Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

matumbo

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2011
Posts
7,224
Reaction score
3,960
Kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha usiku kucha nimepita baadhi ya mitaa alfajiri hii na kukuta wananchi wakikimbia nyumba zao sababu ya kujaa maji ndani. Inatia huruma kwa kweli, awa watu wanahitaji msaada wa haraka kutoka kwa jamii inayowazunguka sababu Serikali imeshashindwa kuwa msaada kwa Wananchi.

Nimepita maeneo ya Tabata, Buguruni, Vingunguti nimekuja kuiona tena hali hiyo Kigogo na sasa nipo magomeni sijajua kwa ndugu zangu pale Kinondoni kutakuwaje.


=====================
Update


Watu 8 wamefariki dunia kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha nchini ambapo mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo,kinondoni wamefariki watu 6 na Temeke watu wawili.
MAFURIKO DAR - BARABARA YA MOROGORO YAFUNGWA

Kufuatia mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam na kusababisha mafuriko ambayo yamepelekea barabara kadhaa kufunikwa na maji; Serikali imetangaza kuifunga Barabara ya Morogoro katika eneo la Jangwani kufuatia daraja kufunikwa na maji.

Aidha, watu wametakiwa kuondoka mapema maeneo ya katikati ya ambako kuna foleni ndefu za magari na kwa mujibu wa utabiri wa hali ya hewa, mvua hizi zitaendelea kunyesha na ambapo madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Hadi wakazi wengi wa maeneo ya mabondeni wameripotiwa kuathiriwa na hali hii kwa nyumba zao kujaa maji na mali zao kusombwa na maji
.


===========================
Update

Mtu mmoja amefariki Dunia baada ya kusombwa na Maji kutokana na mafuriko yaliyotokana na Mvua zinazoendelea Kunyesha Dar es salaam.


attachment.php





satelite.png
 

Attachments

  • A1.png
    A1.png
    70.6 KB · Views: 4,549
  • A2.png
    A2.png
    41.5 KB · Views: 4,462
  • 4.JPG
    4.JPG
    13.7 KB · Views: 4,055
  • mvua.jpg
    mvua.jpg
    78.5 KB · Views: 9,021
Last edited by a moderator:
Tatizo kujenga ovyo bila mpangilio, kujenga mabondeni na ukosefu wa miundo mbinu ya kutolea maji wakati wa mvua,,,
 
Aisee hapo kino nilihama mwezi uliopita. Leo watakuwa wanaogelea hapo
 
Kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha usiku kucha nimepita baadhi ya mitaa alfajiri hii na kukuta wananchi wakikimbia nyumba zao sababu ya kujaa maji ndani.

Nimepita maeneo ya Tabata, Buguruni, Vingunguti nimekuja kuiona tena hali hiyo Kigogo na sasa nipo magomeni sijajua kwa ndugu zangu pale Kino kutakuwaje.

Alifajiri wewe umeshapitia mitaa yote wewe noma....pole yao waliopata mafuriko
 
Pamoja na kutokea mafuriko makubwa miaka nenda miaka rudi ambayo yamewahi kusababisha maafa na pia uharibifu mkubwa wa mali za waathirika lakini hii "Serikali sikivu" haichukui hatua yoyote ya kuboresha miundo mbinu ya jiji ili kupambana na tatizo hili ambalo linazuilika. Ukiwaambia uongozi wa nchi umewashinda wanakuja juu. Hawa wanaojiita viongozi watatembelea maeneo yaliyoathirika na kukenua kenua kama vile wamekuja na msaada wa kweli kisha hao wanasepa zao bila lolote la maana kufanywa.







 
Last edited by a moderator:
Kuna mitaa ambayo serikali ingepiga marufuku watu kuweka makazi, lakin watz ni watu wa kusahau haraka sana
 
Hakuna anaependa kujenga bondeni ni maisha tu, mtu hela ya kujenga pazuri hana na kachoka kupanga.

Ndio maana nimesema baadhi ya sehemu hatarishi serikali ingepiga marufuku toka kitambo, zingepatikana tu sehemu za uswazi za kujenga kwa bei rahisi lakin sio mabondeni.
 
Wale wa jangwani sijui watakua na hali gani maskinii
 
Ungekuwa ulaya msaada dharura saa nyingii ushafika! Ila hapa hata afe mtu
 
Back
Top Bottom