Je, ni uchawi au saikolojia?

Je, ni uchawi au saikolojia?

Kwa huu ujinga wako umezaliwa na kukulia dar na nakushauri ukienda vijijini kuwa muungwana.uchawi upo tena kuna watu kazi zao wanalipwa kwa kwa ajili ya kuroga wengine wafe,wengine wanakufanya uwe chizi uteseke.Mimi binafsi ndugu zangu nilishuhuduwa wakirigwa na kuwa machizi na sio swala la kuhadithiwa
 
Nakupa hii CODE na uizingatie

Kitu chochote ambacho ni IMANI basi ujie ni kitu ambacho HAKIPO au huna UHAKIKA nacho………. So Uchawi na vitabu ulivyo vinukuu vyote ni IMANI

Kitu chochote ambacho KIPO hakiwezi kuwa IMANI…….. Huwezi kusema NAAMINI Trump ni Rais wa Marekani au kusema naamini kuna Bahari ina maji mengi kwasababu ipo na hawezi kuwa IMANI
Ahaa sawa
So kua na imani ni vibaya?
Ukisema NAAMINI chumba namba 5 kina Nyoka…… kikifunguliwa ikawa yupo huwezi tena kusema UNAAMINI kuna nyoka, utasema chumba kina nyoka sababu ni uhalisia(fact)
Lakini mwanzoni ulisema unaamini kwanza sio?
Then baadae ndiyo ukathibitisha ukasema nyoka yupo baada ya kumuona right?

Niambie kuhusu neno (Imani) kama hutojali bro
 
Irrelevant, huwezi kueleza inachokifanya wewe ni tapeli tu.
Narudia kama unaweza kaniroge. Najua huwezi ......nitakuuliza uthibitishe ulivyoniroga na hautaweza.
Mimi nakupa logic ya jinsi ulimwengu unavyoenda, wewe unataka kunifanya mimi mganga wako wa kienyeji?

Nenda katafute wachawi huko vijijini kwa bibi zako, uwaambie haya.
 
Kwa huu ujinga wako
Maneno yako yote yanaweza kukosa maana kama tu kila una pochangia mada utaanza ku m attack mleta mada kama hivi
umezaliwa na kukulia dar na nakushauri ukienda vijijini kuwa muungwana.uchawi upo tena kuna watu kazi zao wanalipwa kwa kwa ajili ya kuroga wengine wafe,wengine wanakufanya uwe chizi uteseke.Mimi binafsi ndugu zangu nilishuhuduwa wakirigwa na kuwa machizi na sio swala la kuhadithiwa
Sawa uchawi upo na unaweza kufanya mtu akawa chizi kama unavyosema

Vipi hakuna namna huo uchawi ukatumika kwa manufaa zaidi?
 
Mimi nakupa logic ya jinsi ulimwengu unavyoenda, wewe unataka kunifanya mimi mganga wako wa kienyeji?

Nenda katafute wachawi huko vijijini kwa bibi zako, uwaambie haya.
Ulimwengu unaenda hata kwa ulaghai na uongo.
Huwezi kuwa mganga wangu kwani siamini katika uchawi kama wewe
Huko kijijini hakuna uchawi bali walaghai na matapeli waliofichama ktk kivuli cha uchawi.
 
Ulimwengu unaenda hata kwa ulaghai na uongo.
Huwezi kuwa mganga wangu kwani siamini katika uchawi kama wewe
Huko kijijini hakuna uchawi bali walaghai na matapeli waliofichama ktk kivuli cha uchawi.
Kweli una akili ndogo sana, kwamba kwa sababu tu wewe Edson huamini, basi mambo hayapo? Hiyo inaitwa main character syndrome unadhani ulimwengu unazunguka kwenye akili yako tu hiyo ndogo.

Baki na huo mtazamo wako wa kizamani.
 
Kweli una akili ndogo sana, kwamba kwa sababu tu wewe Edson huamini, basi mambo hayapo? Hiyo inaitwa main character syndrome unadhani ulimwengu unazunguka kwenye akili yako tu hiyo ndogo.

Baki na huo mtazamo wako wa kizamani.
Wewe mwenye akili nyingi thibitisha uwepo wayo.
 
Eeh buda hii mada iko moto kweli. Mimi naona uchawi ni kama imani tu, mtu akiamini kitu kinafanya kazi kwake. Lakini pia nimeona watu wakifanya mambo ya ajabu ambayo saikolojia pekee haiwezi kueleza, sijui hapo ni nini 😅
 
Eeh buda hii mada iko moto kweli. Mimi naona uchawi ni kama imani tu, mtu akiamini kitu kinafanya kazi kwake. Lakini pia nimeona watu wakifanya mambo ya ajabu ambayo saikolojia pekee haiwezi kueleza, sijui hapo ni nini 😅
Hii comment yako nimesoma kama vile umeandika ukiwa na haraka kama huyo wa kwenye avatar 😅

Licha ya kuona mambo ya ajabu ambayo saikolojia pekee haiwezi kueleza vipi una amini kwenye uchawi?
 
Inapokuja mada ya uchawi huwa kuna kuchanganya kati kuwepo ama kutokuwepo huo uchawi, nguvu ya huo uchawi ama manufaa ya huo uchawi, na imani kuhusu uchawi hapa afrika kulinganisha na jamii zengine hasa wazungu.

Kwa mfano unakuta mtu anapinga kuwepo uchawi halafu yale madhara yenye kuhusishwa na uchawi husema ni suala la saikolojia tu, au tabia tu za mtu mwenyewe ila si uchawi, lakini mtu huyo huyo anajenga hoja kwamba kama kweli uchawi upo mbona hatuoni hiki na kile kuonyesha kuwa kama uchawi ungekuwepo basi ungetumika kuleta athari ama kufanikisha hivyo vitu.

Hapo utaona kumechanganywa kati ya uhalisia wa uwepo wa uchawi na nguvu ama manufaa ya huo uchawi, sidhani kama ni sahihi kuweka vigezo kwamba lazima huo uchawi uweze kufanya hiki na kile ndio tukubali kuwa kweli huo uchawi upo wakati hata hayo mengine yote yaliyokuwepo yenye kuhusishwa na uchawi(iwe kwenye tiba, mali, kesi, mapenzi n.k) yanakataliwa kwa sababu hakuna uthibitisho, sasa huko kuweka vigezo kwamba kama uchawi ungekuwepo kungetakiwa kuwe na hiki na kile sioni kama ni hoja ya msingi naona ni kuchanganya uwepo wa uchawi wenyewe na nguvu ya huo uchawi.
 
hahaa usipomuamini Mungu uchawi nao utakushinda tu

hivyo vitu viwili vinalandana sana
Ila kuna utofauti kwa sababu uchawi hauishii kwenye kuamini tu wakati mwengine watu wanategemea kuona matokeo halisi ya kile kilichofanyika na ndio maana watu huamini Mungu ila akiwa na tatizo hukimbilia kwa mganga, kule anafuata matokeo na si imani.

Ndio maana wapo wasioamini Mungu ila wanaamini mizimu, uchawi, psychic power.
 
Unajua mkanganyiko uko wapi mkuu ni kwamba ukiacha kuamini hizo issue za uchawi wala hutouona kabisa kwenye maisha yako
Huoni hapo kama kuna walakini?

Kama ipi share basi tujifunze
Ni sawa na mtu kutotaka kusikiliza maneno ya watu kuhusu mkewe kuchepuka hali ambayo itamfanya hatoona huko kuchepuka kwa mkewe.
 
Ni sawa na mtu kutotaka kusikiliza maneno ya watu kuhusu mkewe kuchepuka hali ambayo itamfanya hatoona huko kuchepuka kwa mkewe.
Mkuu huu mfano haufanani mbona 🤣

Maana yangu unapoanza kuamini ni tayari umeruhusu ubongo wako ukuundie mapicha picha na marue rue
 
Back
Top Bottom