Kijana swali langu jepesi sana na liko wazi. Nimeomba nipewe ushahidi ya kuwa Biblia ilikuwepo kipindi cha Mtume wetu, iwe kama kitabu pweke au vingi, ukisoma Biblia yenu ambayo tamko hilo limekuwa maalumu kwa kitabu chenu ni kuwa halina hata kitabu kimoja cha asili kama kilivyo kuanzia Taurati, Zaburi mpaka Injilo ya nabii Issa.
Qur'aan ilikusanywa na kuwekwa katika nakala kama ilivyo, tofauti na vitabu vyenu vyote mmekuja kukusanya masalia na uchafu mwingi ambao manabii hawakufundisha mafundisho hayo kama vile utatu mtakatifu, uungu wa nabii Issa (Yesu) na mfano wa hayo.
Bado una deni toka kwangu kwa yale uliyo yasema huko juu kwamba Uislamu umeanzishwa na mapadri au ukatoliki, nasubiri ushahidi wa hili, kadhalika uthibitisho ya kuwa kipindi cha Mtume wetu Muhammad ilikuwepo Biblia.
Shukrani.