Ramadhan Special Thread
Kama unafunga swaumu kwakuwa nyumbani wote wanafunga na inabidi tu ufunge,jua hujafunga kwa ajili ya Allah

Kama unafunga kwakuwa wafanyakazi wenzako wote wamefunga,basi jua hujafunga kwa ajili ya Allah

Kama unafunga swaumu kwakuwa wanafunzi wenzako wote wanafunga na huna namna unaogopa aibu wasikuone kobe,basi jua unafunga si kwa ajili ya Allah


Kagua nia yako na jiulize je nafunga kweli kwa ajili ya Allah?
 
عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضي الله عنه قَالَ:
« مَا رَأَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ ﷺ قَطُّ صَلَّى صَلَاةَ الْمَغْرِبِ حَتَّى يُفْطِرَ وَلَوْ عَلَى شَرْبَةٍ مِنْ مَاءٍ »
Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema:
Sikuwahi kumuona Mtume ﷺ, akiswali swala ya magharibi MPAKA AFUTURU, hata kama ni kwa funda la maji.

➡️ Sunna ni kufuturu KABLA YA KUSWALI Magharibi, hata kama ni tende chache au maji. kuchelewesha kufuturu bila sababu ni kinyume na mwenendo wa Mtume ﷺ.
➡️ Inatakiwa uanze kufuturu kabla ya swala kwa kumfuata Mtume ﷺ.
Mtume hakula chakula kikubwa kwanza, alianza kwa kitu kidogo, kisha akaswali.
➡️ Kuharakisha kufuturu ni katika alama za Ahlus-Sunna.

✍🏼 Abuu Maryam Kambi (Allah amuhifadhi).
whatsapp.com/channel/0029Vb…
( Si ruhusa kubadili chochote )
 
MUHAMMAD ALIKUWA ANAKULA VYAKULA MCHANA KWEUPE MFUNGO WA RAMADHANI , WEWE ENDELEA KUSHINDA NA NJAA


Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Abi A'ufa:

Tulikuwa pamoja na Mtume wa Allah safarini, na jua lilipopoa alimwambia mtu mmoja, “Shuka na unitayarishie kinywaji cha Shairi Yule mtu akasema: Ewe Mtume wa Allah bado mchana! Mtume wa Allah akasema tena mtume "Shuka na uandae kinywaji cha Shairi " Yule mtu akasema: Ewe Mtume wa Allah ! Je, utangoja mpaka jioni, kwa maana bado ni mchana? Mtume akasema tena, "Shuka na uandae kinywaji cha Shairi " Basi mara ya tatu yule mtu akashuka na kumwandalia kinywaji cha Shairi . Mtume wa Allah akakunywa hicho na akaashiria kwa mkono wake upande wa Mashariki, akasema: Unapouona usiku unaingia upande huu, basi mfungaji afungue saumu yake


حَدَّثَنَا عَلِيُّ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ، حَدَّثَنَا جَرِيرُ بْنُ عَبْدِ الْحَمِيدِ، عَنْ أَبِي إِسْحَاقَ الشَّيْبَانِيِّ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ أَبِي أَوْفَى، قَالَ كُنَّا فِي سَفَرٍ مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا غَرَبَتِ الشَّمْسُ قَالَ لِرَجُلٍ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ لِي ‏"‏‏.‏ قَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ لَوْ أَمْسَيْتَ‏.‏ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ ‏"‏‏.‏ قَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ لَوْ أَمْسَيْتَ إِنَّ عَلَيْكَ نَهَارًا‏.‏ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ ‏"‏‏.‏ فَنَزَلَ فَجَدَحَ لَهُ فِي الثَّالِثَةِ، فَشَرِبَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ثُمَّ أَوْمَأَ بِيَدِهِ إِلَى الْمَشْرِقِ فَقَالَ ‏"‏ إِذَا رَأَيْتُمُ اللَّيْلَ قَدْ أَقْبَلَ مِنْ هَا هُنَا فَقَدْ أَفْطَرَ الصَّائِمُ ‏"‏‏.‏

Grade Sahīh

Sahih al-Bukhari 5297. 7, Book 63, Hadith 218


Sahih Muslim 1101b kitabu 6, Hadith 2423
 
MUHAMMAD ALIKUWA ANAKULA VYAKULA MCHANA KWEUPE MFUNGO WA RAMADHANI , WEWE ENDELEA KUSHINDA NA NJAA


Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Abi A'ufa:

Tulikuwa pamoja na Mtume wa Allah safarini, na jua lilipopoa alimwambia mtu mmoja, “Shuka na unitayarishie kinywaji cha Shairi Yule mtu akasema: Ewe Mtume wa Allah bado mchana! Mtume wa Allah akasema tena mtume "Shuka na uandae kinywaji cha Shairi " Yule mtu akasema: Ewe Mtume wa Allah ! Je, utangoja mpaka jioni, kwa maana bado ni mchana? Mtume akasema tena, "Shuka na uandae kinywaji cha Shairi " Basi mara ya tatu yule mtu akashuka na kumwandalia kinywaji cha Shairi . Mtume wa Allah akakunywa hicho na akaashiria kwa mkono wake upande wa Mashariki, akasema: Unapouona usiku unaingia upande huu, basi mfungaji afungue saumu yake


حَدَّثَنَا عَلِيُّ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ، حَدَّثَنَا جَرِيرُ بْنُ عَبْدِ الْحَمِيدِ، عَنْ أَبِي إِسْحَاقَ الشَّيْبَانِيِّ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ أَبِي أَوْفَى، قَالَ كُنَّا فِي سَفَرٍ مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا غَرَبَتِ الشَّمْسُ قَالَ لِرَجُلٍ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ لِي ‏"‏‏.‏ قَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ لَوْ أَمْسَيْتَ‏.‏ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ ‏"‏‏.‏ قَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ لَوْ أَمْسَيْتَ إِنَّ عَلَيْكَ نَهَارًا‏.‏ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ انْزِلْ فَاجْدَحْ ‏"‏‏.‏ فَنَزَلَ فَجَدَحَ لَهُ فِي الثَّالِثَةِ، فَشَرِبَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ثُمَّ أَوْمَأَ بِيَدِهِ إِلَى الْمَشْرِقِ فَقَالَ ‏"‏ إِذَا رَأَيْتُمُ اللَّيْلَ قَدْ أَقْبَلَ مِنْ هَا هُنَا فَقَدْ أَفْطَرَ الصَّائِمُ ‏"‏‏.‏

Grade Sahīh

Sahih al-Bukhari 5297. 7, Book 63, Hadith 218


Sahih Muslim 1101b kitabu 6, Hadith 2423
Pole sana.

Kwa taarifa yako msafiri yeyote amepewa udhuru ya funga.

Hata wewe ukisafiri ni ruhusa kwako kutofunga.
 
Jamani tupo katka kukumbushan katk yale yaliyo mema na kukatazana katka yale yasiofaa pia usione aibu kuuliza chochote ambacho hukifaham wanaokijua watakufahamisha jaman hapa ktk swala pana mambo mengi sana ya kustaajabisha na ya kushangaza pia mtu ukiona swala yakushinda namanisha huiwez au hujui yanayotamkwa pindi mtu anapokuwa anaswali please jamn uliza au kam waon haya mfate mtu pm akufahamishe zaid Jamani kuhusu kutia udhu pia kwa baadhi ya waislam ni tatizo uliza sote tupo hap kwa ajil ya kujifunza ukion aibu kuuliz hap unawez kwenda pm ya yoyote na swala lako likawekwa mezan tukajadil MWENYEZI MUNGU NDO MUWEZA WA YOTE WABILLAH TAUFFIK ASALAM ALYKUM WARAHMA TULLAH WABARAKATUH
Naaam
 
Yaliyo Muhimu Kwa Ujumla Wa Kutekeleza ´Ibaadah Ya Swawm (Kufunga)


1. Niyyah.
Allaah (Subhanahu wa Ta’ala) Amesema:

ﻭَﻣَﺎ ﺃُﻣِﺮُﻭﺍ ﺇِﻟَّﺎ ﻟِﻴَﻌْﺒُﺪُﻭﺍ ﺍﻟﻠَّﻪَ ﻣُﺨْﻠِﺼِﻴﻦَ ﻟَﻪُ ﺍﻟﺪِّﻳﻦَ ﺣُﻨَﻔَﺎﺀ ﻭَﻳُﻘِﻴﻤُﻮﺍ ﺍﻟﺼَّﻠَﺎﺓَ ﻭَﻳُﺆْﺗُﻮﺍ ﺍﻟﺰَّﻛَﺎﺓَ ﻭَﺫَﻟِﻚَ ﺩِﻳﻦُ ﺍﻟْﻘَﻴِّﻤَﺔِ


“Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Allaah kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Swalah, na watoe Zakaah. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti.”
(Suuratul Bayyinah 98 : 05)


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) amesema:

’’Kila kitendo hulipwa (kutokana na) niyyah na kila mtu ni lili alilonuwiya.’’
Na niyyah mahala pake ni moyoni. Niyyah ya kufunga ni lazima iwe moyoni kila usiku kabla ya wakati wa Fajr kuingiya.
Hafsah (Radhiya Allaahu ´anha) amesema mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) amesema:

‘’Hana swawm asiyenuwia kufunga kabla ya fajr.’’

[Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh al-Jamiy´ as-Saghiyr, na.6238. Pia imerikodiwa na Abu Dawuud, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy].


2. Kujiepusha katika masiku ya kuamka na swawm na chochote chenye kubatilisha swawm yako (tangu wakati wa adhaana ya pili) na usiku mpaka kutakapopambauka (Jua kuchomoza).


Amesema Allaah (Subhanahu wa Ta’ala):

ﻭَﻛُﻠُﻮﺍْ ﻭَﺍﺷْﺮَﺑُﻮﺍْ ﺣَﺘَّﻰ ﻳَﺘَﺒَﻴَّﻦَ ﻟَﻜُﻢُ ﺍﻟْﺨَﻴْﻂُ ﺍﻷَﺑْﻴَﺾُ ﻣِﻦَ ﺍﻟْﺨَﻴْﻂِ ﺍﻷَﺳْﻮَﺩِ ﻣِﻦَ ﺍﻟْﻔَﺠْﺮِ ﺛُﻢَّ ﺃَﺗِﻤُّﻮﺍْ ﺍﻟﺼِّﻴَﺎﻡَ ﺇِﻟَﻰ ﺍﻟَّﻠﻴْﻞِ


“Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni swawm mpaka usiku.”
(Suuratul-Baqarah: 187).
🙏🏻🙏🏻🙏🏻
 
حكم دعاء القنوت في التراويح


HUKMU YA DUA YA QUNUUT NDANI YA SWALA YA TARAWEEH

📩 #السؤال :
Suali:

ما حكم قراءة دعاء القنوت في الوتر في ليالي رمضان؟ وهل يجوز تركه؟

Ni ipi hukmu ya kusoma Dua ya Qunuut ndani ya Swala ya Witri katika usiku wa Ramadhan? Na je Inajuzu kuiwacha?

📄 #الجواب :
Jawabu:
القنوت #سنة في الوتر ، وإذا تركه في بعض الأحيان فلا بأس.

Dua ya Qunuut ni Sunna katika Witri , na atakapoiwacha katika baadhi ya hali basi hakuna tabu.

📚 مجموع فتاوى ومقالات الشيخ ابن باز 30/32🎀
 
IMG-20260228-WA0002.jpg
 
Tawhid: Msingi wa Uhai wa Imani
Maana ya Tawhid

Tawhid ni kuamini na kuthibitisha kuwa Allah ni Mmoja, hana mshirika, hana mfano, hana anayefanana naye katika Uungu, Majina na Sifa Zake. Neno lenyewe linatokana na “wahhada” likimaanisha kuufanya mmoja.

Katika Qur’an Tukufu, Qur'an inasema:
“Sema: Yeye ni Allah Mmoja.” (Surah Al-Ikhlas 112:1)
Huu ndio moyo wa Uislamu. Bila Tawhid, ibada hugeuka kuwa kivuli kisicho na mwili.

Aina za Tawhid
Wanazuoni wameigawa Tawhid katika sehemu kuu tatu:
1. Tawhid ar-Rububiyyah
Kuamini kuwa Allah ndiye Muumba, Mlezi, Mpangaji wa kila kitu. Hakuna anayetoa uhai, riziki au mauti isipokuwa Yeye.
“Allah ni Muumba wa kila kitu.” (39:62)
Hapa moyo hutulia. Unapojua Mlezi ni Mmoja, hutaishi kwa hofu ya viumbe.

2. Tawhid al-Uluhiyyah
Kumpwekesha Allah katika ibada. Swala, dua, nadhiri, kuchinja, tawakkal, yote yaelekezwe Kwake pekee.
Hili ndilo lililokuwa kiini cha da‘wah ya Mitume wote akiwemo Muhammad ambaye aliwaita watu waseme:

“La ilaha illa Allah”
Kauli fupi, lakini ina uzito wa mbingu na ardhi.

3. Tawhid al-Asma wa Sifat
Kuamini Majina na Sifa za Allah kama zilivyokuja katika Qur’an na Sunnah, bila kupotosha, kufananisha au kupunguza.
Allah ni Ar-Rahman, Al-‘Alim, Al-Qadir. Sifa Zake ni kamilifu, si kama za viumbe.

Umuhimu wa Tawhid

Ni kusudio la kuumbwa kwa mwanadamu
“Sikuwaumba majini na wanadamu ila waniabudu.” (51:56)

Ni sharti la kukubaliwa kwa ibada
Ibada bila Tawhid ni kama mwili bila roho.
Ni sababu ya kuingia Peponi
Mtume alisema:
“Atakayekufa hali ya kuwa anajua kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah, ataingia Peponi.”
Hatari ya Kinyume cha Tawhid
Kinyume cha Tawhid ni shirki, kumshirikisha Allah. Hili ndilo dhambi kubwa zaidi.
“Hakika Allah hasamehe kushirikishwa...” (4:48)

Shirki ni kama tone la sumu katika maji safi. Linaweza kuharibu uzima wote wa imani.
Tawhid Katika Maisha ya Kila Siku
Tawhid si nadharia tu. Ni mwanga wa kila hatua:
Unapopatwa na shida, unamwomba Allah pekee.
Unapofanikiwa, unamshukuru Yeye pekee.
Unapohofia kesho, unamtegemea Yeye pekee.
Moyo wa mwenye Tawhid huwa huru. Hauinamii watu kwa kuogopa riziki wala sifa zao.

Hitimisho
Tawhid ni kama mzizi wa mti. Mizizi ikiwa imara, matawi hustawi na matunda huwa matamu. Bila mzizi, kila upepo huuangusha.
Tujiulize:
Je, ibada zetu zinamwelekea Allah peke Yake?
Je, tunamtegemea Yeye katika dhiki na raha?
Allah atujaalie tuwe miongoni mwa watu wa Tawhid ya kweli, wenye nyoyo safi na ibada zilizo na ikhlas.
 
Level ya Juu Kabisa ya Funga: Kuacha Matamanio na Kumkumbuka Allah kwa Moyo Wote

Funga si njaa tu. Si kiu tu. Si kuhesabu saa mpaka adhana ya Magharibi ipaze sauti. Funga ni safari ya ndani, safari ya kutoka tumbo kwenda moyoni, kutoka mazoea kwenda utambuzi, kutoka matamanio kwenda utumwa wa kweli kwa Allah.

Allah Anasema:
“Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa swaumu kama ilivyofaradhishwa kwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kuwa wachamungu.” (Al-Baqarah 2:183)

Lengo la funga si mateso, bali ni taqwa. Na taqwa ni hali ya moyo, si hali ya tumbo.

Funga ya Kawaida na Funga ya Kiwango cha Juu
Watu wengi hufunga kwa kuacha kula na kunywa. Hii ni ngazi ya kwanza. Ni muhimu, ni sahihi, ni faradhi. Lakini bado ni mwanzo tu.

Mtume ﷺ amesema:
“Mwenye kuacha kula na kunywa lakini hakuacha kusema uongo na kuutenda, basi Allah hana haja ya yeye kuacha chakula na kinywaji chake.” (Bukhari)

Hapa ndipo tunapoelewa:
Funga ya kweli si ya mdomo tu, bali ni ya moyo, macho, masikio, na nafsi nzima.
Level ya juu kabisa ya funga ni pale mtu anapofunga:

Macho yake dhidi ya haramu
Masikio yake dhidi ya batili
Ulimi wake dhidi ya maneno ya maumivu
Na zaidi ya yote…
Moyo wake dhidi ya matamanio yanayompeleka mbali na Allah

Kuacha Matamanio: Mapinduzi ya Ndani
Matamanio si chakula tu. Ni hasira, ni kiburi, ni riyaa, ni tamaa ya sifa, ni kutaka kuonekana.

Funga ya juu ni pale unapokuwa na uwezo wa kufanya dhambi… lakini unaamua kuacha kwa sababu Allah anakutazama.
Ni pale nafsi inaposema:
“Fanya.”
Na moyo unasema:
“Allah yupo.”
Hapo ndipo roho inaanza kuwa huru.

Kumkumbuka Allah kwa Moyo Wote
Dhikr si tasbih mikononi tu. Dhikr ya juu ni hali ya moyo ambayo inahisi uwepo wa Allah kila saa.

Mtume Muhammad ﷺ alikuwa akimkumbuka Allah katika hali zote. Ndiyo maana moyo wake haukuwa mateka wa dunia.
Muhammad alituonyesha kwamba ibada ya kweli ni ile inayogeuza moyo kuwa hai.
Mtu akifika hatua hii:
Chakula hakimtawali
Hasira haimtawali
Sifa za watu hazimtawali
Dunia haimtawali
Anakuwa mfungaji hata baada ya Ramadhani kuisha.

Funga Inayokupandisha Daraja
Wapo wanaofunga kwa tumbo.
Wapo wanaofunga kwa viungo.
Lakini wachache hufunga kwa moyo.

Na wale wanaofunga kwa moyo, huwa wanahisi ladha ya ibada ambayo haiandikwi kwa kalamu wala kupimwa kwa mizani ya dunia.
Wanapokuwa na njaa, wanahisi ukaribu na Allah.
Wanapokuwa na kiu, wanahisi rehema Zake.
Wanapopambana na nafsi, wanahisi ushindi wa ndani.
Hiyo ndiyo level ya juu kabisa ya funga.

Hitimisho
Funga ni shule.
Na somo lake kuu ni: kumdhibiti nafsi na kumuweka Allah mbele ya kila kitu.
Ukiacha chakula lakini hujaacha matamanio, bado uko njiani.

Lakini ukiacha matamanio na moyo wako ukajaa dhikr ya Allah, umefika kileleni.
Mwenyezi Mungu Atujaalie tufunge kwa miili yetu, kwa nafsi zetu, na zaidi kwa mioyo yetu.
 
Surah Ash-Shuraa (42:30):
“Na misiba inayokupateni ni kwa sababu ya yale iliyoyachuma mikono yenu, na (Allah) anasamehe mengi.”

Aya hii ni kama kioo cha moyo; inatuonesha sura zetu za ndani na wakati huo huo inatupaka dawa ya matumaini

1. Maana ya “kwa yale iliyoyachuma mikono yenu”
“Mikono” hapa si tu viungo vya mwili. Ni ishara ya matendo yote ya mwanadamu; mazuri na mabaya.
Aya inatukumbusha kuwa:
Baadhi ya misiba ni matokeo ya makosa yetu.
Dhambi zinaweza kuwa sababu ya mitihani.
Uzembe, dhulma, kiburi, au kupuuza maamrisho ya Allah vinaweza kuzaa matunda machungu.

Ni kama kupanda mbegu ya miiba halafu kushangaa kwanini miguu inaumizwa.
Lakini si kila msiba ni adhabu. Wakati mwingine ni:
Kuinua daraja
Kufuta madhambi
Jaribio la subira
Njia ya kumrudisha mja karibu na Mola wake

2. “Na anasamehe mengi”
Hii ndio sehemu inayobeba nuru
Allah anatuambia wazi kuwa:
Si kila kosa linafuatiwa na adhabu.
Dhambi nyingi zinasamehewa bila hata sisi kujua.
Rehema Yake ni pana kuliko makosa yetu.
Fikiria: kama kila kosa lingelipiwa papo hapo, nani angebaki?
Lakini Allah anaifunika dhambi, anachelewesha adhabu, anatoa fursa ya tawba.

3. Mafunzo muhimu kutoka aya hii
Kujitathmini – Kila unapopatwa na tatizo, jiulize: je kuna jambo nahitaji kurekebisha?
Kutokata tamaa – Rehema ya Allah ni kubwa kuliko kosa lako.
Kufanya tawba – Msiba unaweza kuwa mlango wa kurudi kwa Allah.
Kuwa na mizani sahihi – Usimhukumu kila mwenye matatizo kuwa anaadhibiwa; Allah ndiye Mjuzi wa hakika.

4. Mizani ya Kiimani
Muislamu anapoona neema → anamshukuru Allah.
Anapoona mtihani → anatafakari, anatubia, anasubiri.

Aya hii inatufundisha uwajibikaji na matumaini kwa wakati mmoja. Ni aya ya tahadhari, lakini pia ni aya ya rehema.
 
KUFIKIA KUMI LA KATI LA MWEZI WA RAMADHAN

🖇️العشر الأواسط من رمضان

Siku Kumi za Katikati za Ramadhani.

📌قَالَ العَلّامَة صَالِح الفَوْزَان حَفِظَهُ الله تعالى :

Amesema Mwanachuoni Swaleh Al-Fawzan (Allah Amhifadhi):

ﻓﻤﻦ ﻛﺎﻥ ﻗﺪ ﺃﺣﺴﻦَ ﻓﻴﻬﺎ ﻭﺣﻔِﻈَﻬَﺎ؛ ﻓﻌﻠﻴﻪ ﺑﺎﻟﺘﺰﻭّﺩِ ﻭﺍﻹﻛﻤﺎﻝِ ﻟﺒﻘﻴﺔ ﺍﻟﺸﻬﺮِ،

"Basi tuzihesabu nafsi zetu katika hizi (siku) kumi zilizopita; ni vipi tumezipitisha? Na je, tumezihifadhi kwa kumtii Allah (Aliyetukuka na Kushinda) na kufaidika nazo?
Yule ambaye amefanya wema ndani yake na akazihifadhi, basi na azidishe na akamilishe masiku yaliyobaki.

ﻭﻣﻦ ﻛﺎﻥ ﻣﻔﺮﻃًﺎ ﻓﻲ ﺍﻟﻌﺸﺮِ ﺍﻟﻤﺎﺿﻴﺔ ﻭﻣﺘﻜﺎﺳﻼً؛ً ﻓﻌﻠﻴﻪ ﺑﺎﻟﺘﻮﺑﺔ ﻭ ﺍﻻﺳﺘﺪﺭﺍﻙِ ﻟﻤﺎ ﺑﻘﻲَ ﻣﻦ ﻫﺬﺍ ﺍﻟﺸﻬﺮِ ﻗﺒﻞ ﺃﻥ ﻳﻔﻮﺕَ ﻛﻠُّﻪ ﻭﻟﻢ ﻳﺤﺼﻞ ﻋﻠﻰ ﺷﻲﺀ.

Na yule aliyekuwa mzembe katika masiku kumi yaliyopita na akawa mvivu, basi ni juu yake kutubu na kurekebisha yale yaliyobaki katika mwezi huu kabla hayajapita yote na akawa hajapata chochote."

(ﻣﺠﺎﻟﺲ ﺷﻬﺮ ﺭﻣﻀﺎﻥ ﺍﻟﻤﺒﺎﺭﻙ" صـ (46).⁩

Chanzo: Majalis Shahru Ramadan Al-Mubarak, ukurasa wa (46).

Tarjama Raudhwatu ssalafiyyah

Kwa faida mbalimbali ungana nasi katika channel zetu

WhatsApp link


Telegram link


WASAMBAZIE WENGINE KWA FAAIDAH

الدال على الخير كفاعله

نسأل الله أن ينفعنا وينفع جميع المسلمين.. آمين
 
Umuhimu wa Uchamungu (Taqwa) Katika Maisha ya Muislamu

Uchamungu ni taa ya moyo. Ni kama dira ya baharia katikati ya bahari yenye mawimbi makubwa. Bila dira, jahazi huzunguka tu. Bila uchamungu, moyo huzunguka katika matamanio.

Katika Uislamu, uchamungu (taqwa) ni hali ya kumcha Allah kwa kutekeleza amri Zake na kuacha makatazo Yake kwa ikhlas na utii.

Maana ya Uchamungu​

Allah Anasema katika Qur’an:
“Enyi mlioamini! Mcheni Allah kama inavyostahili kumcha, wala msife isipokuwa mmekuwa Waislamu.”
(Qur’an 3:102)

Hii inaonesha kuwa uchamungu si jambo la msimu. Ni safari ya maisha yote. Ni ulinzi wa nafsi dhidi ya maasi, na ni ngao dhidi ya ghadhabu ya Allah.

1. Uchamungu Humfanya Mja Awe Karibu na Allah
Allah Anasema:
“Hakika aliye mtukufu zaidi kwenu mbele ya Allah ni yule aliye mchamungu zaidi.”
(Qur’an 49:13)
Heshima ya kweli mbele ya Allah haipimwi kwa mali wala cheo. Inapimwa kwa uchamungu. Moyo uliosheheni taqwa ni kama bustani yenye harufu ya imani .

2. Uchamungu Huleta Njia ya Kutokea Katika Shida
Allah Anasema:
“Na anayemcha Allah, Atamfanyia njia ya kutokea. Na Atamruzuku kwa njia asizotarajia.”
(Qur’an 65:2-3)

Taqwa ni ufunguo wa milango iliyofungwa. Wakati wengine wanaona ukuta, mwenye uchamungu huona mlango mdogo unaofunguka taratibu.

3. Uchamungu Hupokea Matendo
Allah Anasema:
“Hakika Allah Anakubali (matendo) kutoka kwa wachamungu.”
(Qur’an 5:27)
Si kila tendo lina uzito mbele ya Allah. Uzito wake hupimwa kwa taqwa. Swala, swaumu, sadaka bila uchamungu ni kama mwili bila roho.

4. Uchamungu Huleta Amani ya Moyo
Mwenye uchamungu huishi kwa utulivu hata katika dhoruba. Anajua kuwa kila jambo ni kwa qadari ya Allah. Hilo humfanya awe na subira, shukrani, na matumaini.
Moyo wa mchamungu ni kama ardhi yenye rutuba. Hata mvua ya majaribu ikianguka, hutoa mimea ya imani.

5. Uchamungu Ni Njia ya Kuokoka Siku ya Mwisho
Katika Siku ya Qiyama, mali na watoto havitasaidia isipokuwa moyo uliosalimika. Moyo huo ni moyo wa taqwa.
Mtume Muhammad ﷺ alifundisha kuwa Allah haangalii sura wala mali zetu, bali huangalia nyoyo na matendo yetu. Hii inaonesha kuwa uchamungu ni siri ya mafanikio ya Akhera.

Uchamungu si maneno ya midomoni, bali ni mwanga wa ndani unaoonekana kwa matendo.
Ni kujenga ukuta kati yako na maasi.
Ni kumkumbuka Allah hata pale hakuna anayekuona.
Ni kuchagua halali hata kama haramu inaonekana rahisi.
Mwenye taqwa anatembea duniani kwa tahadhari, lakini moyo wake uko juu, ukitamani radhi za Allah.
Allah Atujaalie tuwe miongoni mwa wachamungu. Ameen.
 
Imepokewa kutoka kwa Ka'b ibn Ujrah (na pia kwa riwaya ya Anas bin Malik) kwamba:
Mtume wa Allah ﷺ, Muhammad, alipanda juu ya mimbari akasema:
“Aamiin, Aamiin, Aamiin.”

Wakasema Maswahaba:
“Ewe Mtume wa Allah, tumekusikia ukisema Aamiin mara tatu?”

Akasema:
“Hakika Jibril alinijia akasema:
‘Ameangamia mtu ambaye Ramadhani imeingia kwake kisha akatoka bila kusamehewa.’
Nikasema: Aamiin.

Akasema: ‘Ameangamia mtu ambaye amewakuta wazazi wake au mmoja wao katika uzee lakini hawakumuingiza Peponi.’
Nikasema: Aamiin.

Akasema: ‘Ameangamia mtu ambaye umetajwa kwake lakini hakukuswalia.’
Nikasema: Aamiin.”

Hadith hii imepokewa na Imam Ahmad ibn Hanbal na wengine, na imehesabiwa kuwa sahihi na wanazuoni kama Al-Albani.

Hii hadith ni kama kioo kinachotuonesha maeneo matatu ya hatari:
Ramadhani bila msamaha
Kuwakosa wazazi bila kuwahudumia
Kumsahau Mtume kwa kutokuswali juu yake

Ni onyo, lakini pia ni mwaliko. Mlango bado uko wazi. Ramadhani bado ni chemchemi ya rehema.
 
JE FUNGA INASWIHI IKIWA MTU HASWALI?

Uzuri ni kwamba dini ya kiislamu imekamilika kila kitu kiko wazi katika quran na sunnah

Na Mtume( s.w.a ) alisema hivyo ametuacha mahali peupe kabisa, ambapo haina haja ya kutafuta tochi kuanza kumulika jambo fulan kuhusu dini yetu tukaacha quran na sunnah

Jambo la kwanza tutakaloulizwa siku ya kiyama ni swala!!
hivyo kama swala haipo sawa basi amali zako zingine zinazofata zaweza zikawa povu lilopotea tujitahidi na kusimamisha swala ndugu zangu!!

Mtume (s.a.w ) anasema ''kinachotenganisha uislamu na kufru ni kuacha sala''

swala ndiyo nguzo kubwa ya dini hayo mengine yanafuatia, tofauti yetu sisi na wao ni swala hayo mengine hata wao wanafanya kufunga kuhiji n.k

KUFUNGA NA KUACHA SWALA NI DALILI YA UNAFKI SABABU UNACHAGUA KIPI UFANYE KIPI UACHE

Mara ya kwanza Mtume (s.a.w)anapewa swala alipewa vipindi 50
Na falsafa iliyopo hapo ni ili kutuonyesha, Allah(s.w.) ametuleta duniani si kwa jambo lingine lolote isipokuwa IBADA
IBADA ndiyo njia pekee alotuwekea Allah(s.w) kufikia mafanikio ustawi na furaha

Mtume(saw)alikuwa akiswali mpaka miguu inavimba mimi na wewe kujihalalishia kufunga na tunaacha sala ni kujidanganya

(Q 2.283) ''enyi mlioamini mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kuwa wachamungu''
''ILI MUWE WACHAMUNGU'' sasa mwisho wa ramadhani jifanyie mwenyewe self assessment je ramadhani imenisaidia kuwa Mchamungu? nimeacha uwongo? nimeacha wizi? Nimeacha zinaa? Nimeacha pombe? Nimeacha riba?

Japokuwa kuna changamoto tele kutokana na mazingira ya makazini kwetu, vyuoni kwetu majumbani kwetu, ndugu zetu marafiki zetu n.k ila wakati sasa wa kupambana kuisimamisha haki, usiyumbishwe na chochote UISLAMU NDIYO DINI YA HAKI FUATA MAFUNDISHO YAKE NA MAAMRISHO YAKE ILI UPATE MWISHO MWEMA HAPA DUNIANI. HUJUI KIFO CHAKO KIPO LEO KESHO AU YAWEZEKANA RAMADHANI IJAYO IKAKUKUTA KABURINI.

Imani haiombwi imani inatafutwa kisha uhifadhiwa moyoni na huimarika kwa kufanya vitendo vizuri vya kumridhisha Allah (s.w)

Kama mimi na wewe tulikuwa hatusimamishi swala ndio mda muafaka wa kuamka usiku kuomba ''taubatan nasuha '' il mungu atusamehe na kisha tuweke nia ya kuendelea na yale mazuri yote ya kumpendeza Allah(s.w) ambayo tunayaanza mda huu kuelekea Ramadhan, na tuanze leo ndugu yangu wala tusisubiri kesho,wakati ni sasa
Mtume(s.w) anatushauri tuwe na pupa/haraka katika kuyaendea mambo ya kheri na subra katika mitihani/kuyaendea maovu

Na unapoamua kuyafanya ya Mungu (s.w) tegemea mitihan yakila aina ila cha muhimu uwe na msimamo KWANI NI BORA YAHARIBIKE YAKO ILA USIYAHARIBU(AMRI) YA MUNGU(S.W) NA IKIWA HUTAYAHARIBU YA MUNGU(S.W) JUA YA KWAMBA YAKWAKO PIA KAMWE HAYATAHARIBIKA

''Kumbusha hakika ukumbusho huwafaa wenye kuamini'' (51:5)
Wabilah tawfiq .
 
Hizi ni baadhi ya hadith za Mtume Muhammad ﷺ kuhusu umuhimu wa swaumu:

1️⃣ Swaumu ni Ngao
Mtume ﷺ amesema:
"الصِّيَامُ جُنَّةٌ"
“Swaumu ni ngao.”
(Imepokewa na Sahih al-Bukhari na Sahih Muslim)

Maana yake: Swaumu ni kinga dhidi ya maasi na pia kinga dhidi ya Moto wa Jahannam. Ni kama ngao ya askari vitani, lakini vita hii ni dhidi ya nafsi na matamanio.

2️⃣ Swaumu ni kwa ajili ya Allah, na Yeye ndiye hulipa
Mtume ﷺ amesema kuwa Allah amesema:
"كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ لَهُ إِلَّا الصِّيَامَ، فَإِنَّهُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ"
“Kila amali ya mwana wa Adam ni yake isipokuwa swaumu; hakika swaumu ni Yangu, na Mimi ndiye nitakayeilipa.”
(Imepokewa na Sahih al-Bukhari na Sahih Muslim)


Hii ni heshima ya kipekee. Swaumu imepewa hadhi ya siri kati ya mja na Mola wake.

3️⃣ Furaha Mbili za Mwenye Kufunga
Mtume ﷺ amesema:
“Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha anapofungua na furaha atakapokutana na Mola wake.”
(Sahih al-Bukhari)

Furaha ya kwanza ni ya dunia, ya pili ni ya Akhera.

4️⃣ Mlango wa Rayyan
Mtume ﷺ amesema:
“Hakika Peponi kuna mlango unaoitwa Ar-Rayyan. Wataingia humo watu wa swaumu siku ya Kiyama…”
(Sahih al-Bukhari na Sahih Muslim)

Ni mlango maalum kwa waliovumilia kiu na njaa kwa ajili ya Allah.

5️⃣ Swaumu ya Ramadhani na Msamaha
Mtume ﷺ amesema:
“Atakayefunga Ramadhani kwa imani na kwa kutarajia malipo atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
(Sahih al-Bukhari na Sahih Muslim)

Ramadhani ni kama bahari ya rehema, anayezama humo kwa imani hutoka akiwa safi.

Swaumu si njaa tu, ni safari. Ni shule ya subira, mafunzo ya ikhlasi, na daraja la kumkaribia Allah. Mwili unapopungua nguvu, roho hupata nguvu mpya.
 
Back
Top Bottom