Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,151
Tuliwahi kuandika hapa JF kuwa hakuna uteuzi au utenguaji unaofanyika kwa bahati mbaya au nzuri, kila uteuzi na utenguaji wa rais hapa Tanzania ni mpango kamili na mkakati mahususi wa muda mfupi, kati au umrefu.
Pia soma >
Kuna jambo fulani niliwahi kudokezwa siku nyingi kidogo kuhusu Profesa Kitila Mkumbo kwenye utawala wa mama nikabakia kushangaa na kusubiri kuona kama kweli litatokea ili niamini. Niliambiwa Kitila Mkumbo angeondolewa kwenye nafasi ya uwaziri (kama geresha ili kuwafumba macho watanzania) halafu baadaye atarejeshwa tena mambo yakiiva!
Unaweza usiamini sana, lakini fahamu tu, katika utawala wa mama, Professa Kitila Mkumbo ndio dalali muhimu wa mapatano katika deal la uuzwaji wa bandari za Tanganyika kwenda kwa waarabu wa Dubai. Muarabu wa Dubai anamuelewa vyema tangu mwanzo Profesa Kitila kwenye hili deal na kwa hali ilipofikia sasa (moto unaowaka chini kwa chini) kwa gharama zote Profesa Kitila imebidi apewe tena majukumu mahususi kumpooza muarabu mezani ili mambo yaende kama awali.
Ili kufanya mambo yaende sawa, kuondoa hatari ya siri kuvuja ovyo na kupunguza miruzi mingi, imebidi haraka sana suala la Mipango liondolewe kutoka wizara ya fedha na suala la uwekezaji (ambalo tayari mchakato wake ulishakamilika ili kulihamisha) liondolewe kutoka viwanda na biashara ili kuundwa kwa wizara mpya ya mipango na uwekezaji, kisha iwe chini ya ofisi ya rais na waziri apewe Profesa Kitila Mkumbo!
Kama tulivyozoea kumuona Profesa Kabudi akiwa mchenga wa deal za Magufuli kipindi kile cha issue za madini na siasa za kidiplomasia, tutegemee kumuona Profesa Kitila na deal za uuzwaji wa Bandari kwenda uarabuni.
Watu wengi wanadanganywa kuwa hili suala la uuzwaji wa bandari limeanza mwaka huu, kiufupi mikataba halisi ilishafanyika tangu mwaka jana, na deal lilianza kutengenezwa tangu mwaka juzi Profesa Kitila akiwa ni waziri husika.
Pia wapo watu wanadhani Profesa Kitila ni mpya kwenye hiyo nafasi, lakini kiuhalisia alishawahi kuwa waziri ofisi ya rais (uwekezaji)hapo kabla tena akiteuliwa na Magufuli. Mwisho kabisa wapo watu wanaodhania kuwa Profesa Kitila amepewa hiyo nafasi kwa kuwa amekuwa mtetezi muhimu wa serikali kuhusu sakata la bandari kuuzwa kwa muarabu, basi watu hao huenda wako sahihi kwa 100%. Siri ya mtungi aijuaye kata!
Kaa mkao wa kula, kuna mengi yatafuata!
Pia soma >
- Rais Samia aunda Wizara Mpya na kufanya Mabadiliko ya kimuundo baadhi ya Wizara. Amteua Profesa Kitila Mkumbo kuwa Waziri
- Prof. Kitila Mkumbo: Watanzania hawapingi uwekezaji wa Bandari, wanataka Mikataba iwe Mizuri
- Serikali imependekeza Sheria zinazolinda Maliasili na Kuikinga Nchi na Mikataba Mibovu zisitumike kwa DP World
Kuna jambo fulani niliwahi kudokezwa siku nyingi kidogo kuhusu Profesa Kitila Mkumbo kwenye utawala wa mama nikabakia kushangaa na kusubiri kuona kama kweli litatokea ili niamini. Niliambiwa Kitila Mkumbo angeondolewa kwenye nafasi ya uwaziri (kama geresha ili kuwafumba macho watanzania) halafu baadaye atarejeshwa tena mambo yakiiva!
Unaweza usiamini sana, lakini fahamu tu, katika utawala wa mama, Professa Kitila Mkumbo ndio dalali muhimu wa mapatano katika deal la uuzwaji wa bandari za Tanganyika kwenda kwa waarabu wa Dubai. Muarabu wa Dubai anamuelewa vyema tangu mwanzo Profesa Kitila kwenye hili deal na kwa hali ilipofikia sasa (moto unaowaka chini kwa chini) kwa gharama zote Profesa Kitila imebidi apewe tena majukumu mahususi kumpooza muarabu mezani ili mambo yaende kama awali.
Ili kufanya mambo yaende sawa, kuondoa hatari ya siri kuvuja ovyo na kupunguza miruzi mingi, imebidi haraka sana suala la Mipango liondolewe kutoka wizara ya fedha na suala la uwekezaji (ambalo tayari mchakato wake ulishakamilika ili kulihamisha) liondolewe kutoka viwanda na biashara ili kuundwa kwa wizara mpya ya mipango na uwekezaji, kisha iwe chini ya ofisi ya rais na waziri apewe Profesa Kitila Mkumbo!
Kama tulivyozoea kumuona Profesa Kabudi akiwa mchenga wa deal za Magufuli kipindi kile cha issue za madini na siasa za kidiplomasia, tutegemee kumuona Profesa Kitila na deal za uuzwaji wa Bandari kwenda uarabuni.
Watu wengi wanadanganywa kuwa hili suala la uuzwaji wa bandari limeanza mwaka huu, kiufupi mikataba halisi ilishafanyika tangu mwaka jana, na deal lilianza kutengenezwa tangu mwaka juzi Profesa Kitila akiwa ni waziri husika.
Pia wapo watu wanadhani Profesa Kitila ni mpya kwenye hiyo nafasi, lakini kiuhalisia alishawahi kuwa waziri ofisi ya rais (uwekezaji)hapo kabla tena akiteuliwa na Magufuli. Mwisho kabisa wapo watu wanaodhania kuwa Profesa Kitila amepewa hiyo nafasi kwa kuwa amekuwa mtetezi muhimu wa serikali kuhusu sakata la bandari kuuzwa kwa muarabu, basi watu hao huenda wako sahihi kwa 100%. Siri ya mtungi aijuaye kata!
Kaa mkao wa kula, kuna mengi yatafuata!