TANZIA Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo cha ndugu yetu Mtanzania mwezetu Michael a.k.a Mike kilichotokea Afrika Kusini

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,141
b8c10902-b431-4036-98cf-4fa2abb03a46.jpg
🇿🇦🇿🇦 MZEE BABA🇿🇦🇿🇦

Ndugu watanzania mabaharia watafutaji na wanaharakati.......

Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo cha ndugu yetu manzania mwezetu Michael aka Mike......

Mike Tanzania anatokea kinondoni......

Ndugu watanzania mike aliamisha makazi yake kutoka Tanzania na kuelekea Mozambique.

Kipindiki Mike anaishi Mozambique alifanya biashara na Mtanzania mwezetu wa kuitwa MISHELI.

MISHELI anaishi Johannesburg south Africa maeneo ya My Fay

Ktk biashara Mike alikuwa akimdai mishali pesa. Kutokana na MISHELI kushindwa kulipa deni ikabidi amwambie Mike amfate South Africa ili ampe gari wamalizane.

Kilicho tokea Mike alitoka Mozambique na kuelekea South Africa na walikutana na MISHELI. Baada ya muda mchache mike hakupatikana tena kwenye simu......

Tumeanza zoezi la kumtafuta mike Sasa yapata siku ya nne hapa Johannesburg. Ndugu watanzania Leo asubuhi ya tarehe 18/3/2024 tumefanikiwa kupata mwili wa mike katika mochwari ya hilbrow iliyopo Johannesburg.

Mike ameuwawa Kwa kupigwa bunduki kutokana na details za mochwari mwili wa mike umekutwa Johannesburg twist / plain street tarehe 11/3/2024

......ANAYEDAI KAVUTWA FROM THERE KAULIWA .......

HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WATANZANIA WOTE.,..

CASE ISHAFUNGULIWA.,.......

IMEANDIKWA NA MOHAMED TAIBALH MSANGI

TAREHE 18/3/2024

MIKE NA MISHELI WALISOMA WOTE SHULE YA MSINGI

MIKE ALIONDOKA TANZANIA MWAKA 1999
 
Anaandika Mohamed Msangi, Mtanzania anayeishi SA
__________
Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo cha ndugu yetu, Mtanzania mwezetu Michael aka Mike mzaliwa wa Kinondoni. Mwaka 1999 Mike alihamisha makazi yake kutoka Tanzania kuelekea Mozambique akijishughulisha na biashara mbalimbali zikiwemo za magari na electronics.

Alifanya biashara na Mtanzania mwezetu wa kuitwa Misheli, aliyekua anaishi Johannesburg SA maeneo ya MyFay. Mike na Misheli wamesoma pamoja shule ya msingi Kumbukumbu, Kinondoni, na Mike ndiye aliyemsaidia Misheli kuja SA.

Katika biashara zake Mike alikuwa akimdai Mishali pesa, lakini Misheli alishindwa kulipa kwa muda mrefu, ikabidi amwambie Mike amfate South Africa ili ampe gari wamalizane. Mike akakubali. Akatoka Mozambique na kufika South Africa na wakakutana na Misheli.

Wakakabidhiana gari na kumaliza deni. Lakini baada ya muda mchache Mike hakupatikana tena kwenye simu. Baadhi ya Watanzania tunaoishi SA tulikua na miadi ya kukutana nae kabla hajarudi Mozambique. Tulipompigia mchana alisema yuko na Misheli lakini baadae akawa hapatikani. Tulipompigia Misheli akasema waameshaachana.

Tukaanza zoezi la kumtafuta hapa Johannesburg. Kwa zaidi ya wiki 1 tulimtafuta bila mafanikio, hadi asubuhi ya tarehe 18/3/2024 tulipoupata mwili wake katika mochwari ya Hilbrow iliyopo Johannesburg. Ripoti inaonesha Mike aliuwawa kwa kupigwa bunduki. Mwili wake ulikutwa Twist/Plain street, jijini Johannesburg tar.11/3/2024.

Mamlaka jijini Johannesburg zilichukua mwili na kuuweka Mochwari hadi tar.18 March tulipoukuta. Polisi wanamshikilia Misheli kwa tuhuma za mauaji ya Mike. Inadaiwa kuwa Misheli alimkabidhi Mike gari halafu akatuma vijana wampige risasi na kumpora gari hiyo wairudishe kwake.

Hivi ndivyo binadamu tulivyokosa utu. Fikiria rafiki yako mmesoma wote shule ya msingi. Anatangulia kwenda nje ya nchi, baadae anakusaidia na wewe uende. Unafika lakini unafanya biashara unakwama, anakukopesha mtaji. Unashindwa kumlipa kwa wakati. Mnakubaliana umpe gari. Baadae unatuma vijana wamuue ili wachukue gari. Huu ni zaidi ya unyama. Halafu tukikutana huko nje mnasema diaspora hatupendani. Tutapendanaje kwa hali hii? Rest easy Mike.!
 
Back
Top Bottom