Kwanini CHADEMA haijawahi KURUDIA mgombea Urais?

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,103
22,551
Salaam, Shalom!!

Tukiwa msibani, tuendelee kupiga stori kidogo!!

Chama Cha DEMOKRASIA na Maendeleo CHADEMA, kilianzishwa May 1992 na Ndugu Mtei aliyewahi kuwa Governor wa Benki kuu ya Tanzania.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, CDM haikusimamisha kabisa mgombea Urais, Nia ilikuwa ni kusoma mchezo wa siasa za Nchi hii, na kuunga mkono chama kilichokuwa na nguvu Kwa wakati huo.

Mwaka 2005, CDM, ilisimamisha mgombea Urais Kwa mara ya kwanza, Mgombea Urais huyo wa wakati huo aliitwa Ndugu Freeman Aikael Mbowe. Baada ya Uchaguzi huo, chama kikaanza kuenea Kwa Kasi, hii ni baada ya Aliyekuwa mgombea Urais wa chama hicho, kuamua kuongeza juhudi ya kulijenga chama.

Mwaka 2010, chama hiki, kiliamua kuja na mgombea Urais mwingine tena, time hii, alikuja ndugu Dr Wilbroad Slaa. Chama kikaendelea kupata uungwaji mkono zaidi.

Mwaka 2015, Dr Slaa alitamani sana kugombea tena akiamini ana nguvu na umaarufu wa kutosha kushinda uchaguzi, lakini kama kawaida ya Chama hiki, kikamramba chenga ya MWILI na kumleta mgombea mpya tena, Time hii, ilimchukua Mzee Lowassa Kutoka timu pinzani Kwa Imani kuwa ingizo Hilo, litaleta tija, na Kweli, tuliiona mambo yalibadilika.

Mwaka 2020, Chama kikatuletea mgombea mpya tena, mgombea Machachari, Ndugu Tundu Antipas Lissu, inasemekana, pasingelikuwa na changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi Ule, chama kingepiga hatua kubwa zaidi.

Kwa trend hii, CDM imeonyesha DEMOKRASIA ya hali ya juu, maana Kila baada ya miaka mitano, imebadili mgombea tofauti na chama Dola, CCM, wao Kila baada ya miaka 10 ndo hubadili mgombea Urais,labda itokee ameitwa mbele za HAKI!!

Kuelekea 2025, CDM itaendeleza Utaratibu huu wa kuja na mgombea mpya, au itaangalia kati ya wagombea Bora waliopita na kutuletea mojawapo?

Kwanini CDM haikuwa ikirudia wagombea Urais kama CCCM
na CUF ya Lipumba?


Karibuni 🙏
 
CCM ingeiga utamaduni wa CDM, kubadili mgombea Kila baada ya miaka 5, maana wananchi wameanza kuchoshwa na mgombea huyo huyo miaka 10.

Cc: Lucas mwashambwa
Watanzania hakuna popote pale wamewahi kusema kuwa wanachoshwa na viongozi wa CCM kukaa madarakani kwa miaka kumi. Bali huwa tunashuhudia wananchi wakitamani katiba ibadilishwe ili aliyepo madarakani aongezewe muda wa kuongoza zaidi ya ile kumi iliyopo kikatiba.

Mfano kwa sasa watu wengi sana wanatani katiba ibadilishwe ili Rais samia aendelee kuongoza Taifa letu hata baada ya 2030
 
Maoni yangu ni kuwa, CDM, isirudie tena, kuazima mgombea Toka chama Dola!!

Kufanya hivi, ni kuzima ndoto za Vijana waliopikwa vyema kuchukua Nchi.
 
Watanzania hakuna popote pale wamewahi kusema kuwa wanachoshwa na viongozi wa CCM kukaa madarakani kwa miaka kumi. Bali huwa tunashuhudia wananchi wakitamani katiba ibadilishwe ili aliyepo madarakani aongezewe muda wa kuongoza zaidi ya ile kumi iliyopo kikatiba.

Mfano kwa sasa watu wengi sana wanatani katiba ibadilishwe ili Rais samia aendelee kuongoza Taifa letu hata baada ya 2030
Huku mtaani, wananchi wanasema, miaka mitatu ya huyu, ni kama 10 hivi!!

Mitano inatosha, kama Kweli ni waumini wa DEMOKRASIA kama CHADEMA.
 
Salaam, Shalom!!

Tukiwa msibani, tuendelee kupiga stori kidogo!!

Chama Cha DEMOKRASIA na Maendeleo CHADEMA, kilianzishwa May 1992 na Ndugu Mtei aliyewahi kuwa Governor wa Benki kuu ya Tanzania.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, CDM haikusimamisha kabisa mgombea Urais, Nia ilikuwa ni kusoma mchezo wa siasa za Nchi hii, na kuunga mkono chama kilichokuwa na nguvu Kwa wakati huo.

Mwaka 2005, CDM, ilisimamisha mgombea Urais Kwa mara ya kwanza, Mgombea Urais huyo wa wakati huo aliitwa Ndugu Freeman Aikael Mbowe. Baada ya Uchaguzi huo, chama kikaanza kuenea Kwa Kasi, hii ni baada ya Aliyekuwa mgombea Urais wa chama hicho, kuamua kuongeza juhudi ya kulijenga chama.

Mwaka 2010, chama hiki, kiliamua kuja na mgombea Urais mwingine tena, time hii, alikuja ndugu Dr Wilbroad Slaa. Chama kikaendelea kupata uungwaji mkono zaidi.

Mwaka 2015, Dr Slaa alitamani sana kugombea tena akiamini ana nguvu na umaarufu wa kutosha kushinda uchaguzi, lakini kama kawaida ya Chama hiki, kikamramba chenga ya MWILI na kumleta mgombea mpya tena, Time hii, ilimchukua Mzee Lowassa Kutoka timu pinzani Kwa Imani kuwa ingizo Hilo, litaleta tija, na Kweli, tuliiona mambo yalibadilika.

Mwaka 2020, Chama kikatuletea mgombea mpya tena, mgombea Machachari, Ndugu Tundu Antipas Lissu, inasemekana, pasingelikuwa na changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi Ule, chama kingepiga hatua kubwa zaidi.

Kwa trend hii, CDM imeonyesha DEMOKRASIA ya hali ya juu, maana Kila baada ya miaka mitano, imebadili mgombea tofauti na chama Dola, CCM, wao Kila baada ya miaka 10 ndo hubadili mgombea Urais,labda itokee ameitwa mbele za HAKI!!

Kuelekea 2025, CDM itaendeleza Utaratibu huu wa kuja na mgombea mpya, au itaangalia kati ya wagombea Bora waliopita na kutuletea mojawapo?

Kwanini CDM haikuwa ikirudia wagombea Urais kama CUF ya Lipumba?


Karibuni 🙏
Sasa nayo ni sifa!
 
Wanasema wamechoshwa na uchafuzi wanaofanyiwa, hivyo hawatashiriki chafuzi zijazo.
Hujawaelewa,

Wamesema watahakikisha TUME HURU ya UCHAGUZI inapatikana kabla ya kuingia uchaguzi wowote!!
 
Ndo mkubali, CDM imewaacha mbali kidemokrasia.

Wao, Kila baada ya miaka 5 wanatuletea mgombea mpya na makaratasi yake.
Chadema haijawahi Kuwa na mgombea uRais bwashee 😄

Hao uliowataja wote ni CCM isipokuwa Tundu Lisu ni NCCR Mageuzi

Chadema iliasisiwa kama Club ya Mabwanyenye na siasa zao zilipangwa kuishia bungeni ambapo Mabwanyenye Wangekuwa wanaweka CHAWA wao

Na hata ukiangalia Wabunge wote wa Chadema huwa wanawekwa tu ndio yule Shujaa Magufuli 2020 naye akajiwekea wa Kwake wale 19 na Chadema hawajawahi kuwashtaki mahakamani 😀
 
Back
Top Bottom