Mahakama ya Afrika yaiagiza Tanzania kufanya marekebisho ya sheria inayowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia uchaguzi

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Kesi itakayotolewa uamuzi Leo ni kesi iliyofunguliwa na Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inapinga Vifungu vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ambavyo vinaruhusu wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi, ikidiwa kuwa 'makada wa Chama Cha Mapinduzi' ambacho ni chama tawala hivyo mpeleka maombi anadai kuwa ni vigumu uchaguzi kuwa wa huru na wa haki, lakini pia inadaiwa kuwa vifungu hivyo vinakiuka haki ya usawa mbele ya sheria ikiwa ni pamoja na haki ya wananchi kuchagua viongozi wao wanaowataka kwa uhuru.

UPDATES:
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu imeagiza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya marekebisho ya sheria ya Taifa ya uchaguzi inayotoa uhalali kwa Wakurugenzi (DED) kusimamia uchaguzi.

Uamuzi huo umetolewa kufuatia kutupilia mbali kwa mara nyingine ushahidi wa upande wa Serikali kwenye ile kesi ya kupinga hiyo.

Kufuatia maelekezo hayo mahakama hiyo imeielekeza Serikali ndani miezi 12 kupeleka ripoti ya utekelezaji wa uamuzi huo.

Ikumbukwe Kesi hiyo ambayo uamuzi wake umetolewa leo June 13, 2023, ilifunguliwa na Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inapinga Vifungu vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ambavyo vinaruhusu wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi,

Ambapo mlalakaji alidai kuwa Wakurugenzi hao ni 'makada wa Chama Cha Mapinduzi' ambacho ni chama tawala hivyo kumpelekea uchaguzi kushindwa kuwa wa huru na wa haki. Lakini pia inadaiwa kuwa vifungu hivyo vinakiuka haki ya usawa mbele ya sheria ikiwa ni pamoja na haki ya wananchi kuchagua viongozi wao wanaowataka kwa uhuru.

Inaweza kukumbukwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 baadhi ya wadau hususani wanasiasa wa vyama vya upinzani Tanzania na Wanaharakati walikosoa vipengere hivyo vinavyotoa mamlaka kwa Wakurugenzi kusimamia uchaguzi, wakitaja Wakurugenzi hao waliokuwa na dhamana kuwa ni makada wa Chama tawala hivyo ilikuwa ni vigumu kwao kusimamia misingi na taratibu za uchaguzi licha ya baadhi ya wengine kuwa na mtazamo tofauti.

Akizungumza kuhusu kesi hiyo mara baada ya uamuzi,Wakili wa upande wa mleta maombi, Jebra Kambole amesema kuwa walichukua uamuzi wa kufungua shauri hilo wakiamini wanaweza kupata haki licha ya kushindwa kwenye mahakama ya rufaa.

“Baada ya kushindwa hiyo kesi mahakama ya Rufaa tuliamini kuna haki zetu hazijawa sawa kwahiyo tukapeleka kesi kwenye mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, kwamba vile vifungu vinavyotoa mamlaka kwa wakurugenzi (DED) vinakiuka mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu”amesema Wakili Jebra Kambore

Ameongeza kuwa “Mahakama imekubaliana na sisi kuwa sheria haijaweka vigezo vya Wakurugenzi hao kusimamia uchaguzi, mahakama imeona kuwa kutokana na kutokuwepo kwa vigezo ni kwamba mtu yoyote anaweza kusimamia uchaguzi. Mahakama imesema Wakurugenzi wasisimamie uchaguzi"

Ikumbukwe Kesi hiyo ambayo uamuzi wake umetolewa leo June 13, 2023, ilifunguliwa na Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inapinga Vifungu vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ambavyo vinaruhusu wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.

Ambapo mlalakaji alidai kuwa Wakurugenzi hao ni 'makada wa Chama Cha Mapinduzi' ambacho ni chama tawala hivyo kumpelekea uchaguzi kushindwa kuwa wa huru na wa haki. Lakini pia inadaiwa kuwa vifungu hivyo vinakiuka haki ya usawa mbele ya sheria ikiwa ni pamoja na haki ya wananchi kuchagua viongozi wao wanaowataka kwa uhuru.

Inaweza kukumbukwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 baadhi ya wadau hususani wanasiasa wa vyama vya upinzani Tanzania na Wanaharakati walikosoa vipengere hivyo vinavyotoa mamlaka kwa Wakurugenzi kusimamia uchaguzi, wakitaja Wakurugenzi hao waliokuwa na dhamana kuwa ni makada wa Chama tawala hivyo ilikuwa ni vigumu kwao kusimamia misingi na taratibu za uchaguzi licha ya baadhi ya wengine kuwa na mtazamo tofauti.

images%20(8).jpg
 
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu imepiga marufuku Wakurugenzi kusimamia chaguzi, yaagiza serikali kufanya marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kupeleka ripoti ya utekelezaji wa marekebisho hayo ndani ya miezi 12.

Mahakama ya Afrika.jpg

Kesi hii ilifunguliwa na mwanasheria Bob Wangwe kupinga wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mtaa kusimamia uchaguzi. Itakumbwa kuwa hii ni mara ya pili kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kupigwa marufuku kusimamia uchaguzi mbali na uamuzi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoamua kuwa waendelee kusimamia chaguzi kwa sababu wanakula viapo vya kukana uanachama wao wa vyama vya siasa kabla ya kusimamia chaguzi.

Chanzo: Jambo TV
 
BreakingNews; Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu imepiga marufuku wakurugenzi kusimamia chaguzi,yaagiza serikali kufanya marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kupeleka ripoti ya utekelezaji wa marekebisho hayo ndani ya miezi12. Kesi hii ilifunguliwa na mwanasheria Bob Wangwe kupinga wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mtaa kusimamia uchaguzi.Itakumbwa kuwa hii ni mara ya pili kwa wakurugenzi wa Halmashauri kupigwa marufuku kusimamia uchaguzi mbali na uamuzi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoamua kuwa waendelee kusimamia chaguzi kwa sababu wanakula viapo vya kukana uanachama wao wa vyama vya siasa kabla ya kusimamia chaguzi
Ushindiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii asante Wangwe
 
Hayawi hayawi sasa yamekua, Mahakama ya Haki za Binadamu - Arusha imetoa hukumu na kupiga marufuku Wakurugenzi na Watendaji wa Halmashauri kusimamia uchaguzi na kwamba Serikali imemuriwa krekebisha sheria hio na kutoa mrejesho wa utekelezaji wa hukumu hii ndani ya miezi 12.

Hili litakua pigo lingine kubwa kwa serikali ya CCM na ushindi kwa wapenda Haki wote wakiongozwa na CHADEMA.

1686651405727.png
 
Utashanga hayo ma ccm yanakata tena rufaa. Yaani Mkurugenzi (kijana/binti wa uvccm) aliyeteuliwa na Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa ccm, eti ndiyo amtangaze mgombea mshindi kutoka chama cha upinzani!! Kirahisi tu!

Yaani ma ccm yanawaona wananchi kama hawana akili vile. Mimi ndiyo maana niliapa mwaka 2019! Siji kupiga kura mpaka hapo nitakapo jiridhisha, kuheshimiwa kwa hiyo kura yangu kupitia Tume Huru ya Uchaguzi.
 
Ushindiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii asante Wangwe
Sasa hawa ndio vijana tunaowataka. Sijaona hata siku moja akijipendekeza kwa watawala hata kuzungumza anazungumza ukweli mtupu.
Ila yapo mavijana hapa nchini na mengine yamo humu ukiyaona yasemayo au kuandika unaweza kukufuru kuwa kuliko kuwa nao bora kufuga mbuzi kwa ajili ya supu sikukuu za Iddi na Pasaka.
 
BreakingNews; Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu imepiga marufuku wakurugenzi kusimamia chaguzi,yaagiza serikali kufanya marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kupeleka ripoti ya utekelezaji wa marekebisho hayo ndani ya miezi12. Kesi hii ilifunguliwa na mwanasheria Bob Wangwe kupinga wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mtaa kusimamia uchaguzi.Itakumbwa kuwa hii ni mara ya pili kwa wakurugenzi wa Halmashauri kupigwa marufuku kusimamia uchaguzi mbali na uamuzi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoamua kuwa waendelee kusimamia chaguzi kwa sababu wanakula viapo vya kukana uanachama wao wa vyama vya siasa kabla ya kusimamia chaguzi
Wazee wa goli la mkono watakata rufaa!!
 
Sasa hawa ndio vijana tunaowataka. Sijaona hata siku moja akijipendekeza kwa watawala hata kuzungumza anazungumza ukweli mtupu.
Ila yapo mavijana hapa nchini na mengine yamo humu ukiyaona yasemayo au kuandika unaweza kukufuru kuwa kuliko kuwa nao bora kufuga mbuzi kwa ajili ya supu sikukuu za Iddi na Pasaka.
Apatiwe Maua yake!
 
BreakingNews; Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu imepiga marufuku wakurugenzi kusimamia chaguzi,yaagiza serikali kufanya marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kupeleka ripoti ya utekelezaji wa marekebisho hayo ndani ya miezi12. Kesi hii ilifunguliwa na mwanasheria Bob Wangwe kupinga wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mtaa kusimamia uchaguzi.Itakumbwa kuwa hii ni mara ya pili kwa wakurugenzi wa Halmashauri kupigwa marufuku kusimamia uchaguzi mbali na uamuzi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyoamua kuwa waendelee kusimamia chaguzi kwa sababu wanakula viapo vya kukana uanachama wao wa vyama vya siasa kabla ya kusimamia chaguzi
Utekelezaji ndiyo itakuwa shida maana hiyo mahakama haina meno, pia Jaji wa Mahakama ya rufaa anakuwa mjinga kiasi kile anabariki MaDED kusimamia uchaguzi kwa kigezo cha kiapo? pumbafu kabisa
 
Hatua nzuri, lakini sitegemei kama hiyo hukumu itatekelezwa. Tuna uzoefu na maamuzi ya mahakama za nje zinazokwenda kinyume na sheria za watawala wa Tanzania.
 
Kuna watu watashangilia kweli...kama watoto...
Mahakama ya Africa inaweza piga marufuku kabisa nchi huru zenye mifumo yake??

Tena ipo Arusha?...

Kuna watu watashangilia utasema hiyo mahakama ina nguvu hizo za kisheria....
Mfano wakipuuzwa watafanya nini?
Wataagiza Nani afanye nini??.

Hizi zote ni stunts za kisheria
 
Back
Top Bottom