฎ๐๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐ฃ๐๐ค ๐ก๐ค๐ฉ๐ ๐ก๐ ๐๐๐จ๐๐ฌ๐ ๐ซ๐ฎ๐ ๐๐ฃ๐๐ช๐๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐ข๐๐ ๐ฅ๐๐ข๐ค๐๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐จ๐๐ฌ๐ ๐ซ๐๐๐ค๐๐ค ๐ซ๐๐ก๐๐ซ๐ฎ๐ค๐๐ฏ๐ช๐ฃ๐๐ช๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐๐๐ง๐ ๐ฎ๐๐ ๐ ๐๐ข๐๐๐ฎ๐ค ๐ ๐๐๐ก๐ ๐ฎ๐ ๐๐ช๐ช๐ฃ๐๐๐ฃ๐ค ๐ฌ๐ ๐๐๐ฃ๐๐๐ฃ๐ฎ๐๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง ๐๐ ๐๐๐ฉ๐ฌ๐ ๐ ๐๐ข๐๐ช๐ง๐ ๐ฎ๐ ๐๐๐ฉ๐ช ๐ฌ๐ ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง.
Kwamba kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar eneo la Bagamoyo ambalo liko Tanzania Bara si sehemu ya Zanzibar. Hivyo basi sisi watu wa Tanzania Bara au Tanganyika ni vema tukapewa ufafanuzi inakuwaje Zanzibar ikamiliki ardhi ya Bara Tanganyika? Mipaka ya Zanzibar inajulikana na uzuri umeainishwa katika katiba ya Zanzibar yenyewe hivyo ni vema tukaambiwa uhalali wa Zanzibar kumiliki eneo hilo. Kama walinunua tuwekwe wazi na kama walihongwa pia tuwekwe wazi.
Kama hatutawekwa wazi basi huu muungano hatutafika nao mbali maana haiwezekani ardhi ya Tanganyika inatumiwa na watanganyika na Wazanzibar lakini ardhi ya Zanzibar inatumika kwa wazanzibar pekee huku Watanganyika au watu wa Bara wakinyimwa fursa ya kumiliki ardhi Zanzibar.
Ni wakati wa sisi wazalendo wa Tanganyika kwenda mahakamani kuhoji uhalali wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuchukua na kumiliki ardhi ya Tanzania bara kinyume na katiba ya Zanzibar yenyewe. Tunahitaji ushauri wa mawakili kwenye jambo hili na pia tunahitaji ufadhili kama inawezekana kufungua kesi. Hujuma za namna hii dhidi ya Tanganyika hazipaswi kukaliwa kimya maana haiwezekani wananchi wa Bagamoyo Tanganyika au Bara wakanyang'anywa ardhi na kupewa wazanzibar wakati huko Zanzibar hakuna wananchi wanaonyang'anywa ardhi na kupewa watu wa bara. Tukikaa kimya kuna siku Loliondo na Ngorongoro huko wanakoondolewa Maasai kwa mtutu wa Bunduki tutaambiwa ni mali ya Zanzibar.
Mwisho, kero za muungano mwarobaini wake ni rasimu ya Warioba ya serikali tatu. Ni vema tutakapoanza mchakato wa Katiba mpya msingi wetu uwe Rasimu ya Warioba ambayo ni mkusanyiko wa maoni ya wananchi Zanzibar na Tanganyika. Tofauti na hapo hatuwezi kuendelea kuwa na muungano huu ambao umejaa malalamiko kutoka pande zote.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Baada ya kuona, kusikiliza na kusoma taarifa hiyo nilipigwa na butwaa. Nilijiuliza kwamba hili jambo linawezekanaje? Kwani kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar Ibara ya 1 inasema; ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง ๐ฃ๐ ๐๐๐๐ ๐๐ข๐๐๐ฎ๐ค ๐๐ฃ๐๐ค ๐ก๐ ๐ข๐๐ฅ๐๐ ๐ ๐ฎ๐๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐ฃ๐๐ค ๐ก๐ค๐ฉ๐ ๐ก๐ ๐๐๐จ๐๐ฌ๐ ๐ซ๐ฎ๐ ๐๐ฃ๐๐ช๐๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐ข๐๐ ๐ฅ๐๐ข๐ค๐๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐จ๐๐ฌ๐ ๐ซ๐๐๐ค๐๐ค ๐ซ๐๐ก๐๐ซ๐ฎ๐ค๐๐ฏ๐ช๐ฃ๐๐ช๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐๐๐ง๐ ๐ฎ๐๐ ๐ ๐๐ข๐๐๐ฎ๐ค ๐ ๐๐๐ก๐ ๐ฎ๐ ๐๐ช๐ช๐ฃ๐๐๐ฃ๐ค ๐ฌ๐ ๐๐๐ฃ๐๐๐ฃ๐ฎ๐๐ ๐ ๐ฃ๐ ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง ๐๐ ๐๐๐ฉ๐ฌ๐ ๐ ๐๐ข๐๐ช๐ง๐ ๐ฎ๐ ๐๐๐ฉ๐ช ๐ฌ๐ ๐๐๐ฃ๐ฏ๐๐๐๐ง.
Kwamba kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar eneo la Bagamoyo ambalo liko Tanzania Bara si sehemu ya Zanzibar. Hivyo basi sisi watu wa Tanzania Bara au Tanganyika ni vema tukapewa ufafanuzi inakuwaje Zanzibar ikamiliki ardhi ya Bara Tanganyika? Mipaka ya Zanzibar inajulikana na uzuri umeainishwa katika katiba ya Zanzibar yenyewe hivyo ni vema tukaambiwa uhalali wa Zanzibar kumiliki eneo hilo. Kama walinunua tuwekwe wazi na kama walihongwa pia tuwekwe wazi.
Kama hatutawekwa wazi basi huu muungano hatutafika nao mbali maana haiwezekani ardhi ya Tanganyika inatumiwa na watanganyika na Wazanzibar lakini ardhi ya Zanzibar inatumika kwa wazanzibar pekee huku Watanganyika au watu wa Bara wakinyimwa fursa ya kumiliki ardhi Zanzibar.
Ni wakati wa sisi wazalendo wa Tanganyika kwenda mahakamani kuhoji uhalali wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuchukua na kumiliki ardhi ya Tanzania bara kinyume na katiba ya Zanzibar yenyewe. Tunahitaji ushauri wa mawakili kwenye jambo hili na pia tunahitaji ufadhili kama inawezekana kufungua kesi. Hujuma za namna hii dhidi ya Tanganyika hazipaswi kukaliwa kimya maana haiwezekani wananchi wa Bagamoyo Tanganyika au Bara wakanyang'anywa ardhi na kupewa wazanzibar wakati huko Zanzibar hakuna wananchi wanaonyang'anywa ardhi na kupewa watu wa bara. Tukikaa kimya kuna siku Loliondo na Ngorongoro huko wanakoondolewa Maasai kwa mtutu wa Bunduki tutaambiwa ni mali ya Zanzibar.
Mwisho, kero za muungano mwarobaini wake ni rasimu ya Warioba ya serikali tatu. Ni vema tutakapoanza mchakato wa Katiba mpya msingi wetu uwe Rasimu ya Warioba ambayo ni mkusanyiko wa maoni ya wananchi Zanzibar na Tanganyika. Tofauti na hapo hatuwezi kuendelea kuwa na muungano huu ambao umejaa malalamiko kutoka pande zote.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.