🌸Lainisheni nyoyo zenu kwa aina mbalimbali za matendo mema ili kuukaribisha Ramadhān.
Na yaliyo na manufaa zaidi kwenu ni yale yanayofanana na matendo yanayotakiwa ndani yake;
kama vile:
kufunga,kuswali,
kusoma Qur’ani, na kutoa sadaka.

Kwa kuzoea matendo haya, mtu huimarishwa katika kuyatekeleza, na hufanywa mepesi juu ya nafsi pale unapowadia wakati huo uliobarikiwa.


 
Ndugu yangu nashukuru kwa nasaha zako, huwa tunakutana kwenye mijadala na wasio kuwa waislamu

Nafurahi mnapoweka michango yenu na ninatamani mjitokeze wengi zaidi tukumbushane kama hivi mambo ya dini yetu tukufu
 
Daud At-ttai ni miongoni mwa wanawazuoni wa kiislamu. Alikuwa ni mwanafunzi wa Imam Abu Hanifa.

Moja katika darsa za Imam Abu Hanifa, Imam kwa ghafla alisimama katikati ya kufundisha na akasema "hii ni elimu (kwa maana anayoifundisha), lakini itekelezwe wapi?"

Katika muktadha huu Imam Abu Hanifa alikuwa anakusudia tofauti kati ya maarifa ama elimu mtu anayosoma na maisha halisi.

Maarifa peke yake (kama kusoma hadithi, fiqhi, tafsiri ya Qur'an) hayatoshi. Yanapaswa kutumika katika adabu, ibada, mahusiano na hukumu za maisha kila siku (na huko ndiko kutosha kwake).

Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasalllam alileta mfano wa maisha ya huruma, usawa, uvumilivu, na heshima kwa kila mwanadamu, bila kujali dini, rangi, hali ya kijamii au kabila.

Je, hii elimu aliyotupatia Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasalllam tunaishia kuisoma ama kuitekeleza kwa kuishi nayo? "Hii ni elimu (maarifa), lakini itekelezwe wapi?" Ndicho Imam Abu Hanifa alichokusudia.

Daud At-ttai alijifanyia tathmini mwenyewe na kujikagua na alipogundua mapungufu yake ni yapi, alijikita kwa Allah subhanahu wataala kwa kuyaishi yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasalllam kwa kuyaishi.

Hivyo ndugu zangu katika imani, wakati huu tunaouendea mwezi mtukufu wa Ramadhani, miongoni mwa vitu tutakavyoomba tusisahau kuomba kwa Allah azitakase nafsi zetu: Ewe Mola wetu! Tunakuomba utujaalie mahabba yako, na utujaalie tuwapende unaowapenda, na utujaalie mahabba ya matendo yanayotukurubisha kwako. Utukufu ni wako. Hakuna Mungu isipokuwa wewe. Utusamehe madhambi yetu. Hakika sisi ni miongoni mwa waja wako tunaokukosea.
 
Waalaykum Salaam Warahmatullahi Wabarakaatuh.

Kwenye kufunga kitu cha kwanza na muhimu ni nia.
 
“Allah haikalifishi nafsi isipokuwa kwa uwezo wake…”
(Qur’an 2:286)

Aya hii iko mwisho wa Suratul Baqarah, kama kifungo cha rehema baada ya sheria, maagizo, na mafunzo mazito. Ni kama Allah anasema:

“Nilichowaamrisha, ninafahamu mnaweza kukitekeleza.”

Maana ya jumla

Allah (ﷻ) hamuweki mtu jukumu linalomzidi uwezo wake wa kimwili, kiakili, au kihisia.
Kila amri, kila wajibu, kila mtihani umeandikwa kwa kipimo cha uwezo wa mhusika.

Kwa lugha nyepesi:
Hakuna amri ya Allah iliyoundwa ili kukuvunja, bali ili kukujenga.

Maelezo kwa undani
1️⃣ Katika ibada
Mgonjwa → anarukhusiwa kukaa kuswali
Msafiri → anarukhusiwa kufupisha swala
Asiyeweza kufunga → analipa au kutoa fidia
Hii inaonyesha kuwa Uislamu si mzigo, bali ni rahma inayobadilika kulingana na hali ya mtu.

2️⃣ Katika mitihani ya maisha
Kupoteza mpendwa, umasikini, maradhi, changamoto za maisha…
Aya hii hutukumbusha:

Kama mtihani umefika kwako, basi ndani yako pia kuna uwezo wa kuubeba, hata kama huujui bado.
Ni kama Allah anakabidhi mzigo pamoja na mabega yanayoweza kuubeba

3️⃣ Katika hesabu ya matendo
Allah hahukumu kwa:

Kile ambacho hukuweza
✔️ Bali kwa kile ulichoweza lakini hukufanya
Ndiyo maana aya inaendelea:
“Kila nafsi itapata mema iliyoyachuma, na itapata mabaya iliyoyachuma…”

Ujumbe wa faraja
Aya hii:
Huondoa hofu ya kushindwa
Huondoa mawazo ya “mimi siwezi”
Huleta tumaini kwamba kila jaribu lina ufunguo wake ndani yako

Ni aya inayosema kwa sauti tulivu:
“Usiogope mzigo wa leo, kwa sababu nguvu ya leo pia ipo.”


Kauli ya Allah:
“Allah haikalifishi nafsi isipokuwa kwa uwezo wake”
si maneno ya sheria pekee, bali ni ahadi ya rehema, muhuri wa huruma, na ujumbe wa matumaini kwa kila moyo unaohisi kuchoka.
 
SHAABAN MWEZI WA MAANDALIZI

JE UNAJUA UFAULU WA HAKIKA NA UNAIJUA KHASARA YA WAZI ISOKUA NA SHAKA?

Kila mwenye akili anatamani kufaulu na ndio malengo yake , na kila mwenye akili anaikimbia khasara

Na watu hukaa na kuwaeleza watu waliofaulu na kufanikiwa kwa kuwataka wanaoskiliza na kuzingatia wawe mfano wao , kama ilivyokua hivyo hivyo watu hukaa na kuwazungumza watu waliofeli na kupata khasara na kuwatahadharisha watu wasiwe mfano wao

JE NI YUPI ALIEFAULU ?

Amesema mola wetu mlezi katika kitabu kitukufu :
{ فمَن زُحۡزِحَ عَنِ ٱلنَّارِ وَأُدۡخِلَ ٱلۡجَنَّةَ فَقَدۡ فَازَۗ وَمَا ٱلۡحَیَوٰةُ ٱلدُّنۡیَاۤ إِلَّا مَتَـٰعُ ٱلۡغُرُورِ }
Na atakaye epushwa na Moto na akatiwa Peponi basi huyo amefuzu , Na maisha ya dunia si kitu ila ni starehe ya udanganyifu.

[Surah Āli-ʿImrān: 185]

Fanya yenye kuwa sababu ya wewe kuipata pepo uwe miongoni mwa waliofaulu

NI NANI ALIEPATA KHASARA

Amesema mola wetu mlezi :
{ فَٱعۡبُدُوا۟ مَا شِئۡتُم مِّن دُونِهِۦۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡخَـٰسِرِینَ ٱلَّذِینَ خَسِرُوۤا۟ أَنفُسَهُمۡ وَأَهۡلِیهِمۡ یَوۡمَ ٱلۡقِیَـٰمَةِۗ أَلَا ذَ ٰ⁠لِكَ هُوَ ٱلۡخُسۡرَانُ ٱلۡمُبِینُ }
Basi nyinyi abuduni mpendacho badala yake Yeye. Sema: Hakika walio pata khasara ni wale walio khasirika nafsi zao na familia zao Siku ya Kiyama. Tambueni kuwa hiyo ndiyo khasara iliyo dhaahiri.

[Surah Az-Zumar: 15]

Abudu utakacho kwa maana ya weka mbele na kubali kuwa dhalili kwa chochote kile unachokitaka na kipe nafasi, mpaka kiwe na nafasi kwako mfano wa nafasi ya ibada ( kwakua sisi waislam ibada ndio jambo lenye nafasi kubwa kwetu ) , lakini tambua khasara ya wazi si khasara ya hapa duniani ya kuondoka hujajenga au huna gari laa bali khasara ya wazi kabisa ni kukhasirika siku ya kiyama kwa kukosa ibada sahiih zenye kukubaliwa

MBELE YETU KUNA MSIMU WA KUSABABISHA KUIPATA PEPO NA KUSALIMIKA NA MOTO, ILI KUUPATA UFAULU WA HAKIKA NA KUSALIMIKA NA KHASARA YA WAZI KWA KIPI UMEJIANDAA?

MAANDALIZI NI SASA NA MATENDO NI UNAPOINGIA MSIMU WENYEWE

Abu fat'hiya khamis kiza
 
“Enyi mlioamini! Itakapoitwa Swala kwa siku ya Ijumaa, nendeni upesi mkamkumbuke Allah na acheni biashara…”
(Qur’an 62:9)


Maana ya “nendeni upesi”
Neno la Kiarabu lililotumika ni “fas‘aw” (فَاسْعَوْا).

Haimaanishi kukimbia kwa miguu kama mtu anayekimbilia basi la mwisho

Wanazuoni wengi wamefafanua kuwa maana yake ni:

Kuwahi kwa nia ya dhati
Kujiandaa mapema
Kutanguliza Swala ya Ijumaa kuliko shughuli za dunia

Kwenda kwa utulivu lakini kwa umuhimu mkubwa
Mtume ﷺ amesema:
“Msije mkakimbia kwenda kwenye Swala, bali njooni kwa utulivu…”
(Hadithi sahihi)

Kwa hiyo, “kuwahi” hapa ni kuwahi kwa moyo na ratiba, si kwa mbio

Kwa nini Allah akaamuru kuwahi?
Siku ya Ijumaa si siku ya kawaida. Ni kama mkutano mkuu wa wiki wa Waumini.
Ndani yake kuna:

Khutba ya mawaidha

Swala ya jamaa yenye ujira mkubwa

Saa ya kukubaliwa dua


Kuchelewa kunamfanya mtu apoteze sehemu ya baraka. Kuna hadithi inayosema malaika husimama mlangoni mwa msikiti wakiandika waliowahi kwa daraja tofauti. Kadri unavyowahi, ndivyo thawabu inavyokuwa kubwa.

“Acheni biashara” ina maana gani?
Aya inaendelea:

“…na acheni biashara. Hayo ni bora kwenu ikiwa mnajua.”
Hii inaonyesha kuwa:
Kazi
Biashara
Mikutano
Shughuli za dunia
Vyote vinasimama kwa muda kwa ajili ya kumtanguliza Allah.

Hii si kupinga kazi, bali ni kuweka kipaumbele. Dunia ni safari, Ijumaa ni kituo cha kujaza roho mafuta

Funzo kuu la aya
Dini inahitaji nidhamu ya muda.
Kumtanguliza Allah huleta baraka katika kazi zako baadaye.

Ijumaa ni siku ya umoja wa Waislamu.
Mtu anayewahi Ijumaa huwa kama anayewahi neema kabla milango haijafungwa.
 
Tukigusia hizi ndoa zinazofungwa kuelekea Ramadhan tunapata picha kuwa ndugu zetu Waislamu ni wanafiki konki.
Yaani Mungu gani anayeweka kipaumbele mwezi wa watu kuwa watakatifu?
Swali: Kama Waislamu wanafunga kwanini demand ya chakula masokoni iwe kubwa?
Wazee wa marketing imekaaje hii?
Walaji wamepungua lakini wafanyabiashara wa vyakula masokoni hushangilia. Imekaa vipi hii?
 
Ndugu unasema mungu gani anaweka mwezi wa upendeleo vp umeitizama kwa lezima 😁
 
Reactions: Lax
Kobazi ni wehu.

1 . Wenye mgogoro na chadema ni Kobazi
2. wenye mgogoro na CUF ni kobaz
Hao jamaa wana PHD za unafiki
 

Nitajisikia aibu kama Mkristo mwenzangu anaweza kuwakosea adabu waislam kwa kiwango hiki!

Kwanza nikuhakikishie mambo yafuatayo ( Mimi ni Mkristo safi ila )

1. Mwislam aliyeshika dini ni mwaminifu mara nyingi sana kwa ibada zake zaidi ya Wakristo.

2. Waislam walioshika dini ni waaminifu mno kufanya nao Biashara ( hawalo haramu )

3. Waislam ni watiifu mno kwa maelekezo ya Imani yao, mara dufu kulinganisha na WA Kristo.

Tujifunze Kuheshimi dini za wenzetu, wana maelekezo yao kwa Imani yao, huna sababu ya kuya challenge, ila unaweza ongea ubora wa Imani yako, Kama watashawishika ni sawa!

Mambo ya Dini za watu achana nayo no ya kizamani sana, Fool!
 
Nani alisema kobazi wanafunga?kobazi wanabadili tu ratiba ya chakula kutoka mchana kwenda usiku,na usiku wanakula kama viwavijeshi halafu ikifika mchana wanajifanya wamefunga huku full kubeua,vijamaa vinafiki kiwango cha lami.

Hii wameiga kutoka kwa muddy,alikua akitamani mke wa mtu anajifanya kashukiwa wahayi😅 ili awapige chenga maamuma.
 
Huwajui kobazi ww kaa kutulia.
 
Mwezi wa Ramadan demand ya chakula inakuwa kubwa sabab Ramadan ni kama sikukuu. Ni mwezi ambao mnakuwa chakula ambacho siku za kawaida hamli. Mihogo, viazi, tambi na uji ambao katika siku za kawaida ni ngum kukuta mtu anakunywa uji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…