Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

[Source ni twitter @JamiiForums]


CEZLX1eW8AAKOsj.jpg:large


CEZKNSHW8AAogGT.jpg:large





 
Duh, na bado mvua inaendelea kunyesha! Hatari sana.

Hali ilianza kama utani. Tukapita kidogo kidogo hadi maji yakafunika boneti nzima. Hapo ni Bestbite Dar es Salaam jirani na Eaters Point. Hakupitiki. MANI Amavubi BAK
 

Attachments

  • 1430996918920.jpg
    1430996918920.jpg
    28.5 KB · Views: 977
  • 1430996943669.jpg
    1430996943669.jpg
    31.9 KB · Views: 948
  • 1430996960390.jpg
    1430996960390.jpg
    27.5 KB · Views: 948
  • 1430996988849.jpg
    1430996988849.jpg
    34.2 KB · Views: 939
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Mtu na akili zako unakaa kwenye Kingo za mto pita Kawawa Road pale Bonde la kigogo,nyumba zipo kwenye kingo za mto halafu watu kama wale waanze kuilaumu serikali? Wale wanajitakia wenyewe.Kila nikizitazama zile nyumba huwa siwaelewi kabisa wale watu.Serikali nailaumu sehemu moja.Inakuaje maeneo kama yale yawe na huduma za maji.na Umeme?
Na hiyo barabara iliko juu ya mto na maji yanakatiza juu yake unaisemaje..??
 
Ok Ok.. Ok...
1. Na yale maji yanayojaa Azikiwe karibu na Holiday inn alaumiwe nani..?? Wanaoishi mabondeni..??
2. Na hayo maji kupita juu ya madaraja alaumiwe nani..?? Wanaoishi mabondeni..??
3. Na hayo mabarabara yanayojengwa mitaro isiyo na "slop" alaumiwe nani..?? Wanaoishi mabondeni..??
4. Na hayo maofisi ya serikali kuyajaza yote city centre alaumiwe nani..??? Wanaoishi mabondeni..??

Mambo mengine tuseme kweli... kama ingekuwa utashi wa watu ufanye kazi basi hamna maana ya kuwa na serikali..

1. Mbona wezi wanawakamata..?? Wezi hawana utashi wa kujuwa kuwa wizi hauruhusiwi..???
2. Mbona waharifu wanakamatwa..??? Utashi hawna..???

SERIKALI NI KILA KITU... IKIWA LEGELEGE HAKUNA JAMBO LITAKWENDA...
Why should I care about maofisi ya serikali? Kwani kila wakati wanaokuwa katika majaribu ya maisha ni hao walioko Azikiwe au walioko Mabondeni? Hivi hapa mada ni kubomoka kwa mabarabara na madaraja au madhira wanayopata watu wa mabondeni? Hivi hata huko unakosema kungekuwa na a cery excellent infrastructure, hao watu wa Jangwani, Msimbazi and the like wangeokoka vipi?

Kwamba kama utashi wa watu ungekuwa ufanye kazi basi kusingekuwa na serikali, serikali mara zote itabaki kuwa mwelekezaji na ni mwananchi mwenyewe ndie mwenye wajibu wa kutekeleza maelekezo! Hata humu majumbani mwetu tunaishia tu kuelekezana na kukaripiana; "acha wizi" "acha uhuni" "acha hiki na kile" lakini tunapokuwa wakahidi hata wazazi nao hututupa mkono vinginevyo jela hivi sasa zingejaa watoto waliopelekwa huko na wazazi wao wenyewe baada ya kuwakaripia hili na lile na baada ya kuona hawasikii wanaamua kuwapeleka polisi! Kama bado ni mtoto mdogo, baba ako atakukanya na usiposikia atakutandika hadi mikwaju lakini ukishakuwa mtu mzima ataishia kukukanya na usiposikia, atakauacha kama ulivyo! Wale watu wa mabondeni ni mijitu mizima na akili zao na wote wanafahamu nini kitawakuta lakini tatizo huwa wanafanya mahesabu, kwamba kati ya siku 365 za mwaka, ni chini ya siku 7 ndizo watahangaika!
 
Hali ilianza kama utani. Tukapita kidogo kidogo hadi maji yakafunika boneti nzima. Hapo ni Bestbite Dar es Salaam jirani na Eaters Point. Hakupitiki. MANI Amavubi BAK

Mpwa leo kama upo uwezekano si pa kutoka nyumbani.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Na hiyo barabara iliko juu ya mto na maji yanakatiza juu yake unaisemaje..??
Sasa ikiwa unaamini serikali ni stupid kwahiyo na mwananchi mwenyewe aendelee kuwa stupid? Yaani kwavile serikali haijajenga miundombinu ndo basi tena na mimi nijenge tu mabondeni?! Don't you think hapo mwananchi ndo angetakiwa kuwa smart zaidi kwa kuona this government is very stupid so I need to learn how to protect myself! Hivi unaweza kupita eneo la hatari ukiwa umeongozana na mtu unayejua kwamba hana msaada kwako?
 
Why should I care about maofisi ya serikali? Kwani kila wakati wanaokuwa katika majaribu ya maisha ni hao walioko Azikiwe au walioko Mabondeni? Hivi hapa mada ni kubomoka kwa mabarabara na madaraja au madhira wanayopata watu wa mabondeni? Hivi hata huko unakosema kungekuwa na a cery excellent infrastructure, hao watu wa Jangwani, Msimbazi and the like wangeokoka vipi?

Kwamba kama utashi wa watu ungekuwa ufanye kazi basi kusingekuwa na serikali, serikali mara zote itabaki kuwa mwelekezaji na ni mwananchi mwenyewe ndie mwenye wajibu wa kutekeleza maelekezo! Hata humu majumbani mwetu tunaishia tu kuelekezana na kukaripiana; "acha wizi" "acha uhuni" "acha hiki na kile" lakini tunapokuwa wakahidi hata wazazi nao hututupa mkono vinginevyo jela hivi sasa zingejaa watoto waliopelekwa huko na wazazi wao wenyewe baada ya kuwakaripia hili na lile na baada ya kuona hawasikii wanaamua kuwapeleka polisi! Kama bado ni mtoto mdogo, baba ako atakukanya na usiposikia atakutandika hadi mikwaju lakini ukishakuwa mtu mzima ataishia kukukanya na usiposikia, atakauacha kama ulivyo! Wale watu wa mabondeni ni mijitu mizima na akili zao na wote wanafahamu nini kitawakuta lakini tatizo huwa wanafanya mahesabu, kwamba kati ya siku 365 za mwaka, ni chini ya siku 7 ndizo watahangaika!

Hapo kwenye BOLD ... NDO TATIZO LAKO LILIPO.... If you you should care then una tatizo
 
Kel-dizo kama una picha au ukipata tupia kwa ajili ya kumbukumbu. Asante
 
Last edited by a moderator:
Hali ilianza kama utani. Tukapita kidogo kidogo hadi maji yakafunika boneti nzima. Hapo ni Bestbite Dar es Salaam jirani na Eaters Point. Hakupitiki. MANI Amavubi BAK

Duh! Sasa hapo mmetokaje? Mmefanikiwa kuvuka kweli?
 
Last edited by a moderator:
Na kati kati ya mji kunakokuwa na mafuriko yale maghorofa yalijengwa kiholela na Wananchi? Acheni kutetea hoja uzembe na ukosefu wa sera? Kule msasani kwenye mafuriko mbona zile nyumba zimejengwa kwa kibali cha Serikali na bado kuna mafuriko? Ni aje?

Hivi wewe ulielewa kweli nilichoandika?

Wananchi ni kina nani kwa mtazamo wako? Manake nachelea kuamini kuwa kwako wewe wananchi ni "walalahoi" wa Manzese, Tandale kwa Mtogole/kwa Tumbo, Kimara, etc.

Nyumba zipi za Msasani zimejengwa kwa kibali cha Serikali? Unazifahamu?
 
Hapo kwenye BOLD ... NDO TATIZO LAKO LILIPO.... If you you should care then una tatizo
Siwezi ku-care kama ambavyo siwezi ku-care kwa mtu ambae amejenga mabondeni makusudi halafu niilaumu serikali wakati mwenyewe ana akili zake timamu na anafahamu kwamba huu ni mkondo wa maji halafu bado anajenga!
 
sasa ndo inaharibu...viongozi wa kisiasa hupebda kusema ni wapiga kura wetu hao hawawezi kuhama
 
Back
Top Bottom