Waziri Prof. Kitila Mkumbo - Tukiongeza Ufanisi Tutafaidika Zaidi na Bandari Zetu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

WAZIRI PROF. KITILA MKUMBO - TUKIONGEZA UFANISI TUTAFAIDIKA ZAIDI NA BANDARI ZETU

"Wenzetu wamepeleka sumu nyingi kwa watu na hawataki tuiondoe, tulikuwa tunawaangalia wakadhani CCM haipo, CCM ipo, serikali ipo na watu wake tupo tutafanya kazi hii (ya kutoa elimu kuhusu uwekezaji wa bandari) hadi kieleweke" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Miaka 30 iliyopita nchi yetu ilikuwa na uchumi uliohodhiwa na serikali, kila shughuli za uchumi zilikuwa zinafanywa na serikali. Baada ya miaka 30 ya uhuru tukaamua tubadilishe mwelekeo wa kisera na kwenda kwenye uchumi wa soko, na uchumi wa soko unagawanya majukumu katika maeneo mawili moja ni kwa serikali na jingine kw sekta binafsi" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Duniani imeonekana njia nzuri ya kuleta maendeleo sio kutegemea misaada bali ni uwekezaji" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Ili nchi yetu ikuze uchumi ni lazima shughuli za uchumi ziongezeke, na huko duniani kuna mitaji mingi na teknolojia, na ile tuendelee ni lazima tuvute mitaji hiyo mikubwa pamoja na teknolojia ije kwetu" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Wataalam wameanisha na kueleza kwamba tukiongeza ufanisi tutafaidika zaidi na hizi bandari zetu katikati bandari zetu. Kufuatia hilo, ndipo serikali kwa niaba yetu ikatoa fursa kwa wawekezaji wenye uwezo waje kuwekeza katika bandari" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji
 

Attachments

  • Kitila-Mkumbo.jpg
    Kitila-Mkumbo.jpg
    373.6 KB · Views: 4

WAZIRI PROF. KITILA MKUMBO - TUKIONGEZA UFANISI TUTAFAIDIKA ZAIDI NA BANDARI ZETU

"Wenzetu wamepeleka sumu nyingi kwa watu na hawataki tuiondoe, tulikuwa tunawaangalia wakadhani CCM haipo, CCM ipo, serikali ipo na watu wake tupo tutafanya kazi hii (ya kutoa elimu kuhusu uwekezaji wa bandari) hadi kieleweke" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Miaka 30 iliyopita nchi yetu ilikuwa na uchumi uliohodhiwa na serikali, kila shughuli za uchumi zilikuwa zinafanywa na serikali. Baada ya miaka 30 ya uhuru tukaamua tubadilishe mwelekeo wa kisera na kwenda kwenye uchumi wa soko, na uchumi wa soko unagawanya majukumu katika maeneo mawili moja ni kwa serikali na jingine kw sekta binafsi" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Duniani imeonekana njia nzuri ya kuleta maendeleo sio kutegemea misaada bali ni uwekezaji" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Ili nchi yetu ikuze uchumi ni lazima shughuli za uchumi ziongezeke, na huko duniani kuna mitaji mingi na teknolojia, na ile tuendelee ni lazima tuvute mitaji hiyo mikubwa pamoja na teknolojia ije kwetu" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Wataalam wameanisha na kueleza kwamba tukiongeza ufanisi tutafaidika zaidi na hizi bandari zetu katikati bandari zetu. Kufuatia hilo, ndipo serikali kwa niaba yetu ikatoa fursa kwa wawekezaji wenye uwezo waje kuwekeza katika bandari" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji
Una shule nzuri tu tena kwa Tittle ya Prof, simamia yaliyo ya kweli na ujibu hoja. Usiegemee upande mmoja kisa tu umekatiwa kipande cha keki.
Siyo dhambi ukiwa kama yule Mzee anayeiongoza Moro, yaani hata ukiwa na akili kama nyuki, ukiingia tu Chichiem unakuwa hazimo., kazi unafiki tu na kujipendekeza.
 
Miaka 30 ya lini, wakati ubinafshaji ulifanyika miaka ya 90? Lini serikali imefanya biashara? Serikali ina uza huduma badala ya kutoa huduma Kwa raia, kwahiyo hiyo ndiyo anayoita biashara siyo?

Aise, acheni uwongo! Serikali ya Tanzania iliacha kufanya biashara tangu 1990 na baada ya kuvuruga na kushindwa kwakuua mashirika ya umma, ikaanza kuuza huduma na kutoza raia tozo...kwahiyo waziri asitupotoshe
 
Miaka 30 ya lini, wakati ubinafaishaji ulifanyika miaka ya 90? Lini serikali imefanya biashara? Serialli ina uza huduma badala ya kutoa huruma Kwa raia, kwahiyo hiyo inaitwa ndiyo anayooita biashara siyo?

Aise, acheni uwongo! Serikali ya Tanzania iliacha kufanya kufanya biashara tangu 1990 na baada ya kuvuruga na kushindwa kwakuua mashorika ya umma, ikaanza kuuza huduma na kutoza raia tozo...kwahiyo waziri asitupotoshe

Miaka ya 90 mpaka sasa miaka mingapi?
Tokea uhuru mpaka mika ya 90 ni miaka mingapi?

Shule mlienda kusomea ujinga?
 
Miaka ya 90 mpaka sasa miaka mingapi?
Tokea uhuru mpaka mika ya 90 ni miaka mingapi?

Shule mlienda kusomea ujinga?
Ebu nisaidie wewe mwenye kusoma na kuuelewa huo Uzi....Lini serikali ilifanya biashara ikaacha lini, mpaka ianze tena? Nisaidie kuelewa wewe uliyesoma hiyo shule, Mimi ngumbaru naona usanii tu hapa
 
Ebu nisaidie wewe mwenye kusoma na kuuelewa huo Uzi....Lini serikali ilifanya biashara ikaacha lini mpaka ianze tena? Nisaidie kielewa wewe uliyesma hiyo shule, Mimi ngumbaru naona usanii tu hapa
Kama ni usanii tu, sepa.
 
Ebu nisaidie wewe mwenye kusoma na kuuelewa huo Uzi....Lini serikali ilifanya biashara ikaacha lini, mpaka ianze tena? Nisaidie kuelewa wewe uliyesoma hiyo shule, Mimi ngumbaru naona usanii tu hapa
Kwani wewe umezaliwa mwaka gani?
Hujui kulikuwa na maduka ya kijiji na ya mtaa yanauza mchele na sigara ya serikali?unajua maana ya RTC?
Shirika la usagaji?lililokuwa linauza unga na mchele?
Hujui Tbl na TTC zote zilikuwa za Serikali?

Sasa ukiambiwa serikali ilikuwa inafanya biashara ulikuwa unaelewa nini?
Hujui hata mikate ilikuwa inatengenezwa na serikali?
Mikate ya siha unaijua??

Wewe mbona kama unabisha the obvious??
 
Aise huwa unanifurahisha kweli unavyoweza kuua argument kibabe ukibanwa😂😂😂
Huwezi mbana ... probably kasikia uvivu kukupa darasa ...uko nyuma Sana ....hujui hata wapi Mwalimu Nyerere alitoa hiyo policy ya maduka ya kijiji na mwaka gani alienda hiyo nchi
 
Bora elimu mtoe nyinyi siyo mnawapa jukumu la kutoa elimu kuhusu bandari
Wakina steve nyerere,wakina kitenge zembwela

Ova
 
Kwani wewe umezaliwa mwaka gani?
Hujui kulikuwa na maduka ya kijiji na ya mtaa yanauza mchele na sigara ya serikali?unajua maana ya RTC?
Shirika la usagaji?lililokuwa linauza unga na mchele?
Hujui Tbl na TTC zote zilikuwa za Serikali?

Sasa ukiambiwa serikali ilikuwa inafanya biashara ulikuwa unaelewa nini?
Hujui hata mikate ilikuwa inatengenezwa na serikali?
Mikate ya siha unaijua??

Wewe mbona kama unabisha the obvious??
Ukitulia na kurudia andiko hili, kisha ukarudi kunisoma, utagundua umejibu Kwa hisia Ili kujilinda pasipo kuelewa.
 
Huwezi mbana ... probably kasikia uvivu kukupa darasa ...uko nyuma Sana ....hujui hata wapi Mwalimu Nyerere alitoa hiyo policy ya maduka ya kijiji na mwaka gani alienda hiyo nchi
Aise, haya mahaba haya!
 

WAZIRI PROF. KITILA MKUMBO - TUKIONGEZA UFANISI TUTAFAIDIKA ZAIDI NA BANDARI ZETU

"Wenzetu wamepeleka sumu nyingi kwa watu na hawataki tuiondoe, tulikuwa tunawaangalia wakadhani CCM haipo, CCM ipo, serikali ipo na watu wake tupo tutafanya kazi hii (ya kutoa elimu kuhusu uwekezaji wa bandari) hadi kieleweke" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Miaka 30 iliyopita nchi yetu ilikuwa na uchumi uliohodhiwa na serikali, kila shughuli za uchumi zilikuwa zinafanywa na serikali. Baada ya miaka 30 ya uhuru tukaamua tubadilishe mwelekeo wa kisera na kwenda kwenye uchumi wa soko, na uchumi wa soko unagawanya majukumu katika maeneo mawili moja ni kwa serikali na jingine kw sekta binafsi" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Duniani imeonekana njia nzuri ya kuleta maendeleo sio kutegemea misaada bali ni uwekezaji" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Ili nchi yetu ikuze uchumi ni lazima shughuli za uchumi ziongezeke, na huko duniani kuna mitaji mingi na teknolojia, na ile tuendelee ni lazima tuvute mitaji hiyo mikubwa pamoja na teknolojia ije kwetu" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji

"Wataalam wameanisha na kueleza kwamba tukiongeza ufanisi tutafaidika zaidi na hizi bandari zetu katikati bandari zetu. Kufuatia hilo, ndipo serikali kwa niaba yetu ikatoa fursa kwa wawekezaji wenye uwezo waje kuwekeza katika bandari" - Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji
Wee professor mburula hakuna anayekataa uwekezaji kwa kuwa ndiyo njia rahisi ya kupata mtaji na kuharakisha maendeleo.

Tunachokataa sisi kama Wazalendo wa nchi hii ni mkataba mbovu na usiokubalika baina ya DPW na serikali ya CCM kukabidhi rasilimali zetu kwa DPW. Hatutaki DPW wakabidhiwe bandari zote za bahari, nchi kavu na maziwa. Hatutaki ardhi yetu kuuzwa kwa hao DPW.

Tunataka ukomo wa mkataba uwe wazi. Tunataka TPA iwe na uwezo wa kusimamia shughuli za bandari na kupata mapato ya kodi na ushuru unaotozwa kwa huduma za bandari na pia tunataka uwazi katika ajira za wazawa nk.

Tanzania ilikwisha jipatia uhuru wake hatutaki ukoloni mamboleo!
 
Tatizo letu kubwa ni kutoweka concept vizuri kabla ya ku implement.

Hapa waziri anaingia na mawazo ya kuiondoa serikali kwenye biashara as if it is true kuwa serikali inafanya biashara....Serikali ilisha binafsisha mashirika yote ikabakiza zile key ambazo zinahusiana na usalama wa nchi pamoja na service sector...kwakua ilikosea kubinafsisha nakufanya kiholela bila kufanya upembuzi yakinifu hata bila kuzi pilot, kuona pros and cons, hatimaye tukaua uchumi na misingi yake na baadaye ikapelekea serikali ikakosa mapato. Ili kufidia hilo pengo ikajiingiza kwenye kuuza huduma badala ya kutoa huduma bora baada ya kukusanya Kodi kutoka Kwa wazalishaji. Mbaya zaidi baada ya kuua vitega uchumi vyote ambavyo ilivikabidhi bila uyakinifu Kwa watu ambao hawakuwa na basisi zozote zaidi ya mawazo ya kufikirika, tukaingiza siasa kwenye uendeshaji wa zile key sectors kwakuweka watu waongoze kisiasa huku tukichukua mapato wakati mwingine kisiasa na kutumia kwenye chaguzi, ku finance posho etc, hii as a result ikapelekea mashirika hayo badala ya kujiendesha efficiently na effectively nayo yakawa hayawezi kujiendesha bila subsidies. Mbali zaidi hizo. Sabisidies hazipo kwakua serikali ilisha ua vitega uchumi vya nchi through ubinafsishaji...Tukaishia kukopa Ili ku subsidize huduma kama kujenga shule na hata kuendesha hayo mashirika yanayoendeshwa kwakukosa efficiency.

Sasa Leo unaposikia viongozi wanasema wanataka kubinafsisha sijui wanataka kubinafsisha nini ambacho hawaku binafaisha mpaka sasa...You only see kwamba hatujaelewa bado tatizo letu ninini,it's more of gambling and politicking badala ya kuelewa kwamba hatuna misingi Bora ya uchumi.

Serikali itambue kuwa inawajibu wa kujenga msingi imara wa uchumi na huo ni from scratch kwakua production zote zipo crippled, kusema inabinafsisha sijui Wana taka kutoa nini cha ziada hata baada ya kubinafsisha Kila kitu miaka hiyo ya 90, kwakua madini yote yapo private sector, kilimo Kiko private, hakuna hata kimoja kinafanywa na serikali Cha uzalishaji zaidi ya huduma ambazo wamezi commodify na kusababisha kuongeza Kwa ugumu wa maisha badala ya kuboresha maisha ya jamii... Hakuna ajira nabado unaona watu wanataka hata hiki kidogo kilichobaki wakipoke Kwa mikataba mibovu na hapo unaona kabisa ni kikundi fulani ambacho kinataka ku act smart, wakijidai kutumia mgongo wa watanzania, wanataka na wao wapate kumiliki vitu vya umma pasipo kutoa jasho....Hawataki kufufua mashirika yaliyokufa, no wanajificha kwenye kusema eti uchumi wa soko, upi huo? Haupo kwakua hakuna chochote ambacho ni chaku produce ambacho hakipo Kwa soko, kamani ndege, hiyo ni huduma, kama ni bandari hiyo ni semi huduma, kama ni nishati hiyo ni service kufuel economy na yenyewe si product japo ipo comodified....Uvuvi, ufugaji ni private

Kama serikali inataka kweli kuongea lugha sahihi, basi iseme inafufua uchumi kwakufufua mashirika ya umma yaliyouzwa lakini yakashindwa ku produce na siyo kusema wanataka kubinafsisha wakati tayari yalisha binafsishwa...


Kufufua na kutengeneza mashirika mengine yakawa private inawezekana kabisa, but they have to find right people ambao watauondoa huu uchumi kutoka kuwa political dominated na kuwa economical dominant. Hii siyo ilimradi, you need serious, committed experts na siyo siasa.
 
Infact ni muda huu serikali inatakiwa irudi katika biashara Ili iweze kutengeneza corporates ambazo zita empower watanzania na kujenga base kwenye economy ya nchi, kinyume kabisa na waziri anachotuambia watanzania. Hakuna nchi ilishawahi Jenga base ya economy kwakutegemea foreign investments.

Serikali kwakua ndiyo ilidanganywa enzo hizo ikaua uchumi na kukosesha watanzania ajira hadi kuwa impoverish, ni jukumu lake sasa kuwajenga upya Ili kuwapa uwezo wa kuform base ya economy ambayo itakuwa imara na isiyo vulnerable kwenye global economic shocks....Hizo baada ya eshatblishment at secondary stage ndizo zitakuwa private baada ya serikali kuuza hisa zake Kwa awamu Hadi kujiondoa kabisa kwenye biashara hiyo husika. Hii ni kwasababu watanzania wengi hawana purchasing power, ukiacha freely bila kuwatengenezea safety nets watageuka wachanja kuni na wateka maji katikati nchi Yao wenyewe, huku wachache wenye nafasi za kisiasa wakiwa ndiyo Wana consolidate wealth and power....Na kwakua is shortlived tunaweka amani yetu rehani
 
Watanzania tusidanganywe na ubinafsishaji ambao ndiyo umetuletea huu udhalili na ukosefu wa ajira,kama watu hawana uwezo, watafute watanzania wenye uwezo wa kusaidia wapo wengine, kwakua wengi wamesoma siku hizi na Wana exposure za kutosha ila mifumo yetu ya partisan na nepotism inayoangalia teuzi badala ya kuruhusu free competition ndiyo kikwazo....Ndiyo sababu tunahitaji Katiba mpya Ili hawa mawaziri wangefanyiwa interview tukaona if they have right thinking ama la....
 
Back
Top Bottom