Ujumbe kwa Rais Samia; Mwalimu Mkuu wa Kitinku awafukuza shule watoto wa Mzee Salum kwa sababu wanakwenda kuswali siku ya ijumaa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,142


Je Sheria ya nchi inasemaje ? soma hapo chini 👇

WhatsApp Image 2024-02-17 at 07.06.00.jpeg


ASalam Alaykum,

Hongera nyingi sana kwa ndugu yetu wa imani ya kiislamu kwa jihad kubwa aliejitolea wa ujasiri mkubwa kuongea hayo bila oga na hatimaye natija yake ameamsha usingizi hisiya ya siyo ya viongozi na Mashekh wetu tuu bali hata viongozi wetu wa serikali kuwa kutukumbusha na nyaraka ilyotolewa mwaka 1999. na wizard ya elimu...hatuwezi kujua kiasi ya malipo yake kubwa atapewa na Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala. Pia kuwa zindua viongozi wa dini na Mashekh wetu kuweza kutambua makosa yetu kotika kujua haki zetu nyingi tulizo nazo katika Serikali yetu ya Mungano wa Tanzania.

Alhamdulillah.. sasa wanafunzi wa kiislamu wengi watapewa haki yao ya kutimiza ibada sala ya ijuma na sasa itakuwa ni thawabu ja'ariyah kwa huyo bwana.. hata siyo kiongozi wala Sheikh. Bali alikerwa na kuchukua uamuzi binti zake wasiende shule ili waende kutimiza ibada ya salaa ya ijumaa.. kweli Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala amempa malipo makubwa ya jitihada zake kupigania haki za wanafunzi wote wapate ruhusa ya kutimiza ibada ya salaa za ijumaa...Ameen

Kweli Alhamdulillah ametupa darasa kubwa sana...tusiogope kusema ukweli kunusuru Dini la
Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala na yeye ndie atawalipa .. Ameen
 
Ijumaa ni siku ya kazi. Mzee aache kuwafanya wanawe wawe watoro.

Kwa nilivyoelewa mimi Mzee anataka ijumaa watoto wake wasiende shule siku nzima. Huku kanuni zinasema ijumaa muda wa waislamu kwenda ibada ni saa sita mchana mpaka saa nane mchana
 
Mwalimu mkuu bogas.
Kwamba ye hajui huu utaratibu wa ibada shuleni?
Na walimu kama huyu ndio wasimamizi wa uchaguzi. Ndio maana nchi ina laana kama chao cha walimu na chama chao cha CCM.
Pumbavu zake.
 
Kwa hiyo anawafukuza shule watoto wasipate Elimu yaani Mwalimu anaona sawa watoto kukosa Elimu swala la Ijumaa si masaa kadhaa tu kwani kuna shida gani...
 
Mwalimu mkuu bogas.
Kwamba ye hajui huu utaratibu wa ibada shuleni?
Na walimu kama huyu ndio wasimamizi wa uchaguzi. Ndio maana nchi ina laana kama chao cha walimu na chama chao cha CCM.
Pumbavu zake.
Nafikiri shida hapo mzee anataka ijumaa wasiende kabisa shule na mwongoz ni kuwa ijumaa saa 6-8 ni muda wa ibada, nakumbuka wakati tunasoma kulikuwa na kipidni cha dini muda huo huo. Sisi wengine tulikuwa tunaishia uwanjani kucheza kitenesi na bado tumekuwa raia wema tu kama wengine.
 
View attachment 2906550

Je Sheria ya nchi inasemaje ? soma hapo chini 👇

View attachment 2906553

ASalam Alaykum,

Hongera nyingi sana kwa ndugu yetu wa imani ya kiislamu kwa jihad kubwa aliejitolea wa ujasiri mkubwa kuongea hayo bila oga na hatimaye natija yake ameamsha usingizi hisiya ya siyo ya viongozi na Mashekh wetu tuu bali hata viongozi wetu wa serikali kuwa kutukumbusha na nyaraka ilyotolewa mwaka 1999. na wizard ya elimu...hatuwezi kujua kiasi ya malipo yake kubwa atapewa na Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala. Pia kuwa zindua viongozi wa dini na Mashekh wetu kuweza kutambua makosa yetu kotika kujua haki zetu nyingi tulizo nazo katika Serikali yetu ya Mungano wa Tanzania.

Alhamdulillah.. sasa wanafunzi wa kiislamu wengi watapewa haki yao ya kutimiza ibada sala ya ijuma na sasa itakuwa ni thawabu ja'ariyah kwa huyo bwana.. hata siyo kiongozi wala Sheikh. Bali alikerwa na kuchukua uamuzi binti zake wasiende shule ili waende kutimiza ibada ya salaa ya ijumaa.. kweli Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala amempa malipo makubwa ya jitihada zake kupigania haki za wanafunzi wote wapate ruhusa ya kutimiza ibada ya salaa za ijumaa...Ameen

Kweli Alhamdulillah ametupa darasa kubwa sana...tusiogope kusema ukweli kunusuru Dini la
Mwenyeezi Mungu Subhana Wataala na yeye ndie atawalipa .. Ameen
Acha upuuzi wako, huyo mjinga mwenzio kwenye video aliyorekodi mwenyewe anaokana akiwa ameshika barua ya wito kutokana na utoro wa watoto wake.
Kwa hiyo watoto wakiislam ktk hiyo shule ni hao wawili tu, kwa hiyo unataka hao watoto siku ya ijumaa wasiende shule,jms na jmpl? Mbona kwa ajirq ijumaa mko maofisini na hamfungui midomo?
Mshauri huyo jamaa yako awapeleke shule ya kiislam lkn shule za serikali zinaendeshwa kisheria.

Analalamika umbali wa kutoka na kwenda shule hilo linahusiana vipi na mkuu wa shule? Huyu chizi kijijini kwake kuna shule lkn kutokana na ujinga wake kagombana na walimu na kisha kuwaamisha watoto wake na kuwapeleka shule iliyoko kilomita 5.
Huyu ndo wale wazazi wapuuzi wanaojificha kwenye kiburi cha dini na kuzalisha watoto wa kwenda kujiunga na Alishabab.
Kama hili jambo likifuatiliwa kwa undani utakuta huyu mzazi anawanyanyasa sana familia yake.
Hawa ndo wale wazazi ambao wanawanyima watoto wao wakike haki ya elimu na baadae kuishia kuwaingilia kimwili
 
Kwa hiyo anawafukuza shule watoto wasipate Elimu yaani Mwalimu anaona sawa watoto kukosa Elimu swala la Ijumaa si masaa kadhaa tu kwani kuna shida gani...
Huyo mwalimu sio chizi, tungesikia na yeye upande wake. Pia huyo mzee watoto wake ndio waislamu pekee hapo shule? Kwanini yeye tu ndio aambiwe aondoke na wanae?
 
Huyo mwalimu sio chizi, tungesikia na yeye upande wake. Pia huyo mzee watoto wake ndio waislamu pekee hapo shule? Kwanini yeye tu ndio aambiwe aondoke na wanae?
Naona Vijijini watu wanahamasishwa kupeleka watoto shule pana kijiji niliwahi pita huko Longido ndani ndani pana watu wanatoa Elimu kwa wazazi ili wawaruhusu watoto wao wajiunge na shule na vitu vyote wanapewa bure kwa hiyo sababu kuwafukuza shule watoto ajatumia busara kabisa mimi sijazungumzia mambo ya dini nazungumzia haki ya watoto kupata Elimu.
 
Naona Vijijini watu wanahamasishwa kupeleka watoto shule pana kijiji niliwahi pita huko Longido ndani ndani pana watu wanatoa Elimu kwa wazazi ili wawaruhusu watoto wao wajiunge na shule na vitu vyote wanapewa bure kwa hiyo sababu kuwafukuza shule watoto ajatumia busara kabisa mimi sijazungumzia mambo ya dini nazungumzia haki ya watoto kupata Elimu.
Ukihamasishwa uje shule haina maana kuwa uje kwa terms zako. Ukikiuka taratibu utafukuzwa. Huwezi tu kuamua mimi kila jumatano watoto wangu hawaji wataenda kuchungq ng'ombe.
 
Huyo ni mwakilishi wa jamii nyingi za wananchi wenye changamoto za maisha.

Mwl mkuu yupo sawasawa kabisa akisimamia maendeleo ya wanafunzi wake, Mzazi kakosa kabisa mbinu mbadala ya kuhakikisha watoto wake wanasoma kwa urahisi .ameshindwa sababu ya mahangaiko ya maisha.

Watoto kwa jinsi wanavyotembea umbali mrefu hqkika hamu ya shule wanayo.
Wapo wafanyakazi mijini imewalazimu kupeleka watoto wao kwenye shule za BWENI ili tu changamoto za maisha na shule kwa watoto ziende pamoja.

Kwa huyu mzazi kwa walio na mapenzi mema wampatie BAISKELI aweze kuwapeleka watoto wake shule asubuhi. Wawahi.

Aelimishwe Ijumaa afuate maelekezo ya wizard.
 
Ukihamasishwa uje shule haina maana kuwa uje kwa terms zako. Ukikiuka taratibu utafukuzwa. Huwezi tu kuamua mimi kila jumatano watoto wangu hawaji wataenda kuchungq ng'ombe.
Umetoa mfano wa hovyo mtu na imani yake anazungumzia Ijumaa anakwenda kuswali wewe unazungumzia kuchunga ng'ombe wacha tuishie hapa naona unashika kete yeyote..
 
Back
Top Bottom