Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

View attachment 249800
Huwezi kuamini lakini ni ukweli.. Lori Tani 20 limesombwa na mto Darajani Kinyerezi... this is now na mvua inaendelea km kawaida.


Hili gari lilijaribu kuvuka mto jana kwa kupitia bondeni, likashindwa kuvuka kwa kupata breakdown.
Mvua zilizonyesha usiku kucha leo zimelikuta hapo na siyo kwamba limesombwa na maji.
 
Madhara ya Posta ni madogo ukilinganisha na madhara ya watu wanaoishi mabondeni! Wewe umeshawahi kusikia kwamba Posta kuna watu wamekufa kwa mafuriko? Wanaokufa ni wale wale waliojipeleka wenyewe kwenye mikondo ya maji! Lakini kwa upande mwingine, upumbavu wa serikali usiwafanye watu nao wawe wapumbavu! Kati kati ya jiji kutokuwa na miundombinu isiwe sababu ya kufumbia macho upumbavu unaofanywa na watu wa mabondeni kwa makusudi!

Isemeni hii ishu kwa ukubwa wake.... madhara si mpaka afe mtu... Wa mabondeni wamekufa .. wa posta uchumi umeathirika... tena ukizingatia foleni inakuwa kubwa kuliko kawaida..
 
Mtu na akili zako unakaa kwenye Kingo za mto pita Kawawa Road pale Bonde la kigogo,nyumba zipo kwenye kingo za mto halafu watu kama wale waanze kuilaumu serikali? Wale wanajitakia wenyewe.Kila nikizitazama zile nyumba huwa siwaelewi kabisa wale watu.Serikali nailaumu sehemu moja.Inakuaje maeneo kama yale yawe na huduma za maji.na Umeme?


Sitapenda kubishana kwa hili. Lakini ungejuwa role ya serikali katika makazi na ujenzi wala usingekuja na hoja ya "mtu binafsi" coz ujenzi sio ishu ya mtu binafsi, akijenga mmoja hovyo inaathiri majirani hadi mtaa mzima...
 
BOA Africa wamefunga mapema sababu ya mvua. Kawaida wanafunga saa 10, leo wamefunga saa 9!.
P.
 

watanzania sisi watu ajabu sana!! yaani hatujuagi kuna vitu vinaitwa natural disasters vinatokea duniani kote hivi mafuriko tunachoonga je ikitokea tetemeko kama lile la Nepal tutasemaje? yametokea mafuriko na hadi sasa Mungu katunusuru hatuja poteza hata raia mmoja tunaandika vitu kama hivi. kama ni kujenga ovyo woote tunajenga hovyo hovyo! tusilete siasa katika majanga ya asili mbona migomo inatosha kufanyia siasa!!! natural disasters its shameful!!!
utasikia SERIKALI HIYO ,, HA HA HAHAHA HATA MIMI NISEMAGA SERIKALI
 
recuperation_chaleur_eau_domestique.jpg


sewage-system.jpg
mipango miji hawajaweka
 
Naomba unifahamishe tujadiliane maana Ngalikihinja na BAK sijawaelewa mpaka sasa hoja zao.

Hoja ni kuwa serikali inafanya uzembe kwenye jambo hili... Mafuriko si mara ya kwanza kutokea... Na kila yanapotokea akina nyie maneno yenu ndo haya.... Hii ishu uzembe upo hapa...
1. Mipango miji.... Hii inapelekea kila muda fulani foleni zipo direction moja eg. asubuhi wote kwenda city centre, jioni tunajipanga kurudi majumbani.... Huduma zote muhimu zimejazwa sehemu moja
2. Mitaro almost yote haina 'slop'... Mtaro hauna tofauti na septic tanks... Maana almost kila mtaro maji yanatuama...
3. Mabarabara mengine maji yanatuama.... mfano Akiba, posta mpya, milenium tower, bamaga... etc
4. Watoa vibali vya ujenzi wanaruhusu watu kujenga kwenye njia za maji bila kutoa altenative route ya maji. Kumbuka maji hayazuiliwi bali yanabadilishiwa uelekeo... Mfano wa hili ni apartment nyuma ya Mayfair plaza... Zile zimejengwa kwenye njia ya maji na hawajayapa hayo maji njia mbadala
5. Huduma za kijamii kubwa kubwa zote zipo concentrated city centre.... check soko la kariakoo, mahospitali almost yote, maofisi ya serikali almost yote (wizara, mamlaka etc), mabenki huku pembeni vi-ATM tu....
6. Kambi za majeshi zipo mjini.... JKT, JWT, etc...

Na uzembe mkubwa sana upo hapa...

Kwa TAnzania, siku zote wananchi wanaanza kuishi eneo fulani na baadaye huduma zinafuata....

Nchi zingine, serikali inaingia sehemu kama Goba inapima viwanja inatengeneza njia inapele utilities zote (maji, umeme etc) halafu wananchi mtavuntika tu kwenda...

In Tanzania, hakuna communications kati ya wizara mbalimbali za serikali... Leo hii ujenzi wanamaliza tu kujenga lami, kesho wizara ya maji inabomoa kupitisha bomba...

NB: Usipoelewa hapa, we basii tenaa

CC

Dinazarde
 
Asikudanganye mtu!! hii mvua ina mkono wa CHADEMA! mgomo wa madereva umewashinda sasa wameingia kwenye mvua ilimradi tu watu wasiende makazini!! hivi hawa jamaa tukiwakabidhi nchi hali itakuwaje!?? nchi nzima si itafunikwa na theluji!! hahahahahahahahaaaa.... LOL..

U made my day though tafran ya mvua si ndogo! Wasivyo na haya itasingiziwa CDM ndio inahujumu hadi mvua zinazuia watu kujiletea maendeleo yao kwi kwi kwi!
 
Ghorofa gani? Na nani alitoa kibali?

We kumbe huna data ni ubishani tu unaoendeleza tena usio na tija...
1. Ghorofa lililopo opposite ocean road hospital
2. Ghorofa lililopo kati ya Golden tulip na Seaclif, ambalo Rita Mlaki akiwa naibu waziri wa ujenzi aliling'ang'ania libomolewe lakini hadi leo linatumika
...

Pitia hapa

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/123613-masaki-flats-bounce-back-4.html
 
Tuko page moja Mkuu kamwe siwezi kuitetea hii Serikali dhalimu ambayo ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo mbali mbali nchini kwetu.

Ikiwa mimi natetea upumbavu na wewe unatetea nini kama sio huo huo upumbavu? Serikali ni ya kipumbavu kwa kuwa imeshindwa kutimiza wajibu wa kuokoa maeneo ya kati kati ya mji amabayo yamejengwa vizuri, je hiyo ni sababu tosha ya kuwafanya wananchi nao wawe wapumbavu wa kujenga mabondeni? Unataka kuniambia kati kati ya mji kungekuwa na miundombinu mizuri ndo wapumbavu wasingejenga kwenye mabonde? Unataka kuniambia kungekua na miundo mbinu mizuri kati kati ya mji, ina maana watu wa mabondeni wasingekumbwa na mafuriko? Yaani kwa kuwa serikali ni ya kipumbavu na wananchi nao ndo wawe wapumbavu? By the way, hivi unajua maana ya kulaumu wewe? Mie nalaumu au nawaponda wapumbavu wanaojenga mabondeni? Hivi wewe kwa akili yako na ufahamu wako yale mafuriko ya Jangwani na Kigogo yanatokana na miundombinu mibovu katikati ya jiji? Ushawahi kusikia kati kati ya jiji amekufa mtu kwa mafuriko?
 
Njia ya Masana kuelekea Goba, imekatwa na maji mahali pawili!. Kutoka Tegeta kwenda Mwenge, foleni imeanzia Lugalo, ila kutoka Mwenge kwenda Tegeta, hakuna foleni, nikilinganisha na jana, nilitoka town saa 11 jioni, nikafika home saa 5 usiku, leo nimetoka saa 7 saa hizi niko home!, hadi watoto wanashangaa, dogo anashangaa kumuona dady saa hizi!, hivyo mvua hizi sio kila kitu ni balaa tupu,pia imesaidia!.

Pasco
 
We kumbe huna data ni ubishani tu unaoendeleza tena usio na tija...
1. Ghorofa lililopo opposite ocean road hospital
2. Ghorofa lililopo kati ya Golden tulip na Seaclif, ambalo Rita Mlaki akiwa naibu waziri wa ujenzi aliling'ang'ania libomolewe lakini hadi leo linatumika
...

Pitia hapa

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/123613-masaki-flats-bounce-back-4.html

Kuna mafuriko yoyote yaliyosababishwa na uwepo wa ghorofa hilo? Halafu hujajibu nani alitoa kibali.
 
Sitapenda kubishana kwa hili. Lakini ungejuwa role ya serikali katika makazi na ujenzi wala usingekuja na hoja ya "mtu binafsi" coz ujenzi sio ishu ya mtu binafsi, akijenga mmoja hovyo inaathiri majirani hadi mtaa mzima...
Unasemaje kuhusu wale watu nyumba zao zipo kwenye kingo za mto ambapo mvua kidogo tu inafika kwenye majumba yao? wale watu wasiilaumu serikali wajilaumu wenyewe.
 

Hoja ni kuwa serikali inafanya uzembe kwenye jambo hili... Mafuriko si mara ya kwanza kutokea... Na kila yanapotokea akina nyie maneno yenu ndo haya.... Hii ishu uzembe upo hapa...
1. Mipango miji.... Hii inapelekea kila muda fulani foleni zipo direction moja eg. asubuhi wote kwenda city centre, jioni tunajipanga kurudi majumbani.... Huduma zote muhimu zimejazwa sehemu moja
2. Mitaro almost yote haina 'slop'... Mtaro hauna tofauti na septic tanks... Maana almost kila mtaro maji yanatuama...
3. Mabarabara mengine maji yanatuama.... mfano Akiba, posta mpya, milenium tower, bamaga... etc
4. Watoa vibali vya ujenzi wanaruhusu watu kujenga kwenye njia za maji bila kutoa altenative route ya maji. Kumbuka maji hayazuiliwi bali yanabadilishiwa uelekeo... Mfano wa hili ni apartment nyuma ya Mayfair plaza... Zile zimejengwa kwenye njia ya maji na hawajayapa hayo maji njia mbadala
5. Huduma za kijamii kubwa kubwa zote zipo concentrated city centre.... check soko la kariakoo, mahospitali almost yote, maofisi ya serikali almost yote (wizara, mamlaka etc), mabenki huku pembeni vi-ATM tu....
6. Kambi za majeshi zipo mjini.... JKT, JWT, etc...

Na uzembe mkubwa sana upo hapa...

Kwa TAnzania, siku zote wananchi wanaanza kuishi eneo fulani na baadaye huduma zinafuata....

Nchi zingine, serikali inaingia sehemu kama Goba inapima viwanja inatengeneza njia inapele utilities zote (maji, umeme etc) halafu wananchi mtavuntika tu kwenda...

In Tanzania, hakuna communications kati ya wizara mbalimbali za serikali... Leo hii ujenzi wanamaliza tu kujenga lami, kesho wizara ya maji inabomoa kupitisha bomba...

NB: Usipoelewa hapa, we basii tenaa

CC

Dinazarde

1. Ni Serikali hiyo inajaza uchafu mitaro na kusababisha mitaro kuziba na hivyo kuzuia maji kupita?

2. Uwepo wa maofisi na huduma za jamii sehemu moja, Posta na Kariakoo, (kulingana na maneno yako) kunasababishaje mafuriko Dar es Salaam? Kuna kambi gani ya jeshi (JWTZ au JKT) mjini?

3. Wewe mwananchi unakubalije kujenga au kupewa kibali cha ujenzi sehemu ya njia ya maji?






Dinazarde & BAK
 
Huwa ikinyesha mvua hapo Dar ndio unajua kuwa Dar es Salaam ni kijiji kikubwa kilichopachikwa jina la jiji...

Ni wapumbavu pekee wanaoweza kuitambua Dar es Salaam kama jiji...

Mvua zinanyesha hapo miaka nenda rudi, mafuriko yanatokea miaka nenda rudi...

Lakini hakuna hatua zinazochukuliwa sio na serikali au wananchi...
 
Back
Top Bottom