Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam


11045470_10155523151595156_2024276234841109571_n.jpg
 
Poleni wana DSM kwa mafuriko.. Hameni Dar hamtaki.
 
Wanapopiga stop magorofa, wanashindwaje kupiga stop hizo nyumba...??

Haya ile ghorofa opposite na ocean road hospital, vibali alitoa nani..??? Mbona hao hao watoa vibali ndo walitaka jengo lipunguzwe wakati lishamalizwa kujenga na linatumika..??

Haya lile ghorofa lililopo kati Seaclif na golden Tulip hotel hapa Dar lililoshikiwa bango na akina Rita Mlaki kuwa libomolewe liliishia wapi..? Mbona linatumika sasa...??? Kuiondoa serikali kwenye hili ni kazi sana...

CC

BAK

Sasa hoja yako hapo ni nini?
 
HII SERIKALI YA CCM INASHINDWA KUCHIMBA MITARO YA KUPITISHA MAJI HATA HAPO POSTA(ikulu) KUELEKEZA MAJI BAHARINI...BADO MNATAKA IENDELEE KUTAWALA NCHI. SHEM ON U
 
Acha kutendea upumbavu wewe!! Hivi mafuriko ya Dar yapo mabondeni tu? Na huko kati kati ya Jiji nani wa kulaumiwa!? Ni wananchi ndio walivamia na kujenga hovyo bila vibali? Miundo mbinu ya Dar ni bado ile ya mwaka 47 ambapo population ilikuwa 250, 000. Serikali pamoja na kuona ongezeko kubwa la watu haikufanya lolote kuboresha miundo mbinu (drainage system) lakini wewe hilo hulioni. Kuna faida gani ya kukatwa kodi kama Serikali haiboreshi mambo mbali mbali nchini ikiwemo kuepuka maafa ya mara kwa mara yanayosababishwa na utendaji mbovu. Acha kutetea ujinga wewe Ibambasi Ibambasi

Punguza munkari brother, twende hoja kwa hoja.

Nakuuliza swali moja; chanzo cha mafuriko, au tuseme, kujaa maji kwa mitaa ya Dar es Salaam mvua inaponyesha, ni kipi?
 
Maeneo ya Mbezi kutokea Goba kuna magari yametelekezwa njiani kutokana na maji mengi. Kuna gari dogo ya Toyota (jamii ya saloon kama sikosei) Imetelekezwa hapa Mbezi tangi bovu na imefunikwa na maji yanayotokea huku ukanda wa juu! Pia nyumba nyingi maeneo haya ya Mbezi beach zimezingirwa na maji na zimetelekezwa! .
Kiukweli ni balaa!, njia ya Goba Rd kutokea Massana, imekatika, hivyo magari yanapita mtaani kwangu kuzungukia.

Home kwangu maji yamefurika na kufumua ufuniko wa cesspit! maji ya mvua ndia yamejaza cesspit na kureplace contents kutitirishia barabarani!, kiukweli leo ni majanga!.

Ukuta wa Makongo sekondari, umeanguka!. Pale Tangi Bovu, kuna daladala ilitanua kumbe barabara pembeni imelowa, ikaporomoka dala dala hilo limelala mtaroni!. Pale Lugalo kumetokea landslide, pande la udogo limemegeka na kudondokea barabarani!.

Kiukweli leo... sijui!.

Pasco
 

Stranded as floods engulf the Jangwani bridge on Morogoro road in Dar es salaam today

CEZxjMAWIAAaEI9.jpg
 
Kote kote tu majanga, tunaogopa kwenda mikoani muda huu ajali nyingi sana
Hata mikoani ni hivi hivi tu, kwani kule Morogoro na mwanza mvua zilikoleta maafa sio mikoani? Tubanane hapahapa
 
Back
Top Bottom