Mkuu kujiua ni kosa kisheria, na kama utakamatwa ukawa katika harakati za kujiondoa uhai sheria hiyo itakubana, je kwanini hao wanao jenga kingoni mwa mito sheria hiyo isitumike dhidi yao?Why should I care about maofisi ya serikali? Kwani kila wakati wanaokuwa katika majaribu ya maisha ni hao walioko Azikiwe au walioko Mabondeni? Hivi hapa mada ni kubomoka kwa mabarabara na madaraja au madhira wanayopata watu wa mabondeni? Hivi hata huko unakosema kungekuwa na a cery excellent infrastructure, hao watu wa Jangwani, Msimbazi and the like wangeokoka vipi?
Kwamba kama utashi wa watu ungekuwa ufanye kazi basi kusingekuwa na serikali, serikali mara zote itabaki kuwa mwelekezaji na ni mwananchi mwenyewe ndie mwenye wajibu wa kutekeleza maelekezo! Hata humu majumbani mwetu tunaishia tu kuelekezana na kukaripiana; "acha wizi" "acha uhuni" "acha hiki na kile" lakini tunapokuwa wakahidi hata wazazi nao hututupa mkono vinginevyo jela hivi sasa zingejaa watoto waliopelekwa huko na wazazi wao wenyewe baada ya kuwakaripia hili na lile na baada ya kuona hawasikii wanaamua kuwapeleka polisi! Kama bado ni mtoto mdogo, baba ako atakukanya na usiposikia atakutandika hadi mikwaju lakini ukishakuwa mtu mzima ataishia kukukanya na usiposikia, atakauacha kama ulivyo! Wale watu wa mabondeni ni mijitu mizima na akili zao na wote wanafahamu nini kitawakuta lakini tatizo huwa wanafanya mahesabu, kwamba kati ya siku 365 za mwaka, ni chini ya siku 7 ndizo watahangaika!