ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,597
- 21,640
Naam ndugu zangu katika imani,sasa ebu tuangalie mambo ya HESABU
Inaposemwa kuamini juu ya hesabu ni kuamini kwamba tunahesabiwa kwa matendo yetu tunayo fanya,kila jema au ovu unalofanya linaingia katika akaunti ama ya mema au mabaya
Na Allah wallah ni rahim mno,jema moja hulipwa thawabu kumi mfano wake na ovu moja hulipwa kwa ovu moja tu,lakini inashangaza maovu yatashinda mema na mtu kuingia motoni! Allah atujalie tusiwe miongoni mwao
Na jema moja kulipwa thawabu kumi ni kwa uchache lkn malipo hufikia mpaka mara mia saba na zaidi,na hii itatokana na nia yako unapofanya jambo hilo husika,nia yako ikiwa madhubuti kabisa kwa kutaka radhi za Allah basi utapata malipo zaidi
Kwahiyo ni jukumu letu kufanya mambo ya kheri zaidi ili tukusanye thawabu nyingi zaidi ili besabu zetu ziwe nzur zaidi
Kuonyesha ukarimu wa Allah juu ya waja wake,ukinuia tu kufanya jambo jema na bahati mbaya usilifanye basi unalipwa thawabu moja,na lau ukalifanya unapata kumi mfano wake
Na ukinuia kufanya jambo baya na usilifanye unalipwa jema moja au unapata thawabu moja na lau ukalifanya unapata ovu moja,ebu angalia jinsi Mola wetu mtukufu alivyokuwa mkarimu mno
Sijui huwa tunafeli wapi?
Kikubwa jitahidi sana kuwekeza katika mambo ya kheri ili kesho akhera uwe miongoni mwa waja wenye kupata rehma za Allah,na tujitahidi sana kuwekeza katika mambo ya kheri ambayo ya kuendelea hata kama tutaondoka hapa duniani basi tuendelee kupata hesabu nzuri
Mfano chimba kisima,panda miti yenye kivuli na matunda ambapo watu watanufaika,jenga misikiti kwa kuchangia sadaka zako katika ujenzi wa nyumba za Allah,jenga madrassa na mambo kama hayo,haya mambo hata ukifa bado utaendelea kuchuma thawabu
Na mwezi huu wa ramadhani kama uchumi wako unaruhusu toa sana sadaka kwa ajili ya Allah kwani malipo yake ni marudufu
Swali sana swala za sunna ikiwemo tarawehe kwani kipindi cha ramadhani swala ya sunna hulipwa kama swala ya faradhi na swala ya faradhi hulipwa mara sabini,ewe mja wa Allah huu ni mwezi wa kuchuma basi pambana upate machumo bora zaidi
Kwahiyo amini katika hesabu za matendo yako na ndio hizo zitakuwa mustakabali wako wa kuingia peponi au motoni
Tumche Allah
Inaposemwa kuamini juu ya hesabu ni kuamini kwamba tunahesabiwa kwa matendo yetu tunayo fanya,kila jema au ovu unalofanya linaingia katika akaunti ama ya mema au mabaya
Na Allah wallah ni rahim mno,jema moja hulipwa thawabu kumi mfano wake na ovu moja hulipwa kwa ovu moja tu,lakini inashangaza maovu yatashinda mema na mtu kuingia motoni! Allah atujalie tusiwe miongoni mwao
Na jema moja kulipwa thawabu kumi ni kwa uchache lkn malipo hufikia mpaka mara mia saba na zaidi,na hii itatokana na nia yako unapofanya jambo hilo husika,nia yako ikiwa madhubuti kabisa kwa kutaka radhi za Allah basi utapata malipo zaidi
Kwahiyo ni jukumu letu kufanya mambo ya kheri zaidi ili tukusanye thawabu nyingi zaidi ili besabu zetu ziwe nzur zaidi
Kuonyesha ukarimu wa Allah juu ya waja wake,ukinuia tu kufanya jambo jema na bahati mbaya usilifanye basi unalipwa thawabu moja,na lau ukalifanya unapata kumi mfano wake
Na ukinuia kufanya jambo baya na usilifanye unalipwa jema moja au unapata thawabu moja na lau ukalifanya unapata ovu moja,ebu angalia jinsi Mola wetu mtukufu alivyokuwa mkarimu mno
Sijui huwa tunafeli wapi?
Kikubwa jitahidi sana kuwekeza katika mambo ya kheri ili kesho akhera uwe miongoni mwa waja wenye kupata rehma za Allah,na tujitahidi sana kuwekeza katika mambo ya kheri ambayo ya kuendelea hata kama tutaondoka hapa duniani basi tuendelee kupata hesabu nzuri
Mfano chimba kisima,panda miti yenye kivuli na matunda ambapo watu watanufaika,jenga misikiti kwa kuchangia sadaka zako katika ujenzi wa nyumba za Allah,jenga madrassa na mambo kama hayo,haya mambo hata ukifa bado utaendelea kuchuma thawabu
Na mwezi huu wa ramadhani kama uchumi wako unaruhusu toa sana sadaka kwa ajili ya Allah kwani malipo yake ni marudufu
Swali sana swala za sunna ikiwemo tarawehe kwani kipindi cha ramadhani swala ya sunna hulipwa kama swala ya faradhi na swala ya faradhi hulipwa mara sabini,ewe mja wa Allah huu ni mwezi wa kuchuma basi pambana upate machumo bora zaidi
Kwahiyo amini katika hesabu za matendo yako na ndio hizo zitakuwa mustakabali wako wa kuingia peponi au motoni
Tumche Allah