Waziri Makamba: Hakuna uhaba wa mafuta nchini, amtaka Mkurugenzi wa TPDC akajieleze kabla hawajachukua hatua

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,832
January Makamba: Hakuna uhaba wa mafuta nchini. Hakuna sababu ya kuwa na taharuki. Utaratibu wa kuingiza mafuta unahakikisha kwamba mahitaji yapo wakati wote. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei.

Akijibu swali la mdau alieuliza mkanganyiko kati ya mkurugenzi wa TPDC na kauli yake kujichanganya, Makamba amesema yake ni Kauli ya uhakika ya Serikali. Mkurugenzi wa TPDC atatoa taarifa kuhusu taarifa yake kwasababu aliitoa kwenye semina ya wanahabari lakini ni gazeti moja tu ndio limeandika.

Pia amemtaka mkurugenzi wa TPDC aende ofisini kutoa maelezo kabla hajachukuliwa hatua za ziada.

Aidha, amesema Dizeli iliyopo kwenye matenki nchini hadi leo asubuhi ni lita milioni 90.7. Meli inayoitwa SLOANE SQUARE muda huu inashusha lita milioni 60.9 hivyo kupelekea mafuta ya dizeli kuongezeka na kuwa lita 151,694,926 yanayotosheleza kwa siku 24.

Petroli iliyopo kwenye matenki nchini hadi leo asubuhi ni lita 100,345,631. Meli iitwayo JAMES COOK inashusha lita 22,493,188; meli iitwayo JAG PUNIT iko njiani na lita 30,579,019 hivyo kupeleka mafuta ya petroli kuongezeka na kuwa lita 153,417,838 yanayotosheleza kwa siku 34

Pia soma > TPDC: Mafuta yaliyopo yatosha siku 15


Makamba January mafuta.JPG
 
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema haya...

“Hakuna uhaba wa mafuta nchini. Hakuna sababu ya kuwa na taharuki. Utaratibu wa kuingiza mafuta unahakikisha kwamba mahitaji yapo wakati wote. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei”.

“Kauli ya uhakika ni ya Serikali. Mkurugenzi wa TPDC atatoa taarifa kuhusu taarifa yake hii manake aliitoa kwenye semina ya wanahabari lakini ni gazeti moja tu ndio limeandika. Pia atakuja ofisini kutoa maelezo kabla hatujachukua hatua za ziada”.

Pia soma > TPDC: Mafuta yaliyopo yatosha siku 15
 
Pamoja na yoteyote binafsi ya Makamba Jr.

Naona yuko kwenye pressure sana, either kuna watu wanataka afeli au tayari mbio za Urais zimeanza kuna watu wanataka wamuharibie, maana kila kukicha linazuka jipya.

Makamba Jr kuwa mtulivu inaonekana upo kwenye vita kali, tumia akili kwenye kufanya mambo yako, hiyo wizara ni kubwa na ina mambo mengi, uko mtegoni.
 
Huenda Dk James Mataragio ambaye ni mkurugenzi mkuu wa TPDC akafutwa kazi kwa kile kilichosemwa na Makamba ni kuupotosha umma.

James, hivi karibuni alinukuliwa akisema endapo meli ya mafuta isipotia nanga ndani ya wiki mbili Nchi itashuhudia uhaba mkubwa wa mafuta jambo ambalo limeonekana kumkwaza Makamba.
 
Waziri wa Nishati Januari Makamba amesema Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio atatakiwa kufika ofisi ya Wizara kutoa maelezo kabla ya kuchukuliwa hatua kutokana na kauli yake kuwa mafuta yaliyopo yanatosha kwa siku 15 tu

Waziri Makamba kupitia ukurasa wake wa Twitter amekanusha uwepo wa uhaba wa mafuta nchini na kusema kauli ya uhakika ni ya Serikali. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei​
 
Waziri wa Nishati Januari Makamba amesema Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio atatakiwa kufika ofisi ya Wizara kutoa maelezo kabla ya kuchukuliwa hatua kutokana na kauli yake kuwa mafuta yaliyopo yanatosha kwa siku 15 tu

Waziri Makamba kupitia ukurasa wake wa Twitter amekanusha uwepo wa uhaba wa mafuta nchini na kusema kauli ya uhakika ni ya Serikali. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei​
Ninashauri iundwe tume ya kuchunguza uwepo wa mafuta au la. Makamba anaingiza nchi ngizani kwa maneno yake mengi yasio na mwisho wala mwanzo.
 
January Makamba: Hakuna uhaba wa mafuta nchini. Hakuna sababu ya kuwa na taharuki. Utaratibu wa kuingiza mafuta unahakikisha kwamba mahitaji yapo wakati wote. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei.

Akijibu swali la mdau alieliza mkanganyiko kati ya mkurugenzi wa TPDC na kauli yake kujichanganya, Makamba amesema yake ni Kauli ya uhakika ni ya Serikali. Mkurugenzi wa TPDC atatoa taarifa kuhusu taarifa yake hii kwasababu aliitoa kwenye semina ya wanahabari lakini ni gazeti moja tu ndio limeandika. Pia amemtaka mkurugenzi wa TPDC aende ofisini kutoa maelezo kabla hajachukuliwa hatua za ziada.

Pia soma > TPDC: Mafuta yaliyopo yatosha siku 15


Yale yale matisho ya mwenda kuzimu. Yaani Makamba nae kawa hivi tena??
 
Back
Top Bottom