Katika suratil al asiri Allah ameapa kwa wakati,hakika wakati ni rasimali muhumu sana katika maisha ya mwanadamu,kwahiyo usiutumie wakati wako vibaya hata kidogo hasa katika mwezi huu wa ramadhani

Utamsikia mtu anasema ngoja niende kijiweni nikapoteze wakati hakika ni msiba mkubwa,huu ni wakati wa kufanya amali nyingi zaidi,sikiliza darsa na mawaidha ya dini,soma qur'an,fanya dhikri utajo wa Allah kwa wingi na yale yote ambayo yatakuongezea akaunti ya mema yako

Masiku yenyewe ni machache mno kama anavyosema Allah subhana wa taala,basi ndugu zangu katika imani huu si wakati wa kupoteza mda kuangalia filamu na series mbali mbali,bali ni wakati wa kufanya amali zaidi kadri iweze kanavyo ili tufaidike na mwezi huu

Mtume Muhammad swalla llahu alaihy wasalaam,anasema hakika amepata khasara yule ambaye ramadhani imemfikia na kisha asisamehewe na Allah
 
Hakika matendo bora kabisa ni yale ya mwisho,na hata ramadhani hii ubora wake hasa huja mwishoni na ndio maana hata usiku wa laila tul qadir inasemwa umewekwa katika kumi la mwisho

Ndugu zangu kwakujua hilo kipenzi chetu Muhammad swalla llahu alaihy wassalaam alikuwa anapenda kuomba dua hii katika uhai wake,nasi ni bora tutakidhirisha kuiomba sana dua hii

"Ewe Allah ufanye umri wangu uwe bora zaidi katika mwisho wake,uyafanye matendo yangu yawe bora zaidi katika mwisho wake na uifanye siku yangu ya mwisho bora ni siku nikakayo kutana na wewe"

Inasemwa hutokea mtu akafanya matendo mazuri sana katika umri wake kisha ikabakia ridhaa moja au mbili kuifikia pepo kisha akafanya matendo ya watu wa motoni na kisha kuingia motoni

Inasemwa mtu hutokea akafanya matendo mabaya katika umri wake wote,kisha ikabakia ridhaa moja au mbili kufikia motoni kisha akafanya matendo ya watu wa peponi kisha akaingi peponi

Dua hiyo ya Mtume inaonyesha umuhimu wa kuomba mwisho mwema,kwahiyo tusiache sana kumuomba Allah atupe mwisho mwema

Katika miongoni mwa vita za jihadi,kuna mtu mtu mmoja alikuwa anapigana kwa juhudi kubwa sana katika njia ya Allah,mpaka wakasema mtu huyu ataingia peponi,lkn Mtume alivyowasikia akasema mtu huyu ataingia motoni

Hakika wakiwa uwanja wa vita,masahaba hawakumuelewa kabisa mtume,inakuwaje mtu huyu tunae hapa anapigana katika njia ya Allah na kisha isemwe ataingia motonii,kwakweli iliwasumbua kidogo hii kauli ya rasul

Kama inavyojulikana Mtume swalla llahu alaihy wa salaam hasemi kwa matamanio yake bali huwa ni maono au wahyi toka kwa Allah,basi mwisho wa siku yule mtu kutokana na majeraha aliyoyapata akashindwa kuvumilia maumivu na mwisho wa siku akajiua

Hapo sasa ndio masahaba wakazinduka kutoka usingizini na kukumbuka kauli ya rasul juu ya mtu huyo kuingia motoni

Kumbuka mwisho bora wa matendo yetu ni ya mwisho kabisa,haijalishi ulifanya dhambi gani kubwa,tubadilike na tuazimie kuwa na mwisho mwema na tuombe sana kwa Allah atupe mwisho mwema
 
Mtume Muhammad rehma na amani ziwe juu yake,anasema akitaka mtu daftar lake la matendo limfurahishe siku ya kiama au siku ya hesabu basi apende sana kuomba msamaha kwa kusema astaghfirullah mara kwa mara

Na ndio maana dua bora sana kudumu nayo na ambayo pia ni dhikri nzur kuifanya mwezi huu wa ramadhani ni "Allahuma innaka afuwun tuhibulah afwa fafuana"

Ewe mola wangu hakika wewe ni msamehevu na unapenda kusamehe basi nisamehe

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
Ndugu zangu katika imani matendo ya kiibada ambayo yanapokelewa na Allah ni yale ambayo yamefanywa tu kwa kutaka radhi zake

Je swaumu yako umeifunga kwa kuwa hapo nyumbani wote wamefunga ndio maana umefunga au umefunga kwa ajili ya Allah?

Je umefunga kwakuwa wafanyakazi wenzako wote wamefunga ndio maana nawe umefunga kwa kukwepa aibu?

Je umefunga kwakuwa mume kafunga nawe umefunga au kwakuwa mke kafunga ndio nawe kwa aibu umefunga?

Ndugu yangu katika imani ikiwa umefunga kwa ajili ya watu au mazingira uliyopo basi tambua hakika unashinda na njaa tu,hutalipwa na Allah

Hakika Allah hukubali tu matendo yanayofanywa kwa ajili yake tu

Takasa nia yako kwa kila ibada iwe ni kutoa sadaka,swala,funga au amali nyingine yoyote ile hakikisha ni kwa ajili ya kupata radhi za Allah tu

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
Ukumbusho mzuri sana
 
Ukumbumsho mzuri Allah akulipe, nakukubali sana maalim wewe na kaka adriz Allah awahifadhi
 
Allahu akbar ukumbusho huu umenipa hamasa zaidi
 
Kuomba msamaha "Toba na Istighfar" ni muhimu mno ndio maana katika mambo ya kufanya mtu wakati wa kuomba dua na mtu akitaka Dua yake ikubalike kwa wepesi basi kabla ya kuomba Dua atangulize na Istighfar kwanza kwani madhambi ni kiwazo Cha mambo mengi na chanzo Cha mabalaa.

Kutilia mkazo swala hilo Mtume Mwenyewe Muhammad (Swala na Salamu ziwe juu yake ) licha ya kusamehewa madhambi yake yote yaliyopita na yajayo lakini alikuwa akiomba Msamaha kwa Allaah zaidi ya mara 100 kwa siku , halafu sisi ambao tunakosea kila siku huenda mtu ikampita miezi hajawahi kukakaa kitako kutafakari kusuhu madhambi yake na kutubia na kuomba msamaha.

Na kuomba msamaha na kutubia ni miongoni mwa vitu anavyovioenda mno Allaah ('Azza wa Jalla) kwa mja wake kwani yeye mwenyewe amejifu kuwa msamehevu sana , mwenye huruma , mwenye Kukubali Toba kwa waja nk.

Na inapaswa tuwe tunaopa msamaha na Toba kila mara tunapokosea bila kujali ukubwa wa madhambi yetu , tumerudia mara ngapi dhambi hiyo nk .

Na iwe utaratibu wetu mara kwa mara sio tu muda ambao tunahisi tumekosea ,hapana iwe ni ada yetu sababu Inapendeza Allaah na kuonyesha Utiifu na unyenyekevu kwake Allaah subhanahu wa taa'la na huenda tukifanya madhambi bila kujua na ikawa ninkheri kwetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…