Getang'wan
JF-Expert Member
- Apr 9, 2015
- 3,075
- 3,413
Chakaza, shida yangu hadi kusema ni pandikizi, ni jinsi mambo ya zamani kumhusu hasa ya vitalu na nyara wakati akiwa Waziri MNRT. Kwa zile tuhuma ambazo magazeti ya kiuchunguzi yaliandika, asingekuwa mtu wao, wangekwisha kula nyama.Mkuu Nyalandu sio pandikizi. Isipokuwa sio mgombea sahihi kwa sasa.
Watawala wa kiimla na wababe wanatakiwa kukutana na watu kama Lissu ambaye amesema ukiiba kura hakuna cha kusema 'tunamuachia Mungu'
Sasa tutarajie makubwa kuibuka juu yake. Labda huko ccm kila mtu hadi Baba yao nafsi ziwasute maana rushwa na janjajanja ndio uti wa mgongo wa chama hicho. Vinginevyo, tutarajie mambo ya ajabu na ya aibu ndani ya chama chao. Umesikiliza clip ya Mary Mwanjelwa?