mjingamimi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 46,337
- 57,160
Sawa twende kwenye uzao na tarehe ya kuzaliwa yesu 25 mwezi wa 12 je ni sahihi?
Wacha kujitoa ufahamu sema ukweli kuzaliwa kwa Isa hakukuwa kwa kawaida soma hapa.
19:19 - (Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika
19:20 - Akasema: Nitampataje mwana hali mwanaadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?
19:21 - (Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.
19:22 - Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali.
[emoji3516]maria anachukua mimba take hapo hapo
19:23 - Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!
[emoji3516]anasikia uchungu
19:24 - Pakatangazwa kutoka chini yake: Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji!
19:25 - Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu.
19:26 - Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.
19:27 - Akenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!
[emoji3516]maria kesha jifungua isa.
19:28 - Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.
[emoji3516]dada wa Haruni anaulizwa
19:29 - Akawaashiria (mtoto). Wakasema: Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi
[emoji3516]ndugu wanashangaa mtoto mchanga ataongea vipi ?
19:30 - (Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii.
[emoji3516]Kichanga isa kinaongea