Serengeti fiesta 2014 special thread

Serengeti fiesta 2014 special thread

Sifa za ally kiba zitadumu kwa cku mbili au tatu maana hana kitu kinachomfanya tumsikie kila cku ila Dai utamskia tuu hata kwa kupitia Wema

kumbe anabebwa na wema sio mziki wake?!!
cheap publcity!!!
 
Fiesta fiesta fiesta fiesta kila mwaka mnaharibuu balaaaa hamjui kuchagua wasanii wa kimataifa kuja tanzania kuperform katika show za fiesta...jana ndo kimeonekana kuwa t.i hakuwa chaguo sahihi watu wamefurahi kumuona lkn jee mashabiki pale wengi walikuwa wa hip hop? T.i ni performer mzuri sana ila mashabiki wa tz hawakuwa wanampa mzuka aliokuwa anautegemea kutoka kwa fans.rapper kama huyu dont expect to return in tanzania for shows again coz anajua mistari ake mashabiki wa tz hawaiwezi na kuielewa ili kumpa mzux zaidi....xoxo next tym prime time promotion and clouds ent group fanyeni research kabla ya kuleta mtu(msanii) kuweni na r&d department kujua mashabiki wanataka wasanii wa aina ganiii....
 
Wabongo wanashabikia uhuni wa clouds, Clouds wanataka wasanii wawe cheap ili waweze kuwanyonya vizuri...washaona dogo anapaa hivyo anawapanda kichwani...kumbukeni zile saga za kugomea fiesta zao mikoani akitaka dau refu...
Wanajifanya kumpromote Kiba ili amzime Dai...Mungu ataendelea kumuweka juu kama alivyomuweka Jide...

Yuko wapi Q chillah? Yuko wapi Cowbama? Historia ikataka irudiwe kwa Jide, akagoma kuwa historia, Na Daimond hawezi kuwa historiaaa....

Kama anaubavu aanze life lake, clouds wanazingua

BTW hivi kule uingereza na ujerumani ni clouds pia???
 
Watu bwana et "kiba kawakodi watu wampigie shangwe na wamzomee Baba ubaya""😝😝😝😝😝😝😝😝

Hivi kiba anazo pesa za kuulipa ule umati uliokua unatoa shangwe?

👉👉kubalini tu Mgambo wenu kakalishwa Jana😜😜😜😜😜

TeamKiba4real😍😍😍😍😍😍

Na mshukuru
 
Nakumbuka miaka mitano iliyopita aliyekuwa
nguli wa filamu Nchini Tanzania marehemu
""Steven Kanumba"" alienda kwenye jumba la
Big Brother....
amini usiamini bila sababu yyte ya maana
watanzania ndo walikuwa wa kwanza kuanza
kumsema kuwa hajui kuvaa, nani alimchagua ,
hajui kiingereza mpaka kufikia kumuigiza!!!
Walisahau hata watu maruufu kama Messi na
wengine wengi hawajui kuongea kabisa lugha
hiyo..
Baada ya kifo chake watanzania hawahawa
wakaanza kusema alikuwa nguli
aliyetuwakilisha vizuri nje ya nchi na kulia
sana!!!kumbe wakati akiwa hai tulikuwa
tunamshusha chini..
Miaka mitano baadae Tanzania imempata mtu
anayeiwakilisha vizuri nje ya mipaka na
kuitangaza vizuri nchi yake..
Pasipokuwa na sababu za msingi (chuki binafsi
tu)anapangiwa njama za kuzomewa na
kuabishwa katika ardhi ya nchi yake ambayo
kwa namna moja au nyingine kuna watu
wameifahamu sababu yake!! Ukiuliza sababu za
wengi wao kumchukia ni mafanikio yake lakini
hata kama humpendi mtu hivi ndo hadi
umzomee kwa kiasi kile !!!
leo na kesho naye huyu akitoka utaskia
hawahawa waliokuwa wanamzomea wanaanza
kusema jamaa alikuwa anatuwakilisha vizuri
sana , ametutangaza sana kimataifa!! lakini
Watanzania wenzake ndio vinara wa
kumuangusha..
Si lazima kila mtu ampende Diamond ila
kutumia nguvu kubwa sana kumuangusha mtu
ni ishara ya uwoga na Roho ya kimaskini...
Nimeamini ""maisha bila unafki hayaendi""

👆👆njama😕😕😕??
Nani kamfanyia njama ww

Aujui kua kuna tofauti kubwa kati ya tandale na kko?

Mgambo Wa jiji kafulia Jana kwasabbu mnenguaji wake Madame ubaya akunengua
 
Dogo nilikuwa namkubali sana, lakini alinikera alipoanza kuwadharau waliomfikisha hapo alipo sasa, ajitathimin upya!
 
Wabongo wanashabikia uhuni wa clouds, Clouds wanataka wasanii wawe cheap ili waweze kuwanyonya vizuri...washaona dogo anapaa hivyo anawapanda kichwani...kumbukeni zile saga za kugomea fiesta zao mikoani akitaka dau refu...
Wanajifanya kumpromote Kiba ili amzime Dai...Mungu ataendelea kumuweka juu kama alivyomuweka Jide...

Yuko wapi Q chillah? Yuko wapi Cowbama? Historia ikataka irudiwe kwa Jide, akagoma kuwa historia, Na Daimond hawezi kuwa historiaaa....

Dangote hawezi kuwa historia hata wakiloga
 
Da wanajamvi huyu mdogo wetu amewafanya nini watanzania hasa vijana wenzake,naona ameingia kutumbuiza watu wanamzomea na kupiga kelele na kuita Kiba,Kiba,Kiba,japo alijaribu kupiga nyimbo aliemshirikisha Ney wa mitego ndo angalau kidogo watu walikua wakimshangilia Ney,sasa pana nini wanajamvi

Hatutaki dharau zake...kwani yeye ndo wakwanza kuwa juuu????anadharau utadhani ye hanyi..douchebag
 
Huu uhuni wa Kikwete kuingilia mambo ya kibiashara ya makampuni binafsi kwa sababu Kuna washkaji zake ndio yanasababisha watu wachukie utawala wake. This is pure business, subjectivity haikuwa na nafasi kabisa. Jamaa wanafanya huu uhuni kwa sababu za ushikaji na JK, siku JK anatoka Ikulu November 2015 hii redio itafungwa kabisa na kuchinjiwa baharini. Wameshindwa kupambana na himaya ya Mengi wanaonea wachanga, not fair bana hii radio ya wafu imewatenda wengi Sana. Tena saizi wanashirikiana na Shigongo kutaka hata kuvunja ndoa..

Hahahaha ndugu hawa jamaa bado wapo tena sana usifikiri jk anaweza kuondoka nao. Labda useme siku ccm ikitoka madarakani ndio wanaweza kuishiwa. Lakini bado naona hata ikija chadema wataendelea kutesa tena kwa sana tu kwani Mbowe ni mshkaji wao ndo usiseme kabisa. Wanampelekeaga dili nyingi sana kwenye ukumbi wake wa Billcanas. Na ukumbuke hata kuisha kwa bifu la Ruge na Sugu ushawishi mkubwa ulitoka kwa Mbowe ili kulinda masilahi ya ukumbi wa disco. Sasa we unaona kuna dalili za wao kutoka kwenye system? Labda kutoka kwao ni pale wananchi mtakapoamua kususa kusikiliza media zao au labda waje cuf. Ni ofisi gani,taasi au kampuni gani wasiojuana nayo hapa nchini? Labda nisijue usalama wa taifa tu. We ukisikia wanakwambia kamata fulsa twende zetu huwa unahisi wanamaanisha nini???

Ndug mjini hapa wanaishi wajanja wajanja kama wale na ndo wanakula good time.
 
kikwete akisema wamuache je??unajua kikwete ni nani kwenye jeshi wewe.unajuaje kama hajaomba ruksa??na unajua sheria ya nguo hizo kuvaliwa kwa matamasha?? nadhan hata wao watakua wanamaana hawawezi kuleta fiesta bila kibali kaka

Kumbe sare za jeshi zinaweza kuvaliwa kwa ruksa!
 
Mi kuna kauli moja huwa naipenda sana..."Binadamu ndivyo tulivyo,huwezi kua safi kwa kila mtu..."kuna muda ufike tuwe tunastick kwa kile kitu kimekufanya wewe umfahamu mtu mengine tupakule,kama unemjua mtu sababu ya muziki na unaupenda muziki wake basi habari na scandal zake zote zione na uzipuuzie tu.

Na kingine usanii ni mauzo.
 
Back
Top Bottom