Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Duh! Wanaofanya mtihani form six wameathirika sana! Wameanza na mgomo wa madereva! Mafuriko! Sijui matokeo yatakuwaje!
 
Kufuatia hali kuzidi kuwa tete; Suleiman Kova kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam amewataka wananchi wa mkoa huo kurejea majumbani kwao mapema iwezekanavyo! Barabara nyingi hazipitiki huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha!
 
recuperation_chaleur_eau_domestique.jpg


sewage-system.jpg
 
Hii mvua ikinyesha week nzima watu watakufa njaa
 
Kule jangwani wananchi wana hali kwanza jamani
 
Kuna watu hua wanasifia wao ni wa Daresalam wanatuona wa mikoani washamba haahhhhhhhaaaaa leo kama namuona Muuza Sura anavyoogelea ,jiji ambalo ikulu ipo inashindwa kuweka miundo mbinu mizuri hhhhhheeeeeee CCM HOYEEEEEEEEEE
 
Last edited by a moderator:
Ifike wakati watu waende nje ya mji, kwani lazima kuonekana unakaa mjini ili hali unaishi kwenye bwawa la maji ya chooni???????? nyumba nyingine ni kinyaa lakini mtu anang'ang'ania hapo hapo kisa yupo karibu na kariakoo ni ujinga huo sasa. hapo serikali ya ccm haihusiki.

Mbona hadi posta hua mfuriko yanafika kwa hiyo napo wahame
 
Bahati nzuri hio ni Landcruiser kwahio tulikua salama kiasi, inatisha sana sana maji yana nguvu mno

Bahati yenu, ila nilivyo muoga ningekua ndio mimi niko kwenye hilo gari wakati wa hizo heka heka sijui ingekuwaje?
BTW....hiyo hapo juu ya dashboard ni kanda au? Mmetisha sana wakuu.
 
Acha kutendea upumbavu wewe!! Hivi mafuriko ya Dar yapo mabondeni tu? Na huko kati kati ya Jiji nani wa kulaumiwa!? Ni wananchi ndio walivamia na kujenga hovyo bila vibali? Miundo mbinu ya Dar ni bado ile ya mwaka 47 ambapo population ilikuwa 250, 000. Serikali pamoja na kuona ongezeko kubwa la watu haikufanya lolote kuboresha miundo mbinu (drainage system) lakini wewe hilo hulioni. Kuna faida gani ya kukatwa kodi kama Serikali haiboreshi mambo mbali mbali nchini ikiwemo kuepuka maafa ya mara kwa mara yanayosababishwa na utendaji mbovu. Acha kutetea ujinga wewe Ibambasi Ibambasi
 
Last edited by a moderator:
Hivi wewe ulielewa kweli nilichoandika?

Wananchi ni kina nani kwa mtazamo wako? Manake nachelea kuamini kuwa kwako wewe wananchi ni "walalahoi" wa Manzese, Tandale kwa Mtogole/kwa Tumbo, Kimara, etc.

Nyumba zipi za Msasani zimejengwa kwa kibali cha Serikali? Unazifahamu?

Wanapopiga stop magorofa, wanashindwaje kupiga stop hizo nyumba...??

Haya ile ghorofa opposite na ocean road hospital, vibali alitoa nani..??? Mbona hao hao watoa vibali ndo walitaka jengo lipunguzwe wakati lishamalizwa kujenga na linatumika..??

Haya lile ghorofa lililopo kati Seaclif na golden Tulip hotel hapa Dar lililoshikiwa bango na akina Rita Mlaki kuwa libomolewe liliishia wapi..? Mbona linatumika sasa...??? Kuiondoa serikali kwenye hili ni kazi sana...

CC

BAK
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Acha kutendea upumbavu wewe!! Hivi mafuriko ya Dar yapo mabondeni tu? Na huko kati kati ya Jiji nani wa kulaumiwa!? Ni wananchi ndio walivamia na kujenga hovyo bila vibali? Miundo mbinu ya Dar ni bado ile ya mwaka 47 ambapo population ilikuwa 250, 000. Serikali pamoja na kuona ongezeko kubwa la watu haikufanya lolote kuboresha miundo mbinu (drainage system) lakini wewe hilo hulioni. Kuna faida gani ya kukatwa kodi kama Serikali haiboreshi mambo mbali mbali nchini ikiwemo kuepuka maafa ya mara kwa mara yanayosababishwa na utendaji mbovu. Acha kutetea uzembe.

Unakatwa kodi ila wananunulia magari ya anasa. Wanakopa ila wanaenda kutumbua. Hii serikali ni majanga
 
  • Thanks
Reactions: BAK
MAFURIKO DAR - BARABARA YA MOROGORO YAFUNGWA

Kufuatia mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam na kusababisha mafuriko ambayo yamepelekea barabara kadhaa kufunikwa na maji; Serikali imetangaza kuifunga Barabara ya Morogoro katika eneo la Jangwani kufuatia daraja kufunikwa na maji.

Aidha, watu wametakiwa kuondoka mapema maeneo ya katikati ya ambako kuna foleni ndefu za magari na kwa mujibu wa utabiri wa hali ya hewa, mvua hizi zitaendelea kunyesha na ambapo madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Hadi wakazi wengi wa maeneo ya mabondeni wameripotiwa kuathiriwa na hali hii kwa nyumba zao kujaa maji na mali zao kusombwa na maji.
 
Back
Top Bottom