Kuajiriwa ni utumwa

Kuajiriwa ni utumwa

HIVI UTUMWA TUNAUPA TAFSIRI YA UPANA UPI HASA? HATA KWENDA BENKI KUTAFUTA MKOPO ILI UANZISHE KIWANDA CHAKO NI UTUMWA KWA NAMNA NYINGINE ( JAMAA YANGU ALIMPA MTU TAX AMLETEE PESA KWA SIKU,SIKU MOJA MWENYE TAX ALILOA MVUA WAKATI ANAENDA KANISANI NA FAMILIA YAKE,HALAFU TAX DREVA KAFIKA KANISANI FRESH NA MKEWE KWA KUTUMIA TAX YA JAMAA), UKIUANGALIA UTUMWA VIZURI, UTAONA NI KIKUNDI KIDOGO SANA DUNIANI NDO KIMEONDOKA KWENYE UTUMWA WA JUMLA WA KUONEKANA, WA KUTOONEKANA.
Stori hii haina mashiko yoyote... Kwa hiyo mwenye tax anautumwa gani hapo?

Anajua pesa yake iko pale pale.
 
Katika 10 unawaona wamefanikiwa kwenye ujasiriamali.... kuna 1000 waliochemka

Kuna wanaoamini kuna raha ya milele nje ya ajira, kumbe huko ndio kunataka bidii x 10 ya ajirani.

Tunao wengi tu waliotoka kwenye nje ya ajira, halafu wamerudi

Cha muhimu jua wapi unaweza ukavumilia mateso yake.

Ila ukitaka kuwa bilionea, ni ngumu kuwa hivyo kwenye ajira... ila kama ni maisha tu mazuri, kwenye ajira unaweza ukayapata
 
Ulishawahi kufikiria kuwa, kila mmoja akitaka kujiajiri itakuwaje? Yaani asiwepo aliyeajiriwa na mwingine, unaona huo uwezekano?
Yaani kila mtu afanye kazi yake mwenyewe bila kusaidiwa na mtu mwingine, inawezekana hiyo?
Ndo maana nikatoa bandiko kimtazamo wangu, najua haiwezekani. Lazima kuwe na master and servant
 
Ukielewa Code za mtaa Hustle inakua rahisi sanaaaaaaaa me niliacha kazi baada ya kupewa code na mwanangu alieishia form 2 kwa kukosa ada ila kwa sasa ni Fogo hapa mbeya na deal zake sio kitoto
Hakika sema huwa mnaziweka siri sana hizo code
 
Ngoja nikupe siri moja hivi ambayo itakusaidia ili usiaibike mtaani na familia yako kukudharau.
Tengeneza wazo la biashara au mradi ambao unaona unaendana na kipaji chako na moyo wako unapenda kufanya.
Kisha anza kujitangaza polepole na kutoa huduma wakati bado umeajiriwa.
NB:
Usiache kazi kabla biashara haijasimama,inachukua miaka mingi biashara kujenga jina na kuzoeleka ili iwe stable
Shukran mkuu nitalifanyia kazi
 
Sema kweli hiki kitu hata me kinaniwazisha sana, kwa mshahara wangu huu hata nikisema nijibane siwezi pata nauli ya kwenda Dubai na kula maisha kwa wiki. Wakati nina wana kibao walioko kwenye business zao mjini sehemu kama Dubai na China wanaingia karibu kila mwezi . Kuna siku nitafanya maamuzi magumu inshallah
Kweli mkuu...
 
Sema kweli hiki kitu hata me kinaniwazisha sana, kwa mshahara wangu huu hata nikisema nijibane siwezi pata nauli ya kwenda Dubai na kula maisha kwa wiki. Wakati nina wana kibao walioko kwenye business zao mjini sehemu kama Dubai na China wanaingia karibu kila mwezi . Kuna siku nitafanya maamuzi magumu inshallah
Endelea kujidanganya sana, tuliza matako yako kwenye hiyo ajira yako tena ukae kwa kutulia ukimshukuru Mungu. Acha mihemko ya kitoto, usikae ukaona maisha ya watu fulani ukadhani ndivyo yalivyo.
By the way KUJIAJIRI si jambo ambalo linaweza kufanywa na kila mtu, ungekua una uwezo au kipaji cha kujiajiri nikuambie tu ungekuwa umejiajiri zamani na watu wangeona uwezo wako tangu zamani.
Vijana wa Tz mnapenda sana kujidanganya kwa kusikiliza maneno ya watu mwisho mnaishia kwenye kufanyiwa mambo mabaya ya aibu na kujihusisha na uhalifu na ushirikina.
 
Endelea kujidanganya sana, tuliza matako yako kwenye hiyo ajira yako tena ukae kwa kutulia ukimshukuru Mungu. Acha mihemko ya kitoto, usikae ukaona maisha ya watu fulani ukadhani ndivyo yalivyo.
By the way KUJIAJIRI si jambo ambalo linaweza kufanywa na kila mtu, ungekua una uwezo au kipaji cha kujiajiri nikuambie tu ungekuwa umejiajiri zamani na watu wangeona uwezo wako tangu zamani.
Vijana wa Tz mnapenda sana kujidanganya kwa kusikiliza maneno ya watu mwisho mnaishia kwenye kufanyiwa mambo mabaya ya aibu na kujihusisha na uhalifu na ushirikina.
Naelewa si rahisi ndio maana nikayaita maamuzi magumu, ntaenda hatua kwa hatua ila kitu cha kuajiliwa maisha yangu yote itakuwa failure maishani mwangu serious
 
Endelea kujidanganya sana, tuliza matako yako kwenye hiyo ajira yako tena ukae kwa kutulia ukimshukuru Mungu. Acha mihemko ya kitoto, usikae ukaona maisha ya watu fulani ukadhani ndivyo yalivyo.
By the way KUJIAJIRI si jambo ambalo linaweza kufanywa na kila mtu, ungekua una uwezo au kipaji cha kujiajiri nikuambie tu ungekuwa umejiajiri zamani na watu wangeona uwezo wako tangu zamani.
Vijana wa Tz mnapenda sana kujidanganya kwa kusikiliza maneno ya watu mwisho mnaishia kwenye kufanyiwa mambo mabaya ya aibu na kujihusisha na uhalifu na ushirikina.
Hahaha wanaamini stori za vijiweni
 
Na huu ndo ukweli Mchungu...

Silali usiku na mchana nafikiria namna ya kutoka kwenye huu mtego.
View attachment 3641392

Yaani asubuhi ya leo niende tena kufanya jambo lile lile mpka nitakapo fika miaka 60.

Hapana kwa kweli, mimi sio mmatumbi mjinga.. I need to wake the *** up and find something worth dying for.

Ndugu zangu ambao mpo complacent na kuajiriwa hivi huwa mnajisikiaje?
Maisha yenyewe ni utumwa tu
 
Sijamaanisha kila mtu aji ajiri.. Haiwekezekani

Stori hii haina mashiko yoyote... Kwa hiyo mwenye tax anautumwa gani hapo?

Anajua pesa yake iko pale pale.
anayehangaika na matengenezo ya gari huwa ni nani vile? Angalia, gari ununue wewe, matengenezo ufanye wewe, tax driver akuletee 10,000/ baada ya kukata hela yake aliyopata kwa siku, hata akipata laki tatu, yako kama mmiliki wa gari ni 10,000/. Bagosha, hapo nani mtumwa??
 
Kila mtu akijiajiri nani atafanya kazi kwa mwenzake?

Umewaza kuhusu walimu? Madaktari? Polisi? N.k
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom