Mungu tuepushe na madhara ya miili, nafsi na roho zetu!.
Lawama zote ziiendee Ccm na serikali yake kwa kushindwa kuwa proactive wala reactive. Serikali ina wataalam wa miundombinu wengi ambao wamesoma vizuri wakahitimu (achana na wale wakupasishwa wa sasa), wameajiriwa na wanalipwa mishahara - kodi zetu kwa kazi hiyo.
Ni nini kinaifanya serikali ishindwe kuwatumia katika kuhakikisha miundo mbinu yetu iko vizuri ili kuepusha fedheha hii ya kurudia rudia kwa majanga ambayo yamepoteza uahi wa ndugu zetu, mali, na kuleta magonjwa ya milipuko yanayotugharimu fedha nyingi za kigeni na kudidimiza uchumi wetu? Ninaamini wataalam wana majibu sahihi ya kuboresha na kuimarisha miundo mibnu ili watanzania tuishi kwa amani na tuone mvua ni baraka na si laana ila serikali haitaki kuwatumia ama kwa kutokujali shida za wananchi ama kwa kutokujua thamani na maana halisiya utaalamu.
Ujenzi holela ambao ndio chimbuko kubwa linasopelekea athari za mvua kuwa mbaya na kwa kiwango kikubwa, unalelewa na serikali kutokuzingatia na kumaanisha kufanya kazi kwa ufanisi na kwa malengo ya kuboresha ustawi wa taifa.
Tuna mipango miji, upimaji na ramani wanalipwa mishahara kila mwezi january to december, na hadi marehemu wako kwenye payrolls za serikali. Lakini hawa watu, wanakuwa desk officers ama private dealers!.
Kuna ugumu gani wa kusurvey viwanja na maeneo kwa wingi ili anayehitaji kujenga aonyeshwe eneo lake kama vile route za magari ya abilia?
Ajabu hawa wataalam, kazi yao ni kwenda kupima maeneo kwa maombi ya watu binafsi baada ya ujenzi holela bila considerations za mahitaji muhimu ya general public, wanalipwa fedha sawa na private surveyors, kitu kinachokithirisha ukosefu wa miundo mbinu sahihi na mwisho ni kama tunavyoona.
Ni jambo lisilofikirika kwamba watu wanajenga mchana, serikali inaona haichukui hatua yoyote, badala yake inakwenda kuweka namba kwenye zile nyumba holela, inachukua kodi, wakati huo huo, umeme wanawekewa, na maji ya serikali wanapelekewa, bills wanalilpa kwa serikali kila mwezi, na soko wanajengewa, local Governments wanachukua levy, kodi wengine wanalipa na baraka zote za serikali kama vile hakuna kosa lolote lipo. Ni jambo la ajabu mvua zinaanza kunyesha, mafuriko yanaanza, serikali inawageuka eti wahame wamejenga mabondeni, mara wamejenga bila mifereji, mara eneo walilojenga si la makazi, mara walipo ni mkondo wa mto hivyo wameziba mto na hadhithi nyingi kibao.
SWALI LA KUJIULIZA, NIA THABITI YA SERIKALI KULINDA NA KUSIMAMIA MASLAHI NA USTAWI WA UMMA IKO WAPI?
KWA UZEMBE HUU, BILA KUBADILISHA UTAWALA, TANZANIA ITAKUWA BADO IPO KWA MIAKA MICHACHE IJAYO?
TAFAKARI!.