Ajira ya mtoto wa Mkapa yazua utata
na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
WAKATI taasisi za dola zikiwa zimeshaanza kuifanyia uchunguzi Kampuni ya Tanpower Resources inayohusishwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, utata umeibuka kuhusu ajira ya mtoto wake mmoja ambaye ameajiriwa katika ofisi moja nyeti serikalini.
Utata huo ambao tayari umeanza kuwatia wasiwasi watendaji, unatokana na ukweli kwamba, mtoto huyo ambaye naye ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni hiyo, hivi karibuni aliajiriwa katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Maofisa wa juu wa serikali waliozungumza na Tanzania Daima kwa sharti la kutotajwa majina yao, wanasema kwamba, mtoto huyo wa Mkapa aitwaye, Nicholaus Merinyo (39), Januari mwaka huu aliajiriwa kama mwanasheria wa serikali.
Uchunguzi wa Tanzania Daima, umedhihirisha kuwa kijana huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria, aliajiriwa Januari mwaka huu na tayari ameshapangiwa kituo cha kazi kwenye Ofisi ya Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Kanda ya Dar es Salaam.
Ofisa mmoja wa juu serikalini alilieleza gazeti hili kwamba, tayari baadhi ya watendaji ambao ndio waliopewa dhamana ya kufanya uchunguzi dhidi ya kampuni hiyo ya Tanpower inayolalamikiwa kumilikishwa isivyo halali mgodi wa makaa ya mawe ya Kiwira uliopo mkoani Mbeya, wameielezea hatua hiyo ya kumuajiri Nicholaus kuwa inayolenga kuingilia uchunguzi huo.
Mbali ya Nicholaus, wanahisa wengine wa Tanpower Resources, Anna Mkapa ambaye ni mke wa rais huyo mstaafu, aliyekuwa waziri katika serikali ya Mkapa, Daniel Yona, Joseph Mbuna, ambaye ni mkwewe Mkapa na Evans Mapundi.
Kampuni ya TanPower Resources inayomiliki asilimia 85 ya hisa katika Kampuni ya Kiwira Coal and Power Limited (KCML) imekuwa ikituhumiwa kwa muda sasa, kwa kununua mgodi huo uliokuwa ukimilikiwa na serikali kwa bei ya sh milioni 700 katika mazingira ya kutia shaka.
Baadhi ya wataalamu wa masuala ya ubinafsishaji na uthamanishaji wanasema kwamba, bei halisi ya mgodi huo ambao umeme wake unatarajiwa kusaidia taifa kukabiliana na tatizo sugu la kukatikakatika kwa umeme ni shilingi bilioni nne na si sh milioni 700.
Ofisa mmoja wa juu katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) aliliambia gazeti hili kwamba, uchunguzi wa kina dhidi ya kampuni hiyo inayuhusishwa na Mkapa, uliidhinishwa kuanza mwishoni mwa mwaka jana.
Tunakuhakikishia vyombo vya dola ikiwemo ofisi yetu vinaendelea kuchunguza mkataba huo na uchunguzi unafanyika kwa siri na tulianza kazi hiyo mwishoni mwa mwaka jana, alisema ofisa huyo huku akiionyesha Tanzania Daima baadhi ya nakala zinazohusiana na uchunguzi huo.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, ajira ya Nicholas katika ofisi ambayo tayari inamchunguza mwajiriwa ni jambo lisilofungamana na kanuni za utawala bora, kwa vile unavunja kanuni inayopinga mgongano wa masilahi.
Tanzania Daima ilipowasiliana na DPP, Eliezer Feleshi, kwa njia ya simu kuhusu tuhuma hizo, alimtaka mwandishi kuwasiliana naye atakapokuwa amerejea ofisini kutoka nje ya nchi alikokuwa amekwenda kwa shughuli za kikazi.
Hata hivyo mwanasheria mwingine wa serikali alilieleza Tanzania Daima kwamba, ajira hiyo ya Nicholaus inaweza kwa namna moja au nyingine kuingilia uchunguzi ambao tayari umeanza.
Hakuna sababu ya wananchi kuamini kuwa uchunguzi unaofanywa dhidi ya TanPower Resources utafanywa kwa umakini na haki kwa kuwa tayari suala la kulinda watoto wa wakubwa linaweza kupewa kipaumbele, alisema wakili mmoja wa serikali ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.
Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria, Katiba na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Edmund Sengondo Mvungi, alipohojiwa kuhusu ajira hiyo, alisema kuwa ajira ya umma inatakiwa ifungamane na katiba na sheria za nchi.
Si tu kwamba ni kinyume cha sheria kuajiri mtu ambaye ajira yake italeta mgongano wa kimasilahi lakini nafasi ya wakili wa serikali inampa mwajiriwa fursa ya kutekeleza mamlaka ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye kwa mujibu wa Ibara ya 59 (3) ya Katiba ni mshauri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano juu ya mambo ya sheria. Tukiamua kuajiri hovyo hovyo tutakuwa tunajenga misingi ya ufisadi ndani ya serikali, alisema Dk. Mvungi.
Suala hilo linakuja wakati kukiwa na taarifa zinazowatuhumu Mkapa na Yona ambao walikuwa viongozi wa juu serikalini kujiuzia mradi huo wa Kiwira wakati ukiwa mali ya umma chini ya Shirika la Taifa na Maendeleo (NDC) katika mazingira yanayotia shaka.
Taarifa zilizopata kuandikwa na gazeti moja la kila siku (siyo Tanzania Daima) mwishoni mwa mwezi uliopita, zilikariri nyaraka ambazo zilikuwa zikionyesha kuwa Mkapa na Yona walisajili kampuni hiyo Desemba 29, 2004, mwaka mmoja tu kabla rais huyo mstaafu hajamaliza kipindi chake cha pili na cha mwisho cha uongozi na kisha Machi mwaka 2005 kampuni hiyo ikanunua mgodi huo wa makaa ya mawe wa Kiwira.
Mgodi huo ulioko mkoani Mbeya hivi sasa unakamilisha mradi wenye thamani ya dola za Marekani milioni 27.8 (takriban bilioni 340) wa kuzalisha umeme utakaokuwa ukiuzwa Shirika la Taifa la Ugavi wa Umeme (Tanesco).
Kikubwa ambacho kimekuwa kikizusha maswali kuhusu hilo ni ukweli kwamba, kampuni hiyo ya TanPower iliyokuwa imesajiliwa katika kipindi kisichozidi miezi mitatu tu, tena ikiwa na wanahisa wazito ndiyo iliyoshinda zabuni wa ununuzi wa mgodi huo, kwa bei ambayo imeacha maswali mengi.
Nyaraka zaidi zinaonyesha kwamba mkakati wa kupata mradi huo zilianzishwa na Yona ambaye Machi 24, aliandika barua wakati huo akiwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Evans Mapundi aliyekuja kuwa mkurugenzi katika kampuni hiyo ya TanPower Resources (T) Ltd.
Katika barua yake hiyo iliyoandikwa kwa Kiingereza Yona alisema; I am glad to inform you that the government has agreed to go into joint venture partnership with TanPower Resources (T) Ltd in managing and operating Kiwira Coal Mines Ltd, as outlined in your writen proposal. Tafsiri yake: Nina furaha kukuarifu kwamba Serikali imekubali kuwa na ubia na TanPower Resources (T) Ltd. Katika kumeneji na kuendesha kampuni ya Mgodi wa Kiwira.
Katika barua hiyo, Yona alisema serikali imeteua timu ya kufanya majadiliano na TanPower Resources jinsi ya kuendesha mchakato huo kwa haraka kisheria na kitaalamu.
Katika barua yake hiyo, Yona anataja majina ya maofisa wa serikali walioteuliwa katika timu ya majadiliano kuwa ni: Ms A. Bukuku (Mwenyekiti), Kaimu Kamishna wa Madini, Omari Chambo, Mtaalamu wa Ushauri wa Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma- PSRC, J.J. Ngelime na wakili wa Serikali, B. Sahel.
Aidha, kumbukumbu zinaonyesha kuwa, nakala za barua hiyo zilisambazwa kwa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba, aliyekuwa Waziri wa Mipango na Ubinafsishaji, Dk. Abdallah Kigoda, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Andrew Chenge, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Marten Lumbanga, aliyekuwa Mwenyekiti wa PSRC, John Rubambe na aliyekuwa Mwenyekiti wa KCML, Rumisha Kimambo.
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 9 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
dhamana.na heshima kubwa waliokupa malofa na makabwela wa tz asante yao ni kuwaibia unafikili utaishi milele duniani yukowapi napolean utamjibu nini mungu wako kesho kwa dhuluma uliowatendea raia wako mkapa na mafisadi wenzako muogopeni mungu
na peter, arusha, - 16.04.08 @ 12:31 | #6848
Simtetei Nicholaus lakini mwaka jana nilifanya naye 'Internship' katika ofisi hiyo na kumuacha akiendelea kama mwanasheria mwanafunzi. Nilimuona kama mwanasheria mwenye uwezo wa kufnya kazi na kujituma. Kama taratibu za ajira zilifuatwa na watanzania wengine wakahojiwa tumpe nafasi, vinginevyo watoto wa wakubwa watakasa pa kufanya kazi wakati wana sifa walizosomea.
Kama upelelezi ulianza mwishoni mwa mwaka jana, Nicholaus nilimmkuta tangu mwanzoni mwa mwaka jana kwa ajili ya mazoezi kwa vitendo. Cha msingi apangiwe kazi ingine ambayo hatahusika na upelelezi wa kampuni hiyo maana ofisi ya mwanasheria ni kubwa na pana sana.
na T.MUZUMA, Narita-Japan, - 16.04.08 @ 12:51 | #6859
Mambo kama haya yanaonyesha jinsi viongozi wetu wanavyowadharau wananchi wa nchi hii tukufu. Haiwezekani wakacheza michezo ya kitoto namna hii kama kweli wanatuheshimu.
Mkapa uliyoyafanya yanatosha kuizika nchi hii, bado unaendelea na dharau ileile!! Mungu si Athmani, itafika siku zako arobaini zitatimia na tutakukaanga kwa mafuta yako mwenyewe. Wanaokulinda hawatadumu milele.
Hivi wewe unajisikiaje kama Mkristu unapolalamikiwa na taifa zima? Hivi hizo mali ulizojilimbikizia utazitumia wapi na kwa namna gani? Hivi una habari kwamba utakufa sawasawa na sisi unaotudhulumu? Hivi una habari nawe vilevile utazikwa kaburini na wala sio mbinguni au hata angani? Yaangalie sana maneno haya, ni madogo lakini makubwa.
Sala ya kila Mtanzania sasa hivi ni Mungu atusaidie tuweze kukuweka mbaroni na kukutaka ujibu kwetu sisi na kwa Mungu wako. Ikitokea ukafariki kabla ya kutimiza hili tutakuwa tumepata hasara isiyo kifani!!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu watokomeze mafisadi.
na Amk, Dar, - 16.04.08 @ 12:53 | #6860
unajua kuna mambo mengine mtu unaweza fanya ukamkufuru Mungu....kwa mfano, naomba tukiamka kesho viongozi wote wa CCM wafe...huu ni ushenzi,tena uliokithiri....hausemekeki!!
na mdau, tz, - 16.04.08 @ 13:05 | #6867
Hivi mtu kweli na akili zako unamtetea Nicholaus??Au ni wewe mwenyewe Nic unajisafisha....??At nifanya naye internship mwaka jana aibu tupu ina maana jamaa amemaliza bachelor yake mwaka jana,u see jinsi alivyotapeli kama baba yake fisadi mkubwa, MUDA SI MREFU TUTAANZA KUPIGA NAO KWA MAPANGA...TUMECHOKA NA KUNYONYWA NA VITA LAZIMA. YEYE NA BABA YAKE NA MAMA WOTE WEZI WAKUBWA HAWASTAILI KUISHI DUNIANI
na ATANASI MSAKI, dar, - 16.04.08 @ 13:11 | #6869
ndg yangu T.MUZUMA, Narita-Japan, - 16.04.08 @ 12:51 | #6859
usichokijua ni kwamba kwanini mkapa na kundi lake lilishiriki kwenye ubadhirifu mkubwa wa rasilimali za taifa hili(KIWIRA,ANABEN,EPA,UUZAJI WA NBC,BOTMIKATABA MIBOVU YA MADINI,NET GROUP SOLUTION etc)wanataka nico merinyo(ambaye naye ni mtuhumiwa kashfa ya kiwira)afanye kazi katika ofisi ya mwanasheria mkuu(kituo cha Ofisi ya Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Kanda ya Dar es Salaam)
huu ni mkakarti mahususi wa kuhakikisha kwamba ikitokea wakashitakiwa basi anakuwepo mtu pale wa kuvuruga ushahidi kwani katika hili hawa mabwana wenyewe wanajua kwamba hali si shwari na waliyoyafanya kwa taifa hili ni uovu mkubwa!
hivyo basi kijana huyu(nico merinyo) kuajiriwa katika
ofisi ambayo inamchunguza yeye na familia yake juu ya ufisadi ni mgongano wa maslahi wenye lengo la kuvuga upelelezi dhidi ya tuhuma zinazowakabili!
hivyo aondoke au aondolewe mara moja!
na jingo - 16.04.08 @ 13:13 | #6871
Tukuwaanbia Mkapa hana busara wala chochote zaidi ya kuendeshwa na mkewe mama mpenda pesa/ Sasa angalia kila uchafu yupo.
Ama kweli Nyerere alikula hasara kumbeba nuda asijue atawamaliza watu wake.
Mkapa,mkewe, mwanae, Sumaye, Yona na mafisadi wengine wanapaswa kuvamiwa na wananchi kama vibaka na kupewa displine
na Mpayukaji Msemahovyo, Siri, - 16.04.08 @ 13:16 | #6874
ndugu Mhariri, naoma nitumie nafasi hii kutoa pendekezo jingine. Nashauri pawepo mahali pengine ambapo tutakuwa tukitoa maoni yetu mengine, yasiyofungamana na habari hizi unazoziandaa.iwe kama vile maoni ya wasomaji kwenye magazeti
na David, Dar es Salaam, - 16.04.08 @ 13:19 | #6875
Haya sasa angalia,watu ni wale wale;kama si Mramba ni Yona ni Kigoda ni Chenge ni Karamagi ni Mkapa ni Lowasa ni Sumaye ni Balali na Maafisa wa Madini/Nishadi ambao,yumkini,hutumika ka chambo tu.Rada,ndege ya Rais,BoT/EPA,nk, majina hayo hayakosi,inakuwaje? Yaani Wa-Tz milioni 37 wanatapeliwa na kikundi cha watu wachache.Leo hii ktk Afrika Tz ndo inaongoza kupata misaada toka nchi zilizoendelea,Benki ya dunia imeifutia Tz madeni kibao,pia inazidiwa madini na A.Kusini na Kongo (Zaire) tu,ni pekee duniani kuzalisha Tanzanite,inachuana na A.Kusini kwa mbuga za wanyama duniani,ktk Afrika ni ya pili kwa mifugo mingi baada ya Ethiopia,nk,nk.Je,Mungu angetupa nini ili tumshukuru? Mh Kikwete ktk ziara zake Ulaya amewahi kuulizwa nini sababu ya umasikini wa Tz akawajibu kuwa hata yeye anashangaa na hajui.Kwa miaka mingi wa-Tz tunatafuta kiini cha umasikini wetu hatupati jibu.Ktk hatuba zake Mkapa alikuwa akitugombeza wananchi kuwa eti sisi ni wavivu,hatujitumi.Kumbe jibu ni hili 'tunaporwa na maafisa wa serikali'.
na Matiku, Dar,Tz, - 16.04.08 @ 13:32 | #6884